Jf ilinikutanisha na tapeli wa mapenzi

Wakuu, heshima mbele,

Najuta sana kumtafuta partner humu JF yani pamejaa usanii hapa usipokuwa mjanja kama mimi unalizwa hivi hivi unajiona.


Kipindi kile nilikuja na swala la kutafuta mchumba hapa, kweli huyo aliyejidai mchumba alipatikana bada ya kuchuja chuja na kufanya trial and error. kumbe mchumba hakuwa mchumba bali tapeli wa mapenzi tu. mkasa ulikuwa hivi....... jamaa alisema yuko single na mara ya mwisho kuwa na msichana ni mwaka mmoja uliopita.baada ya kuchat sana kupitia mtandao huu wa JF na email ilibidi tupeane mawasiliano ya simu, na majina ya facebook account. Ukweli mawasiliano yalikuwa hot sana. Simu zilikuwa hazikauki, meseji ndo dahhh siwezi sema, kutwa kuchwa ni kuchat na kupena meseji za mahaba. Ila kwenye facebook friend list yake ilikuwa imefungwa huwezi ona nani ni rafiki yake na huwezi post kwenye wall yake pia.

Basi, sisi tukiwa kwenye mapenzi motomoto na kuliwazana (ila sikuwa mwepesi kutoa tundi ndio ninachoshukuru na kujivunia) kumbe jamaa ana girlfriend wake wa long mie sikujua, basi siku moja niliona friend request ya mdada mmoja hata simjui ameni-add mie bila hiyana kabla ya kumu-accept nikawa natumiana nae inbox kujua ni nani na ni wawapi.....bi dada akaniambia nimuadd kwa faida yangu, ila akawa anadadisi sana kuhusu mahusiano yangu ya kimapenzi, sikuwa muwazi sana hadi aliponitajia jina la facebook la huyu kiumbe tulokutana JF. Huyu binti alisema yeye na huyu fisadi wa mapenzi ni wachumba wa long time ila yeye anafanya kazi mkoani huwa anakuja dsm mara chache sana. Nilimuuliza kuhusu uthibitisho ili niamini maneno yake then alinitumia hadi ushahidi wa pics ambazo sio za kawaida yani za mitego mitego ya kimapenzi zinazoonesha wako na mahusiano live (picha zilionesha hata dates za muda wa karibuni), kuforwad emails za huyu kiumbe wanazotumiana kila leo za kimapenzi n.k.

Ukweli baada ya hayo yote hasira zilinipanda ila nikazituliza nikapata ujasiri wa kumuomba kijana anipishe tugawane ustaarabu. kijana alisita huku akisistiza nimwambie why, mie nikamwambia nimeona siwezi match nae, yeye akawa anasisitiza bado ni mapema mie ku conclude hivyo. Nilipoona anasisitiza nikamwambia live kwamba ana msichana mwingine hivyo ni bora nimpe nafasi ili apumue vizuri! Kijana alibisha hadi leo hii.., pamoja na kumforwadia emails zake lakini wapi bado anakataa.

Hili tukio nimeona nililete ili kuwaasa wasichana wenzangu na hata kaka zangu ambao nao wako kwenye process ya kuisaka ndoa wawe makini sana. mimi kwa hili naweza sema ni Mungu ameniokoa kwani nilikuwa ninaelekea mbali na kuzamia kabisa! huwa nimefikiria ilikuwaje huyu dada akanijua kupitia facebook? au alipewa password na hyu kaka? hapana Mungu aliamua kunionesha na kuniokoa.

Wanawake wenzangu na kaka zangu tumuombe sana Mungu ili atupatie wanaume na wanawake wa ukweli na sio matapeli.

Mbarkiwe sana.

Pole kwa yaliyokukuta, na bahati yako kupata ufunulio kabla mambo hayajaharibika, vinginevyo ungejuta kuzaliwa na kuona aibu hata kutamka hadharani kama unavyofanya leo. Majuto ni mjukuu.

Kwa namna nyingine nakupongeza kwa kuwa na uvumilivu na subira ambayo imekuepusha katika janga lililojificha ndani ya ngozi ya kondoo lakini ndani ni mbwa mwitu mkali. Hata hivyo halijaharibika neno kwa kuwa tunajifunza kutokana na makosa. Jipe moyo Mungu yuko upande wako, soon atakufunulia lililojema zaidi kwako.

Nakupongeza kwa kutoa tahadhari kwetu sote. Mimi na wenzetu wengi tumetahadharishwa vya kutosha.
 
Nimepitia maoni yenu wote, kwa mlionipa pole ninawashukuru sana. Ninaomba pia niweke wazi mambo yafuatayo

1. kuhusu kuonana live tulishaonana na alionekana ni innocent na mcha Mungu kwa maneno yake, pia kwa muonekano sio mtu mbaya au anayeonesha kuwa na tabia mbaya
2. Kwa waliokazia kuhusu ulaji wa tunda, sina haja ya kumdanganya mtu nisiye mjua na asiyenijua ukweli ni huo kwamba kamwe hakuwahi kuuona utupu wangu na kwa hilo siko na sikuwa mrahisi kwa yoyote yule. Kwahiyo kama wewe unalazimisha kuamini hivyo wewe amini tu upendavyo ila tunda ni langu na halikuliwa.
3. Watu hukutana popote na kufanikiwa kuwa na mahusiano yenye manufaa tu, hivyo kukutana na mtu online, street, kanisani au kwingineko hakucount ila ni aina ya mtu uliyekutana naye ndio inacount.
4. Hata kama ingekuwaje, bado ingekuwa vigumu kwa mimi kujua mambo ya mahusiano yake kwani mpenzi wake yuko mkoani kama nilivyokwisha elezea kwenye post yeye ndiye anayejua wanawasiliana lini na kwa namna gani.
5. Hii post iko hapa ili kuwapa somo wengine ambao kwa njia moja au nyingine wana mpango wa kuanzisha mahusiano ili wawe makini na kutojirahisisha kabla ya kujuana kwa undani iwe online, street n.k.

Otherwise michango yenu wote kwa upande mmoja au mwingine inajenga kutegemeana na nini unaamini as far as relationship is concerned.

nimependa ulivyo ... you seem to be wise and confident ... usikate tamaa, vuta subira na enenda taratibu; utampata atakaye kupenda kwa dhati ... amini kuwa yupo ... ni suala la muda tu!
 
msichana ukishamchoma na kumuacha anakuwa mkali huyo dah!. atakusema hadi ujute kwanini umemchoma. utasikia ooh..umeniharibia maisha, kumbe maisha yaliharibika kabla hata hamjaonana. mapenzi si mchezo aisee. unaweza ukafa au ukawa tahila. mi ndo maana huwa sitongozi.

Na wa siwasi na wewe unaweza ukawa ndyo mlengwa hapa mbona unakuwa mkali.
 
Hata wanawake nao hivyo hivyo wengi wao unakuta mwanamke anawanaume zaidi ya mmoja na anawapanga kama foleni ya ATM za NMB na hawajuani

ngoja nicheke kwanza:lol: ni bora tuseme binadamu hatuaminiki hakuna cha mwanamke wala mwanaume, hapo ni kuomba Mungu akufungie ni kweli wapo wenye kuolewa wakianzia mahusiano humu humu mitandaoni ingawa ni wachache , wanaolizwa ni wengi na sio wanawake tu, hata wanaume wameshalizwa sana tu.
 
  • Thanks
Reactions: Sal
Pole Nakadori, mitandao hasa hii ya kijamii haifai, hebu cheki hii video Clip uone jamaa alivyokutana na Jini mtandaoni

hahahaaaaaaaaaaaaaa.... sasa hii si avatar tu ajamni??

aisee kumbe tuko mbali aisee, LOL
 
Last edited by a moderator:
duh nimebaki naduwaa.....huyo dada amejuaje kuwa unataka kuanzisha mahusiano na huyo kaka mpaka akufuate???.......lol pole lakini....mie nahisi ungemtaja humu tumjue...NAME AND SHAME HIM????????????????........kazi kuvizia tu humu hana haya loh,ukute kashawadanganya kibao kwa gia ya ndoa....mmmmmmnh......

Nakubali kabisa wapo wanaume matapeli lakini huu ushahidi aliotoa mtoa mada haudhibitishi kama kweli amedanganywa kwani ana uhakika gani kuwa alieyemletea email ni mwanamke fake na kwamba huyo ndiye aliyemzidi maarifa kwa kumdanganya ni wachumba. nasema hivi kwa sababu mazingira amabayo huyu dada amemfahamu mtoa mada hayako wazi na kuna kila dalili kuwa amezidiwa maarifa na mwanamke mwenzake.
 
Nakubali kabisa wapo wanaume matapeli lakini huu ushahidi aliotoa mtoa mada haudhibitishi kama kweli amedanganywa kwani ana uhakika gani kuwa alieyemletea email ni mwanamke fake na kwamba huyo ndiye aliyemzidi maarifa kwa kumdanganya ni wachumba. nasema hivi kwa sababu mazingira amabayo huyu dada amemfahamu mtoa mada hayako wazi na kuna kila dalili kuwa amezidiwa maarifa na mwanamke mwenzake.

Linaweza kuwepo tatizo la mchujo, sasa kabla hajakaa sawa huyo mwanaume alikuwa bado katika kukusanya kwa ajili ya mchujo, na kumbe waliokusanywa tayari walishaanza kutambua kwamba wako members hivyo kuamua kumlipua jamaa. Hilo nalo ni tatizo na pengine ni kuchezea nafsi za watu. Hili si kwa wanaume tu hata wanawake lipo sana.

Mfano mtu anayepangisha nyumba au kuuza nyumba kwa mtindo wa mnada ni kutesa watu kwa vile kila anayekwenda anakuwa na lengo la kununua, matokea mwenye mkono mrefu wa kufikia pale juu ndiye anaychukua. Wakati mwingine dau lake likipita kiwango kurudisha chini huwa si utaratibu na hivyo hufikia mnada wake kukosa mteja.

Deal nzuri kuna baadhi ya malandlord ambao akishatangaza tena anayekuja na kumwamini basi anaamua kudeal naye kuona kama ana vigezo anavyovitaka, kama hafii basi anamtolea nje na kumkaribisha mwingine hadi anampata mwenye kiango anachotaka.

Wazungu wansema fanya kitu kimoja kwa wakati mmoja hadi kikamilike, lakini vyote kwa mkupuo utakuja kushuhudia hakuna kilichokamilika, ni viporo tu. Kwa hoja yangu hii mwanamke au mwanaume asipokuwa na utaratibu huu anaweza shtukia anaachwa solemba na miaka inazidi kukatika na kushtukia anaangukia ambapo wengi wanamshangaa kana kwamba ni kanyagaboya. Haya mambo ndo hivyo, tunapeana mawazo ya kuwa wa kweli na wawazi ndio maisha mazuri.
 
Mkome kutafuta wachumba kwenye mitandao kwani mtaani hamuonekani???

Humu ni usanii tu

Aliyekwambia mtaani ndio kuna malaika/watakatifu ni nani?kila mahali kuna mapretender wa ajabu na mafisadi wa mapenzi.
Cha msingi mtumaini Mungu wako kwa moyo wako wote wala usizitumainie akili zako(source: Proverb in the Bible).
 
Pole sana ndugu, huyu usanii mwingi. Kuna watu wana tabia chafu ila mtandaoni wanapenda kujionesha ni watakatifu, wengine ni micharuko mitandaoni kiasi kwamba huogopwa na watu ila katika maisha yao hukuta ni wapole na wastaarabu sana. Kuwa makini hata na watu unaojenga nao urafiki wa kawaida.
 
Yeye akasambaze huko kwa wasojua kama kuna ukimwi, biashara ya ku-do bila ndom mbona ishapitwa na wakati siku nyingi. vinginevyo, tukapime. na nikikuhisi utulivu bado, ndom inarudi.

Chunga sana, kuna kisa kililetwa juzijuzi na mwana JF wa zamani kuhusu haya mapenzi ya kwenye mtandao kumbe mtu alikuwa unausambaza UKIMWI makusudi kabisa. Pole.
 
the only advice to men and women.... Be careful, most of social network love is just nothing more than a waste

this is true. Jamani mimi nimejaribu several times haya malovee ya kwenye social forums. Almost 99% ni usanii. Ushauri wangu kwa wale ambao wako serious na kutafuta wapenzi wapige magoti wamwombe mungu watafanikiwa tu. Other altenatives are very complicated and contradictory.

Kumbukeni kwamba ndoa ilianzishwa na mungu katika bustani ya eden kwa ajili ya utukufu wake. Mkono wa shetani ndio ulioingia kuvuruga mpango huu mtakatifu wa mungu. Ndiyo maana yote hayo yanatokea.

Baada ya dhambi wanadamu tulianguka na hatukuweza wala hatuna uwezo wa kujiokoa wenyewe mikononi mwa shetani bali tunahitaji uongozi wa mungu.

Mwomba munu hachoki.
 
Back
Top Bottom