Zion Daughter
JF-Expert Member
- Jul 9, 2009
- 8,921
- 4,235
Ila na wewe ulikuwa hautulii aisee...
https://www.jamiiforums.com/love-co...ywa-na-vijana-natafuta-jibaba.html?highlight=
Haijatulia kabisaa.Amevuna alichopanda
Ila na wewe ulikuwa hautulii aisee...
https://www.jamiiforums.com/love-co...ywa-na-vijana-natafuta-jibaba.html?highlight=
Mmhh
hii itaendelea kutokea kwa wote wanaotafuta mapenzi.
Mapenzi hayatafutwi iwe mitandaoni au huku mitaani tunapoishi,
mapenzi yanatokea kama zao la mahusiano mazuri.
Baadhi ya wakaka huku wako so fake kushinda unavyoweza kuamini...ushauri wangu kuweni waangalifu.
Wakuu, heshima mbele,
Najuta sana kumtafuta partner humu JF yani pamejaa usanii hapa usipokuwa mjanja kama mimi unalizwa hivi hivi unajiona.
Kipindi kile nilikuja na swala la kutafuta mchumba hapa, kweli huyo aliyejidai mchumba alipatikana bada ya kuchuja chuja na kufanya trial and error. kumbe mchumba hakuwa mchumba bali tapeli wa mapenzi tu. mkasa ulikuwa hivi....... jamaa alisema yuko single na mara ya mwisho kuwa na msichana ni mwaka mmoja uliopita.baada ya kuchat sana kupitia mtandao huu wa JF na email ilibidi tupeane mawasiliano ya simu, na majina ya facebook account. Ukweli mawasiliano yalikuwa hot sana. Simu zilikuwa hazikauki, meseji ndo dahhh siwezi sema, kutwa kuchwa ni kuchat na kupena meseji za mahaba. Ila kwenye facebook friend list yake ilikuwa imefungwa huwezi ona nani ni rafiki yake na huwezi post kwenye wall yake pia.
Basi, sisi tukiwa kwenye mapenzi motomoto na kuliwazana (ila sikuwa mwepesi kutoa tundi ndio ninachoshukuru na kujivunia) kumbe jamaa ana girlfriend wake wa long mie sikujua, basi siku moja niliona friend request ya mdada mmoja hata simjui ameni-add mie bila hiyana kabla ya kumu-accept nikawa natumiana nae inbox kujua ni nani na ni wawapi.....bi dada akaniambia nimuadd kwa faida yangu, ila akawa anadadisi sana kuhusu mahusiano yangu ya kimapenzi, sikuwa muwazi sana hadi aliponitajia jina la facebook la huyu kiumbe tulokutana JF. Huyu binti alisema yeye na huyu fisadi wa mapenzi ni wachumba wa long time ila yeye anafanya kazi mkoani huwa anakuja dsm mara chache sana. Nilimuuliza kuhusu uthibitisho ili niamini maneno yake then alinitumia hadi ushahidi wa pics ambazo sio za kawaida yani za mitego mitego ya kimapenzi zinazoonesha wako na mahusiano live (picha zilionesha hata dates za muda wa karibuni), kuforwad emails za huyu kiumbe wanazotumiana kila leo za kimapenzi n.k.
Ukweli baada ya hayo yote hasira zilinipanda ila nikazituliza nikapata ujasiri wa kumuomba kijana anipishe tugawane ustaarabu. kijana alisita huku akisistiza nimwambie why, mie nikamwambia nimeona siwezi match nae, yeye akawa anasisitiza bado ni mapema mie ku conclude hivyo. Nilipoona anasisitiza nikamwambia live kwamba ana msichana mwingine hivyo ni bora nimpe nafasi ili apumue vizuri! Kijana alibisha hadi leo hii.., pamoja na kumforwadia emails zake lakini wapi bado anakataa.
Hili tukio nimeona nililete ili kuwaasa wasichana wenzangu na hata kaka zangu ambao nao wako kwenye process ya kuisaka ndoa wawe makini sana. mimi kwa hili naweza sema ni Mungu ameniokoa kwani nilikuwa ninaelekea mbali na kuzamia kabisa! huwa nimefikiria ilikuwaje huyu dada akanijua kupitia facebook? au alipewa password na hyu kaka? hapana Mungu aliamua kunionesha na kuniokoa.
Wanawake wenzangu na kaka zangu tumuombe sana Mungu ili atupatie wanaume na wanawake wa ukweli na sio matapeli.
Mbarkiwe sana.
A single man in dis world !!!!!!!!!!!!!???????????? I doubt it!
rafiki!sioni faida ya kudanganyana
wewe kama unatafuta wa starehe si useme tu natafuta wa starehe sitaki ndoa wa commitments
mbona wapo weengi humu wako tayari kustarehe na waume na wake za watu bila kuanzishiana threads????/
A single man in dis world !!!!!!!!!!!!!???????????? I doubt it!
ni muda wa kuvuna alichopandaIla na wewe ulikuwa hautulii aisee...
https://www.jamiiforums.com/love-co...ywa-na-vijana-natafuta-jibaba.html?highlight=
Mitch uliliona hili mapema ikabidi ubanane na Kongosho hapohapo kwa Boss,good for you!
Mnakosea sana mnapokuwa mnatafuta ndoa, usitafute ndoa tafuta mpenzi.
rafiki!
Chunga sana, kuna kisa kililetwa juzijuzi na mwana JF wa zamani kuhusu haya mapenzi ya kwenye mtandao kumbe mtu alikuwa unausambaza UKIMWI makusudi kabisa. Pole.
mambo ya kutaka starehe, lol!kafanya nini rafiki????/