neha mimi
JF-Expert Member
- Aug 19, 2014
- 344
- 151
ilikuwa ni saa sita kasoro usiku..maeneo ya nguzo mbili ungalimited,tulikuwa kundi la vijana kama nane tukiwa na mapanga na marungu,tukiwa tunapandisha esoo kutafta riziki kwa kazi zetu zile za usiku,mbele kulikuwa na ngari ndogo[tax]ilikuwa inashuka kuelekea mitaa ya sinoni,mmoja wetu alirusha kitofali kwenye ile gari na kupasua kioo ghafla dereva akakosa muelekeo na kungonga nguzo.ndipo tulitoka na mapanga na kuvamia ile gari kwa lengo la kupora na kukata kata walio humo ndani...hamadi macho yangu mekundu,yalio jawa na uharamia,na sura langu gumu nidhairi utajua nilivyo mkatili....nilikutana na macho ya msichana mrembo ambae alikuwa analia kwa kuomba msaada,ghafla niliingiwa roho ya kimalaika nakumpenda yule binti.ndipo nikawambia manyangau wezangu hakuna ruhusa ya kupora pale wala kumzuru yule binti.ilitokea ugovi mkubwa sana kwa vile nilikua mtemi kama mkwawa niliwazidi nguvu japo nilikatwa panga la paji la uso.ila niliondoka na yule binti mpaka kwao....msichana hakukubali aliniambia nimeumia twende hosptal.from hapo ndo ikawa mwazo wa mahusiano yangu na yeye ambae leo ni mama watoto na mimi nimeamua kumfata yesu
waaaoh umefanya maamuzi mazuri ya kumfata Yesu ubarikiwe