Jela miaka 7 kwa kumuua mwanaume bila kukusudia, alimkuta amesimama na mtalaka wake

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro imemhukumu kifungo cha miaka saba jela Donati Phabian baada ya kupatikana na hatia ya kumuua bila kukusudia Alfred Damas kwa madai ya kumkuta akizungumza na mtalaka.

Phabian alifanya kitendo hicho baada ya kuwakuta wawili hao barabarani katika Kijiji cha Lugangwa, Tarafa ya Matombo Mkoani Morogoro.

Akisoma hukumu hiyo, Jaji Paulo Ngwembe alisema amezingatia kwa kina mazingira yaliyosababisha mauaji hayo na kuona kuwa ni mazingira ya kukosekana kwa utu.

Jaji alisema mshtakiwa aliamua kujichukulia sheria mkononi kwa kumuua mwanaume aliyemkuta amesimama njiani akizungumza na mwanamke ambaye yeye alikuwa mke wake huku akiwa tayari ameshampa talaka.

Licha ya mshtakiwa kufika kituo cha polisi kujielezea kuwa alifanya hivyo kwa sababu bado ana mapenzi na mkewe na asingependa awe na mtu mwingine, alisema hilo ni jambo la mapenzi ya kitoto na kwamba kama angetaka usuluhishi wangeenda mbele ya wazazi wao.

Alisema kimsingi inaonyesha mshtakiwa alijipeleka polisi kwa kulinda usalama wake na si kujutia makosa yake kwamba adhabu hiyo ya miaka saba jela, itamfanya ajutie makosa yake na kuwa fundisho kwa wengine.

Hata hivyo, Jaji Ngwembe alisema hati ya kukata rufani dhidi ya adhabu hiyo iko wazi kwa mshtakiwa pale atakapotaka kufanya hivyo.

Awali, Wakili wa Utetezi, Kisawai Mandela, aliiomba mahakama kumpa mshtakiwa adhabu yenye huruma kwa sababu ni mtendaji kosa kwa mara ya kwanza na ana watoto ambao wanamtegemea.

Naye Wakili wa Serikali, Evelyne Ndunguru, aliiomba mahakama kumpa mshtakiwa adhabu itakayolingana na kosa alilolitenda ili iwe fundisho kwake na wengine wenye tabia za kujichukulia sheria mkononi.

Akisoma shtaka, karani wa mahakama hiyo, Lilian Kombe, alidai kuwa mshtakiwa alifanya kosa hilo mwaka 2021 kwa kumuua mwanamume kwa kumchanja na kisu mwilini mbele ya ndugu wawili wa mwanamke huyo, jambo lililosababisha kifo chake papo hapo.

Wakati huo huo, Amelda Ngagiri (60) mkazi wa kijiji cha Nyandira, wilayani Mvomero amehukumiwa kifungo cha nje kwa miezi 12 na kupewa adhabu ya kusafisha eneo la kituo cha afya Nyandira baada ya kupatikana na hatia ya kuua bila kukusudia.

Jaji Ngwembe alisema ameamua kutoa hukumu hiyo kwa mshtakiwa huyo kutokana na umri wake mkubwa na afya yake kuwa si nzuri na kwamba anapaswa kusafisha kituo hicho na akishindwa atakwenda jela miaka minne.

Awali karani Lilian Kombe alidai kuwa tukio hilo lilitokea Mei 25, 2020 majira ya usiku katika kijiji cha Nyandira ambapo mshtakiwa huku akijua kufanya hivyo ni kosa, alimuua kwa kumshambulia na gongo aliyekuwa amelewa.

Source: IPP
 
Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro imemhukumu kifungo cha miaka saba jela Donati Phabian baada ya kupatikana na hatia ya kumuua bila kukusudia Alfred Damas kwa madai ya kumkuta akizungumza na mtalaka.

Phabian alifanya kitendo hicho baada ya kuwakuta wawili hao barabarani katika Kijiji cha Lugangwa, Tarafa ya Matombo wilayani Morogoro.

Akisoma hukumu hiyo, Jaji Paulo Ngwembe alisema amezingatia kwa kina mazingira yaliyosababisha mauaji hayo na kuona kuwa ni mazingira ya kukosekana kwa utu.

Jaji alisema mshtakiwa aliamua kujichukulia sheria mkononi kwa kumuua mwanaume aliyemkuta amesimama njiani akizungumza na mwanamke ambaye yeye alikuwa mke wake huku akiwa tayari ameshampa talaka.

Licha ya mshtakiwa kufika kituo cha polisi kujielezea kuwa alifanya hivyo kwa sababu bado ana mapenzi na mkewe na asingependa awe na mtu mwingine, alisema hilo ni jambo la mapenzi ya kitoto na kwamba kama angetaka usuluhishi wangeenda mbele ya wazazi wao.

Alisema kimsingi inaonyesha mshtakiwa alijipeleka polisi kwa kulinda usalama wake na si kujutia makosa yake kwamba adhabu hiyo ya miaka saba jela, itamfanya ajutie makosa yake na kuwa fundisho kwa wengine.

Hata hivyo, Jaji Ngwembe alisema hati ya kukata rufani dhidi ya adhabu hiyo iko wazi kwa mshtakiwa pale atakapotaka kufanya hivyo.

Awali, Wakili wa Utetezi, Kisawai Mandela, aliiomba mahakama kumpa mshtakiwa adhabu yenye huruma kwa sababu ni mtendaji kosa kwa mara ya kwanza na ana watoto ambao wanamtegemea.

Naye Wakili wa Serikali, Evelyne Ndunguru, aliiomba mahakama kumpa mshtakiwa adhabu itakayolingana na kosa alilolitenda ili iwe fundisho kwake na wengine wenye tabia za kujichukulia sheria mkononi.

Akisoma shtaka, karani wa mahakama hiyo, Lilian Kombe, alidai kuwa mshtakiwa alifanya kosa hilo mwaka 2021 kwa kumuua mwanamume wa mke wake aliyemwacha kwa kumchanja na kisu mwilini mbele ya ndugu wawili wa mwanamke huyo, jambo lililosababisha kifo chake papo hapo.

Wakati huo huo, Amelda Ngagiri (60) mkazi wa kijiji cha Nyandira, wilayani Mvomero amehukumiwa kifungo cha nje kwa miezi 12 na kupewa adhabu ya kusafisha eneo la kituo cha afya Nyandira baada ya kupatikana na hatia ya kuua bila kukusudia.

Jaji Ngwembe alisema ameamua kutoa hukumu hiyo kwa mshtakiwa huyo kutokana na umri wake mkubwa na afya yake kuwa si nzuri na kwamba anapaswa kusafisha kituo hicho na akishindwa atakwenda jela miaka minne.

Awali karani Lilian Kombe alidai kuwa tukio hilo lilitokea Mei 25, 2020 majira ya usiku katika kijiji cha Nyandira ambapo mshtakiwa huku akijua kufanya hivyo ni kosa, alimuua kwa kumshambulia na gongo aliyekuwa amelewa.

Source: IPP
Alieandika hii habari atakuwa sio mtanzania!
 
Kesi za Mauaji bwana, ndio mana nawambiaga watu waache visebu sebu maaana Mtu anaweza kukupoteza duniani

Na bado akadunda uraiani, ni mazingira tu hapo yanatengenezwa Unapotezwa Watu wanahukumiwa

Kifungo cha nnje wakati wewe ushachimbiwa futi 10 Ardhini,ukiona hii sio mali yangu kaa nayo mbali,mwenye mali akikuonya mara mbili tatu ACHA basi acha.

Wazungu wanakwambia hii sio murder case,hii tunaita manslaughter.
 
Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro imemhukumu kifungo cha miaka saba jela Donati Phabian baada ya kupatikana na hatia ya kumuua bila kukusudia Alfred Damas kwa madai ya kumkuta akizungumza na mtalaka.

Phabian alifanya kitendo hicho baada ya kuwakuta wawili hao barabarani katika Kijiji cha Lugangwa, Tarafa ya Matombo Mkoani Morogoro.

Akisoma hukumu hiyo, Jaji Paulo Ngwembe alisema amezingatia kwa kina mazingira yaliyosababisha mauaji hayo na kuona kuwa ni mazingira ya kukosekana kwa utu.

Jaji alisema mshtakiwa aliamua kujichukulia sheria mkononi kwa kumuua mwanaume aliyemkuta amesimama njiani akizungumza na mwanamke ambaye yeye alikuwa mke wake huku akiwa tayari ameshampa talaka.

Licha ya mshtakiwa kufika kituo cha polisi kujielezea kuwa alifanya hivyo kwa sababu bado ana mapenzi na mkewe na asingependa awe na mtu mwingine, alisema hilo ni jambo la mapenzi ya kitoto na kwamba kama angetaka usuluhishi wangeenda mbele ya wazazi wao.

Alisema kimsingi inaonyesha mshtakiwa alijipeleka polisi kwa kulinda usalama wake na si kujutia makosa yake kwamba adhabu hiyo ya miaka saba jela, itamfanya ajutie makosa yake na kuwa fundisho kwa wengine.

Hata hivyo, Jaji Ngwembe alisema hati ya kukata rufani dhidi ya adhabu hiyo iko wazi kwa mshtakiwa pale atakapotaka kufanya hivyo.

Awali, Wakili wa Utetezi, Kisawai Mandela, aliiomba mahakama kumpa mshtakiwa adhabu yenye huruma kwa sababu ni mtendaji kosa kwa mara ya kwanza na ana watoto ambao wanamtegemea.

Naye Wakili wa Serikali, Evelyne Ndunguru, aliiomba mahakama kumpa mshtakiwa adhabu itakayolingana na kosa alilolitenda ili iwe fundisho kwake na wengine wenye tabia za kujichukulia sheria mkononi.

Akisoma shtaka, karani wa mahakama hiyo, Lilian Kombe, alidai kuwa mshtakiwa alifanya kosa hilo mwaka 2021 kwa kumuua mwanamume kwa kumchanja na kisu mwilini mbele ya ndugu wawili wa mwanamke huyo, jambo lililosababisha kifo chake papo hapo.


Source: IPP
kukubali yaishe shida nini?
 
Kesi za Mauaji bwana, ndio mana nawambiaga watu waache visebu sebu maaana Mtu anaweza kukupoteza duniani

Na bado akadunda uraiani, ni mazingira tu hapo yanatengenezwa Unapotezwa Watu wanahukumiwa

Kifungo cha nnje wakati wewe ushachimbiwa futi 10 Ardhini,ukiona hii sio mali yangu kaa nayo mbali,mwenye mali akikuonya mara mbili tatu ACHA basi acha.

Wazungu wanakwambia hii sio murder case,hii tunaita manslaughter.
Huo ndo ukweli mkuu! Mtu anatengeneza mazingira ya namna ya kukupoteza, hili hata akishtakiwa liwe kosa la manslaughter!
 
Huo ndo ukweli mkuu! Mtu anatengeneza mazingira ya namna ya kukupoteza, hili hata akishtakiwa liwe kosa la manslaughter!
Hii manslaughter sijaielewa kabisa. Mtalaka wake sio mke wake. Huyu jamaa alitakiwa afungwe maisha iwe fundisho kwa wenye wivu wa kijinga. Huyu barabarani kila mwanamke ni x wa mtu, tukianza "kuua bila kukusudia" wanaosimama nao makaburi yatajaa
 
Back
Top Bottom