Je, unataka kulima mazao ya mbogamboga na matunda lakini unakosa maarifa sahihi? Karibu tushauriane hapa

Kwa nchi nzima msimu wenye pesa kwa kitunguu, ni ukivune na ukiuze mwezi novemba hadi april. Kwa mfano mpaka jana gunia la kilo 140, lilikuwa tsh 140,000. Last week lililkuwa tsh 120,000

naomba kuuliza msimu mzuri wa kulima vitunguu maji na soko linakuwa la uhakiki ni upi? Asante.
 
kilimomaarifa.tajiri Mungu akubariki hapa tunajifunza mengi mno na unajibu kila unachoulizwa kwa ufasaha na kwa moyo mkuu tofauti na wengine wanaouza ushauri huku JF ilhali hata unapomuuliza kitu hajibu kwa ufanisi.
 
Last edited by a moderator:
Asante,je nitahitaji mbegu gram ngapi kwa nusu eka na mbolea mifuko mingapi? Mapato yatakuwa kiasi gani kwa nusu eka,pia je ni mbegu gani nzuri yenxe pato?.
 
Asante sana Kiongozi kwa ushauri na elimu hii adimu. Nimevutiwa na kilimo cha matikiti maji. Napenda kujua miezi ipi kilimo hiki kinaweza kufanyika. Na pia miezi ipi tunda ili linakuwa adimu sana ili niweze kujipanga. Na kama nitahitaji usaidizi wako wa karibu wakati naanza kilimo huko naweza kukupata? Asante sana.
 
Asante kilimomaarifa.tajiri naomba muongozo wako mimi nina miche ya nyanya aina ya eden kama 400 ndio ina kama wiki na nusu,nini cha kufanya miche ikiwa bado kwenye kitalu kwa wakati huu? Pia ninakusudia kupandia mbolea aina ya samadi,je kwa kila shimo nitaweka kiasi gani ili isiunguze mche? Asante mengine nitauliza baadae.
 
Last edited by a moderator:
Asante sana kilimomaarifa.tajiri, kabla ya kuweka mbegu kitaluni nilitanguliza mbolea ya samadi na majivu kidogo na baada ya hapo nikanyunyiza DAP kulingana na maelezo yako ya nyuma. Ukweli si kwamba samadi nimenunua hivyo sina hakika ni ya lini ila kuna ambayo inaonekana ni ya zamani maana imeshakuwa kama udongo, kuna ambayo bado iko kwenye mifuko na nyingine iko tu chini wala sijaifunika duh! Nirudi kwenye kupiga dawa ya kanitangaze,je inapigwa juu ya majani au ni chini kwenye shina? Barikiwa
 
Last edited by a moderator:
Samahani naomba kuuliza eti ridomil ikipigwa ni baada ya muda gani itakuwa imekolea vizuri kwenye mmea, kwani nilipiga kwenye viazi baada ya saa 2 ikanyesha mvua, lakini kuna mtu aliniambia kuwa ridomil ikikaa nusu saa tangia kupigwa itakuwa imeshafanya kazi yake.
 
Asante sana kilimomaarifa.tajiri tunashukuru kuwa huchoki na maswali yetu. Sasa nimetafakari ulichoniambia kuhusu mbolea ni cha msingi sana naona nisipandie samadi nipandie za dukani tu ili niwe na hakika wa ninachokifanya,sasa naomba tena kipimo kipya kwa kila shimo,pili nikishaweka niichanganye kwanza na udongo ama niiache tu ikutane na mizizi direct?
 
Last edited by a moderator:
Prishaz

KWA MBOLEA ZA VIWANDANI, HASA WAKATI WA KUPANDIKIZA MICHE SHAMBANI

KIPIMO NI KWAMBA, ILE SIKU YA KUPANDIKIZA MICHE INATAKIWA KILA SHIMO LIPATE MLS 250 ZA MAJI YALIYOCHANGANYWA NA MBOLEA. HAYO MAJI YENYE MBOLEA NDIYO HUWA TUNAYAITA KAMA
STARTER SOLUTION, HII INASAIDIA SANA KUUFANYA MMEA KUPATA STRONG SOLUTION IMMEDIATELY UNAPOKUWA TRANSPLANTED. MMEA UNAPOWEKWA KATIKA SHIMO, MAJI YA KWANZA KUNYONYWA NA MMEA YAWE NI HAYO YENYE MBOLEA.

SASA MBOLEA ZA KUPANDIA NI, DAP, NPK (17;17;17), YARA MILLER WINNER, TSP, MINJINGU MAZAO ETC, KWA HIYO UTACHUKUA GRAM 100 ZA MBOLEA MOJA WAPO (HASA NAPENDEKEZA PANDIA DAP, AU YARA MILLER WINNER) UTAYEYUSHA KATIKA MAJI LITA 20, THEN KWA KILA SHIMO UTAWEKA HIZO MLS 250 KAMA STARTER SOLUTION NDIPO UPANDIKIZE MCHE. HIVYO UNAIWEKA IN FORM OF SOLUTION SIYO KAMA

"USIFANYE KINYUME, CHA KUPANDA MCHE KWANZA NDIO UWEKE HIYO STARTER SOLUTION"


Nimeipenda hii sana huenda ikawa na matokeo ya haraka mno nina hoho zangu ziki kitaluni ntafanya hivo pia.
 
Niliweka mbolea shambani aina ya dap wakati napandikiza miche ya nyanya, sasa nikaishiwa miche na mistari kadhaa ikabaki ikiwa na mbolea. Naomba kuuliza je nikienda kupandikiza miche mingine baada ya wiki mbili ,ile mbolea itakuwa bado na nguvu au itatakiwa niongeze nyingine? Asante.
 
KIONGOZI
NTAKUELEZA ZAIDI KATIKA MATIKITI MAANA NIKO NA UZOEFU NAYO

KAMA MAZAO YOTE YANATAMBAA SI VIZURI SANA UKICHANGANYA

TIKITI,

UDONGO NA JOTO


Usiwe wa kutuamisha maji
Ukiwa Tifutifu, AU kichanga Tifutifu (Clay loam) na hali ya joto kiasi angalau 15- 35 degree inatosha sana
Linahitaji maji mengi mwanzoni lakini kadri linavyoendelea maji unapaswa kupunguza


MUDA WA KUOTA


Ukisia mbegu huchukua siku 5 hadi 10 kuota


KAMA SHAMBA LIKO TAYARI BY NOW, UKIPANDA SIKU 75 HADI 90 (AINA ZA MBEGU ZILIZOPO SOKONI KWA SASA NI HYBRID -ZEBRA, 1. SUKARI F1, 2. MSHINDI, 3. JULIANA ETC) UNAVUNA TIKITI KWA HIYO UNAMIEZI 3, OKT, NOV NA DEC WAKATI TUNAKABIA MWAKA MPYA UNAVUNA.


KWA TIKITI JITAHIDI SANA KUPANDA KWA NAFASI


KAMA UTALIMA MATUTA BASI TUTA LIWE LIMEINUKA KIASI KUJA JUU WALAU SM 20 HIVI LIWE NA UPANA WALAU WA SM 45 HADI 60, UPANDAJI, KUTOKA SHIMO HADI SHIMO SM 90 HADI 100, NA KUTOKA KATIKATI YA TUTA HADI TUTA LINGINE NI MITA 1.5=SM 150, KWA HIYO KWA MATUTA YANAYOFUATANA TIKITI ZIIKIANZA KUTAMBAAA UNAZILAZA ZINAKUTANA KATIKATI YA HIZO TUTA MBILI


KAMA UTAAMUA KUPANDA KWA MAJARUBA KAMA HAYA YA MPUNGA, AMBAPO WATU WENGI HUMWAGIA KWA KUTENGENEZA MITALO YA KIENYEJI YA UMWAGILIAJI BASI, JARUBA LAKO LINAPASWA KUWA NA UPANA WA MITA 3 NA UREFU WOWOTE ULE HATA WA MITA 5 ILI MRADI UWEZE KUMUDU KUINGIZA MAJI.


SASA KWA JARUBA TUNAPANDA PEMBENI KATIKA ANGLE HIZO. KUTOKA SHIMO HADI SHIMO NI HIZO SM 90 (=futi tatu), AMBAPO SASA YAKIAANZA KUTAMBAA UTAYALAZIA KATIKATI HAPO KATIKA HUO UPANA WA MITA 3, SO YA KULIA YATAKUJA HAPO CENTRE, YA KUSHOTO , KASK, NA KUSINI HIVYO HIVYO YANAKUJA KULALA HAPO


MBOLEA ZA KUPANDIA NI MUHIMU SANA


UKIPATA YARA MILA WINNER ( NAMBA HIZI 15:9;20 AINA YA NPK) ITAKUFAA KILA SHIMO UNALOWEKA MBEGU MOJA WEKA GRAMA 10 YA MBOLEA SWA NA KIJIKO KIMOJA KIKUBWA CHA WALI. ZITAOTA BADA YA SIKU 5 HADI 10


AFTER ONE MONTH, UTAWEKA MBOLEA YA KUKUZIA KAMA CAN AU UREA


MAUA YAKIJA JITAHIDI UPATE BOOSTER (HIZO NI MAALUMU KWA AJIRI YA MAUA NA MATUNDA


ZIPO BOOSTER ZINAITWA STAARTER- MFANO HALISI ZILIZOPO MADUKANI NI POLYFEED STARTER-HIZO HUTUMIKA KUPIGA MAUA WAKATI WA MAUA


MATUNDA YAKIJA UTAWEKA POLYFEED FINISHER-HIYO NI KUIMARAISHA MATUNDA, NA PIA UTAFUTE MBOLEA INAITWA YARA NITRABOR (HII INA Calcium na Nitrojen kwa wingi) , husaidia kuzuia tikiti kunyauka, na kuzoa katika kitako-Ugonjwa unaitwa Blosom End Rot

WAKATI WOOTE WA MAISHA YA TIKITI USISAHAU DAWA ZA WADUDU, WANAOKATA MAUA , NA KUTOBOA MATUNDA, DAWA KAMA DUDU ALL AU SELECRON, AU MATCH, AU KARATE MOJA WAPO YATOSHA KUMALIZA WADUDU


LAKINI WAKATI WA KUPIGA HIZI DAWA KUWA MAKINI SANA USIPIGE MCHANA, UTAUWA NYUKI WA KUFANYA UCHAVUSHAJI KUTOFANYIKA-HAPO UTAPATA DIFORMALITIES NYINGI SANA KAMA SHAPELESS KATIKA MATUNDA, PIGA ASUBUHI SANA AU JIONI SANAA,




PIA KAMA UTAONA KUNA HALI YA UKUNGU (UNYEVU NI MWINGI AU BARIDI USIKU AU MCHANA) NI MUHIMU KUWEKA DAWA ZA JAMII YA COPPER, KAMA BLUEE COPPER, AU EBONY KUZUIA UKUNGU,


NI MUHIMU SANA KUHAKIKISHA TIKITIKI ZAKO ZINAPATA MAJI WALAU MARA 3 KWA WIKI, ILI KUPUNGUZA WATER SRESS


GHARAMA ZA MBEGU

KWA EKARI MOJA UTAHITAJI Gram 300 za mbegu , ambapo jumla ya gharama za mbegu ni kati ya tsh 200,000 hadi tsh 300,000

MAVUNO

Kwa kuwa kwa nafasi tajwa hapo juu utakuwa na mashimo yasiyopungua katiya 2000 hadi 3000 Kwa ekari moja. Hivyo kila shimo au kila kamba ya tikiti ikikupa matikiti matatu means utakuwa na mavuno ya vichwa vya tikititi kati ya 6000 hadi 9000, ambayo ni sawa na wastani wa tani 12 hadi 18 kwa ekari moja

Karibu Kiongozi

Asante kwa somo hili la tikiti maji.Mkuu ni mara yangu ya kwanza kulima tikiti maji, nimelima aina ya SUKARI F1 yana wiki tatu sasa,niseme tu kwamba sikupanda na mbolea yeyote na wala sijatumia dawa ya kuuwa wadudu hizo ulizotaja hapo kutokana na aliyenishauri kutumia Dawa ya AGRI FOS 400 kwamba inaua pia wadudu japo haifanyi kazi maana wadudu wanakata majani na pia kuna miche inakauka kutoka chini nikashauriwa kutumia AGRI- FOS 400 lakini tatizo bado linaendelea.baada ya kusoma maelezo yako sijaona hii dawa,naomba kujua kuhusu hii dawa isije ikawa inamadhara kwenye miche hii ya tikiti maana nimepiga mara tatu sasa. Na pia naomba kuuliza je kuna booster ya kupiga kwenye miche ambazo bado hazijatambaa ili zitambae haraka?.,Asante
 
Agri fos 400 kutoka kampuni ya balton ni kiboko sana na magonjwa ya mnyauko hasa kwenye nyanya, hoho na mazao mengine ile dawa inaiingia moja kwa moja kwenye mizizi na kutibu, nimepiga kwenye nyanya zangu hivi karibun zilizokua na late bright nimeanza kuona mabadiliko
 
Mkuu EMoj kwa ushauri zaidi ingia google then tafuta iyo dawa ina maelezo yalijitisheleza uku ukimsubiri ndugu yetu Kilimo maaarifa kujibu maswali yako
 
Back
Top Bottom