Kigi Makasi
JF-Expert Member
- Oct 4, 2022
- 916
- 1,813
Yaani kwa jinsi unavyomwombea na kumshukuru akiamua kuwa mtu wa ovyo anaweza kupasha..., sema uombe aendelee kuwa mstaarabu hivyo hivyoSitoweza msahau baba watoto wangu kwa sababu alinitoa sehemu ambapo hata ndugu zangu wa karibu hawakujua hali niliyokuwa ninapitianilikuwa napitia hali hatarishi na isiyokuwa na mwelekeo wala mwanga.
Hapa nilipo ni kwa sababu yake,mafanikio ninayoyapata japo kidogo mzizi ni yeye kuletwa na Mungu ili anivushe katika mapito.
Anafamilia yake kwa sasa na watoto wengine na upendo uliopo kati yangu,mkewe na Yeye ni ule upendo wa kiMungu
Niliahidi sitokuja fanya mchezo wa kipumbavu wa kutoka nae kimapenzi tena.
Kila ninapowaombea vijana wangu pamoja na wazazi wangu basi babawatoto,mkewe na watoto wao lazima wawepo maombini
Sio kila Ex ni m’baya au ni lazima mkutane kimwili.Kuna maEx hupanda mbegu njema yenye kumea kila kukicha katika maisha ya mhusika