Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limetangaza nafasi za kujiunga na mafunzo kwa wakujitolea, 2017

emmarki

JF-Expert Member
Nov 22, 2012
682
918
Kwa wale wanaopenda kujiunga na JKT kwa mwaka huu nafasi ziko wazi. mchakato unaanzia Wilayani kwako. Tembelea ofisi ya wilaya yako kwa maelezo zaidi.

=========

Jeshi la kujenga taifa JKT limetangaza nafasi ya kujiunga na mafunzo ya jeshi hilo kwa kujitolea kwa mwaka 2017 ambapo vijana kutoka Tanzania bara na Visiwani wanaruhusiwa kuomba. Mkuu wa JKT Meja Jenerali Michael Isamuhyo amesena utaratibu wa vijana kuomba nafasi hizo unaratibiwa na wakuu wa mikoa na wilaya.


TAARIFA KWA UMMA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Michael Isamuhyo anawatangazia vijana wote wa Tanzania Bara Na Visiwani nafasi za kujiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa kujitolea mwaka 2017.

Utaratibu wa vijana kuomba na hatimaye kuchaguliwa kujiunga na mafunzo hayo, unaratibiwa na ofisi za Wakuu wa mikoa na wilaya ambapo muombaji anaishi.

Zoezi la kuchagua vijana litaanza Mwezi Novemba 2017 na vijana watakaochaguliwa watatakiwa kuripoti kwenye makambi ya JKT waliyopangiwa kuanzia tarehe 04 mpaka 09 Desemba 2017.

Jeshi la Kujenga Taifa linaendelea kusisitiza kuwa nafasi za vijana kujiunga na mafunzo ya JKT haziuzwi, aidha yeyote atakaye husika na utapeli wa kuuza au kununua nafasi hizo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

jeshi.PNG
 
Chanzo cha taarfa ni ITV SAA mbili usiku, Aliye na masharti waliyoyatoa atuwekee tuone kama sifa znakubali!
 
Hizi si ajira mkuu, ni nafasi za mafunzo ya jkt kwa kujitolea. Jkt haiajiri inakupa mafunzo na elimu ya stadi za maisha hususani kilimo na ufugaji ili kukuandaa kujitegemea. Kuajiriwa na vyombo vingine ni bahati
 
JKT hakuna ajira kule unaenda kuwa mtumwa mpaka hapo ajira zitakapo toka JWTZ ,TANAPA,POLISI,MAGEREZA,UHAMIAJI haya makundi saa ndyo yanayoenda kuajiri hukohuko JKT wanafuata vijana unapiga interview ukibahatika unachomoka

Tangazo lililotolew ni LA mafunzo ya JKT mafunzo ni miezi 6 mkataba wa kulijenga taifa ni miaka 2 miezi sita ipo ndani ya hiyo miaka 2 kama miaka 2 itaishi bado upo JKT hujapata ajira kwenye makundi niliyotaja hapo juu .unarudi nyumbani unachopewa ni nauli na hela ya kula njiani

Kama una ndoto za kuwa askari omba nafasi kwani kila penye nia hapakosi njia
 
JKT hakuna ajira kule unaenda kuwa mtumwa mpaka hapo ajira zitakapo toka JWTZ ,TANAPA,POLISI,MAGEREZA,UHAMIAJI haya makundi saa ndyo yanayoenda kuajiri hukohuko JKT wanafuata vijana unapiga interview ukibahatika unachomoka

Tangazo lililotolew ni LA mafunzo ya JKT mafunzo ni miezi 6 mkataba wa kulijenga taifa ni miaka 2 miezi sita ipo ndani ya hiyo miaka 2 kama miaka 2 itaishi bado upo JKT hujapata ajira kwenye makundi niliyotaja hapo juu .unarudi nyumbani unachopewa ni nauli na hela ya kula njiani

Kama una ndoto za kuwa askari omba nafasi kwani kila penye nia hapakosi njia
Sawa kabisa tumepitia huko tumeshuhudia watu wakikatwa mabogi na kubaki then mnarudishwa kwenu
 
Back
Top Bottom