Je vijana tuanzishe chama cha kisiasa kulikomboa taifa, au tuendelee na ccm?

ChingaMzalendo

Senior Member
Nov 9, 2008
192
3
Tangu nchi yetu ipate uhuru, wengi wa viongozi waliomadarakani kwa sasa ni wale wale. kwa namna moja au nyingine wamekuwa wabidalishana vyeo kana kwamba Tanzania ni mali yao binafsi.

Wameanza kuwaandaa wanao ili watakapotoka madarakani waendeleze ufisadi na uongozi wa nchi. Watanzania tumechoka na tunataka mabadiliko.

Wapo vijana wengi safi wenye vipaji na uwezo wa kuongoza, mbali na January, Dr. Shayo na Mashaka, wapo vijana wengi ambao wapo nyumbani Tanzania na ughaibuni tunaoweza kuwashirikiashakatika kutafuta namna ya kulikomboa taifa letu dhidi ya UFISADI

Wadau na wana JF nadhani muda umefika kwetu sisi kutafakari mustakabali wa nchi yetu na kuanzisha chama chetu cha vijana ili kulikomboa taifa. Nadhani hata 2010 tunaweza kufanikiwa kuliko kuwaachia wakina Rostam Aziz ambao wameligeuza nchi kama mali zao. Wadau Tujadili ili swala kwa umakini ili tutafute namna mapema.

Haya yote yanakuja kutokana na ukweli kwamba, tumechoka, na hatutaki taifa letu kufikia hatua ya kuingia pabaya, hasa ukizingatia mambo yanakoelekea. Binadamu anapokuwa hana namna, analazimika kufikiri ili kutatua matatizo yake kwani mafisadi wanatulazimisha kuchukua sheria mikononi mwetu
 
you may first define which age group are young people, below 35 years of age? or else; even if you start a party now; you will be already old buddies at maturity.

The priority should be for young people to participate in active politics in existing parties. Ondoeni woga confront them in existing parties!! by joining the same parties!!
 
Tuanzisheni, lakini mimi niwe Mwenyekiti na uchaguzi ujao nigombee Urais. Endelea kuhamasisha wengine.
 
What a turn.

Wapo vijana wengi safi wenye vipaji na uwezo wa kuongoza, mbali na January, Dr. Shayo na Mashaka, wapo vijana wengi ambao wapo nyumbani Tanzania na ughaibuni tunaoweza kuwashirikiashakatika kutafuta namna ya kulikomboa taifa letu dhidi ya UFISADI

You can't hide your whims..lol
 
Back
Top Bottom