Mr. Mtsimbe nakubaliana nawe sana kwa uliloanzisha, nami nipo mbioni kuwasiliana nawe na kujiunga na TPN kama mmojawapo wa Diaspora kwani baadhi yetu tunataka kuja nyumbani sasa.
Na nilikujua toka wakati wa Mnazi Mmoja Applied Computer nikiwa mwanafunzi wako.
Nakutakia kila la kheri na nimekuwa nafuatilia maendeleo ya TPN toka wakati bado kamati ya uanzishwaji.......hongera kwa juhudi zako binafsi na wale wote waliofanikisha ikafikia hapo.
Tupo pamoja, na tunakuja.........!!!!!!
huyu Mwenzetu Naona Kafyatuka Tu, Taratibu Bwana Mdogo.
Mr. Mtsimbe nakubaliana nawe sana kwa uliloanzisha, nami nipo mbioni kuwasiliana nawe na kujiunga na TPN kama mmojawapo wa Diaspora kwani baadhi yetu tunataka kuja nyumbani sasa.
Na nilikujua toka wakati wa Mnazi Mmoja Applied Computer nikiwa mwanafunzi wako.
Nakutakia kila la kheri na nimekuwa nafuatilia maendeleo ya TPN toka wakati bado kamati ya uanzishwaji.......hongera kwa juhudi zako binafsi na wale wote waliofanikisha ikafikia hapo.
Tupo pamoja, na tunakuja.........!!!!!!
Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu, napenda kuwapongeza TPN kwa kualika wana JF ktk umoja wao. Nafikiri ukijiunga na Tpn au umoja wowote ule ni opportunite kubwa ya kujiendeleza wewe mwenyewe na Taifa kwa ujumla. Nadhani ndani ya TPN kuna wataalamu mbalimbali na wazoefu wa Viwanda, usafiri, banks, ustawi wa jamii, uongozi bora, mikataba, biashara za nje na ndani nk. Ila nitoe angalizo kidogo kwani tuna profesional societies nyingi Tz lakini hazina msaada sana hasa kwa mwananchi wa kawaida. Hebu tumieni wazoefu ndani ya TPN kusaidia kupunguza kero hapo bongo. Kuna kero ambazo nahisi kama Society TPN mnaweza kujaribu kuzishughulikia zikamsaidia hata mtanzania wa kawaida, mfano usafiri mkakopa mabasi makubwa sio vipanya from outside na kumanage ipasavyo si mtakuwa mmesaidi while nanyi mkiingiza kipato. Who knows mnaweza kujidevelop na kuanzisha even kiwanda in the future. Ndio watu wanavyofanya nchi za wenzetu. Hebu jaribu kuafatilia history ya makampuni makubwa duniani yalianza na yameendelea vipi. Wazo langu binafsi
Once again Thanks TPN
F2S
Na wewe unahitajika leta mchango wake,
Remember, Mjenga nchi ni mwananchi. Njoo tuungane na TPN tujenge nchi, mawazo yako ni bomba sana!
Njimba
F2S,
Tuwape mda tu hawa TPN labda hapo mbeleni watatuonyesha mambo makubwa nafikiri changamoto zako wataziona.
Sanctus,
I think we have reached somewhere, I am now accepting your "Karibu" it is time for action, I am on my way to TPN's office to register myself. I believe that Mjenga Nchi ni Mwananchi.
We will discuss all TPN's shortfall live. However, not under this name. When is the next members meeting?
See you there Mr President and God bless you.
Njimba
GM,
I can see tunafikiria kitu kimoja na kwa wakati mmoja!
what a coincidence!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Njimba
Bwana Mtsimbe..usiishie hapa tu sasa na kwa michuzi,..juhudi zifanyike kujinadi zaidi kwa jamii ili waweze kuelewa mnafanya nini na mna vision ipi....i hope mtapata member wengi zaidi na wenye mawazo chanya zaidi yakukipeleka chama chenu kwenye mafanikio mnayoyataraji...msichoke..pigeni mzigo ..tafuteni kondoo wa bwana...chama kiwe na nguvu..natumaini kuna vichwa vingi tu (Professionals) nje ya chama chenu vyenye uwezo mkubwa sana na machungu yanayohitajika kusukuma gurudumu la maendeleo ya nchi yetu tatizo wanakosa nafasi ya kuonyesha na kutumia uwezo wao ili wasaidie kusukuma gurudumu hilo...so ingekua vyema chama chenu kikawa kama daraja lakuwatoa huko walipo..kuwaleta pamoja na kutengezeza mazingira ambayo yatawafanya wajisikie na kuguswa kutumia uwezo wao wote na nguvu zao katika kuliletea taifa letu maendeleo ya kweli.........wako wengi sana lakini wanakosa morali na hari ya kuliinua taifa lao..so wanaishia kujinufaisha wenyewe na elimu zao..which is not wrong but ingefaa zaidi kama wangejijali wao na taifa lao kwa pamoja...but tatizo tunarudi pale pale wanakosa sehemu na mazingira muafaka yakutoa mengi yalio kwenye vichwa vyao kulisaidi taifa....
so this is your challenge bw. Mtsimbe.
Mimi ni mwanachama wa TPN, ingawa sijapata muda kujishugulisha rasmi.
Sidhani kama bwana Sanctus Msimbe anataka nikajiunge pale kama Fair Player, anachotaka yeye ni kujiunga kwa jina langu halisi la Mwakaleli Donatus. Siri yangu ya kujiita FairPlayer itabakia yangu.
Hoja ya majina halisi sioni mantiki yake kwa hapa JF
Asanteni sana
Amekuelewa
Mimi ni mtaalamu wa kupindua Nchi vipi nije?
Unataka kujiunga na TPN kutokana na kufahamiana na Mtsimbe toka Mnazi Mmoja ama kutokana na kuelewa Sera kamili za TPN?
Yaani umefuatilia TPN toka bado Kamati ya Uanzishwaji mpaka leo hii hukupata Hamasa ya kujiunga nayo? Mpaka moto huu ambao umewashwa hapa JF ndo umekufumbua macho? Hukuwahi wish kwamba ungekuwa among wanaotajwa kama Founding Members wa TPN?
Kuna namna hapa!!!
Ndugu Mtsimbe,
Katika kuboresha muundo wa jumuia yako, ni vizuri muweke sections zinazotenganisha taaluma mbali mbali ndani ya TPN. Kwa mfano mimi ni mwanachama wa IEEE (Institute of Electrical and Electronics Engineers) ingawa mimi siyo mhandisi wa umeme kama ambavyo ungetegemea, bali ni mhandisi wa mitambo (Mechanical Engineer). Ila kwenye IEEE kuna Automatic Control Society (ACS) ambayo ndiyo imenifanya niwe mwanachama wa IEEE. Vivyo hivyo huko kwenye TPN, ni vizuri muweke vijumuia vidogo vidogo kama hivyo ambavyo vinawakutanisha watu wa fani moja. Hiyo itakuwa na kivutio cha kuleta professionals mbali mbali wakitegemea kukutana na wenzao wenye backgrounds zinazofanana.
Mzalendo Wakunyuti, nashukuru sana kwa mawazo yako mazuri. Nikitumia lugha ya kigeni . . "You have hit the bulls eyes". Nitafikisha maoni yako TPN na tutayafanyia kazi yote. Kama utakuwa DSM tarehe 31 August 2008 karibu katika AGM .
Ndugu yangu HOFSTEDE sikubaliani na wewe suala moja kwamba kila tatizo ni CCM hapana. Bwana Sanctus alichoeleza yeye ni kitu tofauti kabisa na suala la taaluma sasa hiyo CCM huko kwenye taaluma inatoka wapi labda kuhusu hili suala la ajira nakubaliana na wewe kama utakuwa umeajiliwa ikulu na ikafika mahala wana taaluma mnakutana uso kwa uso hapo kuna utata, Lakini na imani mtandao wa TNP unajitegemea utakapojiunga huko siyo lazima ujitangaze kuwa wewe ni JF memberZimwi likujualo halikuli likakwisha, lakini kwa JF CCM wakijua jina lako halisi umejiingiza kifungoni kimawazo. We unafikiri wakijua kuwa wewe ni Ofisa IKULU na upo JF si ndio watajua kuwa mvujisha siri. Hivi hivi anonimity ndio watajirekebisha maana humjui nani adui yako na hivyo itakufanya uwe katika mstari ulionyooka kila wakati. Mnaojitambulisha ni vizuri kwani role yenu humu ni kusoma Ila wapo wenye role ya kijasusi humu. Yaani wafukua habari ili kuisaidia nchi hawa waendelee kuwa ANONIMOUS