Mikael Aweda
JF-Expert Member
- Dec 17, 2010
- 2,973
- 3,901
Wakuu,
Nilipata fursa ya kuhudhuria kikao cha kutathmini mchakato wa APRM kilichoandaliwa na asasi ya kimataifa ya OSEA ktk hoteli ya Kilmanjaro DSM wiki hii.
Kikao hicho kiliwashirikisha vyama vyote vya siasa, ofisi ya msajili, Asasi za kiraia, wabunge, waandishi wa habari viongozi wakubwa wa serikalini, Maprofesa kutoka ndani na nje nk.
Kulikuwa na wasemaji kutoka ndani na nje ya nchi wakiwepo wabunge wajumbe wa APRM wa kwetu na kutoka nchi mbali mbali wakiwepo mmoja wa profesa kutoka ghana aliyewasilisha mada.
Kama kawaida kulikuwa mjadala mzito wengine wakisema kiwango cha utawala bora nchini kinaridhisha na wengine wakisema hakiridhishi.
Mmoja wa wasemaji jenerali Ulimwengu ktk dakika zake za mwisho alichafua hali ya hewa pale alipouliza swali lililoshindwa kujiwa na wote waliokuwemo ktk ukumbi huo.
Aliuliza, wakati tunapojadili utawala bora je, kuna mtu yeyote miongoni mwetu anayejua matokeo ya kura za urais za mwaka 2010 kwa kila jimbo ktk ukumbi huu?
Swali hilo lilibadilisha kabisa hali ya hewa humo ndani hata wale waliokuwa wanasema TZ kuna utawala bora walikaa kimya na wote tukatazamana.
Mwandishi moja akaendelea kuweka chumvi kwenye kidonda kwa kusema yeye alizitafuta na hakufanikiwa.
Hali hiyo ilimfanya mwongoza kipindi kumkaribisha msemaji wa OSEA kufunga mkutano huo ktk mazingira hayo yasiyo na jibu na swali hilo.
My take,
Naomba kutoa changamoto kama kuna mwanajf mwenye jibu la swali la Jenerali UlImwengu atupe kwa faida ya wanajf wote.
Nilipata fursa ya kuhudhuria kikao cha kutathmini mchakato wa APRM kilichoandaliwa na asasi ya kimataifa ya OSEA ktk hoteli ya Kilmanjaro DSM wiki hii.
Kikao hicho kiliwashirikisha vyama vyote vya siasa, ofisi ya msajili, Asasi za kiraia, wabunge, waandishi wa habari viongozi wakubwa wa serikalini, Maprofesa kutoka ndani na nje nk.
Kulikuwa na wasemaji kutoka ndani na nje ya nchi wakiwepo wabunge wajumbe wa APRM wa kwetu na kutoka nchi mbali mbali wakiwepo mmoja wa profesa kutoka ghana aliyewasilisha mada.
Kama kawaida kulikuwa mjadala mzito wengine wakisema kiwango cha utawala bora nchini kinaridhisha na wengine wakisema hakiridhishi.
Mmoja wa wasemaji jenerali Ulimwengu ktk dakika zake za mwisho alichafua hali ya hewa pale alipouliza swali lililoshindwa kujiwa na wote waliokuwemo ktk ukumbi huo.
Aliuliza, wakati tunapojadili utawala bora je, kuna mtu yeyote miongoni mwetu anayejua matokeo ya kura za urais za mwaka 2010 kwa kila jimbo ktk ukumbi huu?
Swali hilo lilibadilisha kabisa hali ya hewa humo ndani hata wale waliokuwa wanasema TZ kuna utawala bora walikaa kimya na wote tukatazamana.
Mwandishi moja akaendelea kuweka chumvi kwenye kidonda kwa kusema yeye alizitafuta na hakufanikiwa.
Hali hiyo ilimfanya mwongoza kipindi kumkaribisha msemaji wa OSEA kufunga mkutano huo ktk mazingira hayo yasiyo na jibu na swali hilo.
My take,
Naomba kutoa changamoto kama kuna mwanajf mwenye jibu la swali la Jenerali UlImwengu atupe kwa faida ya wanajf wote.