Jeshi la polisi hakuna kitu

FredKavishe

JF-Expert Member
Dec 4, 2010
1,090
318
Kwanza kabisa naomba niseme jeshi letu la polisi linatakiwa lisifanye kazi upande wowote ule sababu mishahara yao inatokana na kodi zetu.
Kwann nasema polisi tz hakuna kitu tumeona msiba wa msanii wetu kipenzi KANUMBA uliotokea juzi nyumbani kwake sinza vatican.kifo kilikuwa hakiaminiki kimesababishwa na nn wengine LULU alimsukuma kanumba
Wengine walikuwa wanapigana kisa simu
Wengine wote walikutwa uchi
sasa leo polisi inakuja kusema kifo cha marehemu kilisababishwa na JACK DANIEL ina alcohol 46 percent hapo ndo maswali zaidi yarudi
Hivi si juzi KANUMBA wakati anahojiwa na salama kipindi cha mkasi alisema hanywi pombe??????
Pili jeshi la polisi walivyo wazembe sehemu ya crime scene ambapo ndo nyumbani kwa kanumba kumejeuka kuwa sehemu ya kuomboleza.

Kwa upeo wangu mdogo ile nyumba ingekuwa iwe closed huwezi niambia jack daniel imuue kanumba pia huwezi niambia lulu hajaplay part kwenye hiki kifo.
Pia hatuweze kukwepa mdogo wake hajausika pia

Ndani ya nyumba walikuwa watu watatu mmoja kafa wamebaki wawili hawa ndo wakuhojiwa lakini ushahidi mkubwa mmeshaua kuruhusu nyumba ya crime scene kufanyika maombolezo.
Polisi wangepaswa kuclose nyumba yote kama kwa siku tatu tuaona kwanye muvi na series ya kipelelezi ya CSI au mnataka kuniambia hakuna kitego cha upelezi
Eti mnamuweka mtoto wa watu jela mnamuhoji yeye wakati ushahidi muhimu mumeshaufuta.
Polisi ndo wakubeba lamawa ushahidi mkubwa mmeupoteza ile nyumba ingekuwa closed japo sijasomea upelelezi lakini mngeweka no je movement zao zilikuaje walitoka hapa kwenda kule halafu muhimu kuwa mnarud kumhoji lulu na kaka yake.
Hatuwezi jua labda mtu kutoka nje alikuja kukamilisha huo mpango kwa mkataba maalumu kati ya mdogo mtu na lulu

Mimi huwezi niambia marehemu eti amekunywa jack daniel akafa hapana

My take:
Polisi msirudie tena kosa hili kama kitu kimetokea kinahusishwa na maauaji sehemu iliyotokea ifungwe na kufanya uchunguzi crime scene
Na raisi wetu alivyo mzembe amekwenda kutembelea crime scene na kutoa rambirambi ina maana kabariki hiki kifo

Majanikv

From

Machimboni
 
Kikwete mwenyewe keshasema siku za Kanumba zilishafika, kifo ilikuwa inatafuta sababu tu
 
Jeshi la Polisi la Bongo wako makini sana kwenye mandamano ya CHADEMA tu hicho ndo wanacho jua na kupiga marufuku mikusanyiko isiyo halali siku ya sikukukuu.

Mimi sijawahi ona jeshi la kizembe kama hili yaani siku ya sikukuu ndo wanajifanya wako bise na mbwa na falasi kana kwamba nchi iko kwenye machafuko,
 
mapungufu mengineyo ambayo polisi wameyafumbia macho ni kukwepa kumkamata yule dakitari aliyedai Kanumba bado ni mzima kwa madai feki ya kutowatia khofu wahusika!!!!!! Sheria za makosa ya jinai zipo wazi kuwa pale ambapo mtu amefia nje ya hospitali kwenye mazingira tatanishi basi polisi lazima waitwe kwenye eneo la tukio na kufanya uchunguzi wao wenyewe sasa huyu dakitari alisababisha crime scene to be contaminated pale alipowaagiza wapeleke maiti polisi na hivyo kuvuruga ushahidi ambao polisi walibidi waukusanye wao wenyewe kwa kutumia tekinolojia ya forensic science................polisi hivi sasa wanategemea hearsay kufanya uchunguzi jambo ambalo limepitwa na wakati kwenye ulimwengu huu wa sayansi na tekinolojia....

A contaminated crime scene is a major blow to any criminal prosecution against anyone..............na kwa hatua iliyopo siyo sahihi kwa polisi kumtia ndani Lulu au mtu yeyote yule kwa sababu hakuna ushahidi wowote ule wa foulplay........
 
Hakuna polisi Tz. Kuna genge la wazee wa baraza wanaojiita polisi. Jaribu siku zote fuatilia statement zao katika matukio mbali mbali ni mkanganyo mtupu. Sema bahati nchi yetu kuna raia walokole. Ingelikuwa ni kama S. Africa na aina ya police tulio nao, vibaka wangeenda kuinjua msosi wa mkuu wa kaya pale ikulu na kuula wao.
.
 
Wazee wa intelligencia.....usishangae wakianza kukamata Jf members kwa thread na post wakisingizia intelijensia
 
kwani ukimnywa jack d, huwezi kulewa ukayumba/sukumwa ukagonga kichwa ukafa????????????????????

Halafu unadhani kwenye mahojiano hawa wasanii wanasemaga ukweli? Unakumbuka wema alisema hana boyfriend akapata skendo ya kutembea na mume wa mtu? Usiamini sana mahojiano.....
 
Hakuna polisi Tz. Kuna genge la wazee wa baraza wanaojiita polisi. Jaribu siku zote fuatilia statement zao katika matukio mbali mbali ni mkanganyo mtupu. Sema bahati nchi yetu kuna raia walokole. Ingelikuwa ni kama S. Africa na aina ya police tulio nao, vibaka wangeenda kuinjua msosi wa mkuu wa kaya pale ikulu na kuula wao.
.
kweli kabisa mkuu police nchi hii ni zero zero kabisa!!!!! hawana tofauti na wanojiita eti usalam wa taifa. jwt nawakubari sana!!
 
kwani ukimnywa jack d, huwezi kulewa ukayumba/sukumwa ukagonga kichwa ukafa????????????????????

Halafu unadhani kwenye mahojiano hawa wasanii wanasemaga ukweli? Unakumbuka wema alisema hana boyfriend akapata skendo ya kutembea na mume wa mtu? Usiamini sana mahojiano.....

Hata kama angekuwa amekunywa pombe, namna polisi wanavyofanya kazi hairidhishi. Lakini jeshi pia linaathiriwa na mfumo wa uongozi wa kisiasa. Kama viongozi wa kisiasa wanayapa kipaombele mambo ya kulinda maslahi ya wanasiasa, polisi watapata wapi ari ya kulinda wananchi?
 
just hire the scotland yard will do it right away..forget about this vibaka chaser and anti democracy.hawana tofauti na hao wasanii wenyewe kwa maana halisi ya USANII
 
kweli. . . .

Hata kama angekuwa amekunywa pombe, namna polisi wanavyofanya kazi hairidhishi. Lakini jeshi pia linaathiriwa na mfumo wa uongozi wa kisiasa. Kama viongozi wa kisiasa wanayapa kipaombele mambo ya kulinda maslahi ya wanasiasa, polisi watapata wapi ari ya kulinda wananchi?
 
Wawalete Mossad ndo utajua kama jamaa wale wanafanya kazi yaani hata kama nyumba hiyo waivunje leo na waweke club hakuna shida Mossad watafanya kazi hiyo ndani ya masaa na watakamilisha
 
Back
Top Bottom