GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Hii ni kwa wale wazee wenzangu ambao enzi zetu auditor alionekana kama askari polisi au ametumwa kutafuta mwizi
Kuna wakati huwa nacheka ofisi haina Controls zozote za pesa miaka nenda rudi halafu kila mwaka unatuma auditors wakafanye kitu gani?
Mapungufu ya Control za ndani kuna wakati yalimkasirisha Rais Marehemu JPM na kuamrisha pesa zote za serikali kwenye Benki za biashara ziende Bank of Tanzania na yeye akajikuta ameingia kwenye mkumbo ule ule wa kutoweka kwa 1.5 Trilioni halafu zigo akadondoshewa Prof Assad Mkaguzi mkuu ajibu kama pesa zimetoweka au La! pale Ikulu Dar
Kwa tukio la 1.5 Trilioni lilionyesha kuna mapungufu makubwa kwenye internal control yaani mtu anaweza badili matumizi ya pesa zilizopangwa na Bunge atakavyo yeye kwa mamlaka yake na hakuna control yeyote iliyopo ya kumdhibiti mtu huyo
Cha kushangaza na kuchekesha zaidi bado watu hao unawatungia sheria kuwa "Wafanye lolote lile la uwizi au ufisadi hawatashtakiwa na mtu yeyote kwa makosa ya uwizi na ufisadi walipokuwa madarakani"
Unapunguza control ya kuwashtaki halafu unamwambia auditor akakague ofisi ya Jaji mkuu na Spika wabunge huku si kupoteza muda wa auditor?
Enzi hizo za sisi wahenga Mkaguzi hakutoa taarifa wala hakutoa hadidu za rejea alivamia ofisi ghafla kama vita lakini bado watu waliwadhibiti auditors na waliendelea na kazi mpaka wakastaafu ingawa baadhi walifungwa kwa fitina ndani ya ofisi lakini sio kutokana na report ya CAG kuwa wamekwapua pesa
Dunia ya kidigital watu wanajua auditor anakuja lini na hadidu za rejea ni zipi, Tatizo la sasa ni vijana kutafuna pesa na kusahau kuweka document sawa, Lakini ukiwapa muda kelele zote hizo zinaisha
Auditing sio vita wala mapambano, Audit ni kelele kama kelele zingine tu zinazohitaji uzuiaji, Na kuna mbinu nyingi za kuzuia kelele za auditor
Document na receipt zinazokosekana kwenye maswali ya auditor zinajibika na Kutengenezwa
Ukisikia auditor anabweka ujue kuna document kadhaa kutokana na muda wahusika walishindwa kuweka sawa lakini ukiwapa muda maswali yote ya auditor yana majibu
Auditor akishapewa document zake basi wananchi mtasubiri Audit ya mwaka mwingine na mtapiga kelele tena za wizi zilizozoeleka miaka nenda rudi
Zamani enzi zetu auditor alidhibitiwa kwa kulambishwa asali na kupewa mapochopocho mfano gunia la mchele, gunia la mahindi, na wakati mwingine anakabidhiwa mrembo, Baada ya week zake za Audit anarudi kwenye Familia yake na full gunia za mchele na mapochopocho hapo tegemea hati safi
Ukisikia watu wamepata hati chafu ujue kamati ya fitina na Majungu haikujipanga vizuri, Waliojipanga vizuri auditor hawezi toa hati chafu
Laiti kama watu wangejua maana ya auditing Tanzania wasingepiga kelele eti kuna wizi unafanyika kila mwaka
Hakuna uwizi unafanyika kila mwaka bali kuna mapungufu ya internal control za taasisi husika
Mtapiga kelele kila mwaka lakini tiba ya mambo haya ni katiba mpya
Katiba yetu kuna mahala inajichanganya sana na kuna muda watu hawajui mwisho wa mamlaka yao
Kuna watu wanaambiwa toa pesa hiyo ya barabara ikajenga shule ya kata, Akija auditor anaona kuna makosa lakini huyu mtumishi ameamrishwa
Bila katiba mpya itakayotofautisha mamlaka ya wanasiasa na Serikali basi tegemea report ya CAG ile ile na wanaosomewa ni wale wale na wezi ni wale wale (Nukuu ya Tundu Lisu)
Kuna wakati huwa nacheka ofisi haina Controls zozote za pesa miaka nenda rudi halafu kila mwaka unatuma auditors wakafanye kitu gani?
Mapungufu ya Control za ndani kuna wakati yalimkasirisha Rais Marehemu JPM na kuamrisha pesa zote za serikali kwenye Benki za biashara ziende Bank of Tanzania na yeye akajikuta ameingia kwenye mkumbo ule ule wa kutoweka kwa 1.5 Trilioni halafu zigo akadondoshewa Prof Assad Mkaguzi mkuu ajibu kama pesa zimetoweka au La! pale Ikulu Dar
Kwa tukio la 1.5 Trilioni lilionyesha kuna mapungufu makubwa kwenye internal control yaani mtu anaweza badili matumizi ya pesa zilizopangwa na Bunge atakavyo yeye kwa mamlaka yake na hakuna control yeyote iliyopo ya kumdhibiti mtu huyo
Cha kushangaza na kuchekesha zaidi bado watu hao unawatungia sheria kuwa "Wafanye lolote lile la uwizi au ufisadi hawatashtakiwa na mtu yeyote kwa makosa ya uwizi na ufisadi walipokuwa madarakani"
Unapunguza control ya kuwashtaki halafu unamwambia auditor akakague ofisi ya Jaji mkuu na Spika wabunge huku si kupoteza muda wa auditor?
Enzi hizo za sisi wahenga Mkaguzi hakutoa taarifa wala hakutoa hadidu za rejea alivamia ofisi ghafla kama vita lakini bado watu waliwadhibiti auditors na waliendelea na kazi mpaka wakastaafu ingawa baadhi walifungwa kwa fitina ndani ya ofisi lakini sio kutokana na report ya CAG kuwa wamekwapua pesa
Dunia ya kidigital watu wanajua auditor anakuja lini na hadidu za rejea ni zipi, Tatizo la sasa ni vijana kutafuna pesa na kusahau kuweka document sawa, Lakini ukiwapa muda kelele zote hizo zinaisha
Auditing sio vita wala mapambano, Audit ni kelele kama kelele zingine tu zinazohitaji uzuiaji, Na kuna mbinu nyingi za kuzuia kelele za auditor
Document na receipt zinazokosekana kwenye maswali ya auditor zinajibika na Kutengenezwa
Ukisikia auditor anabweka ujue kuna document kadhaa kutokana na muda wahusika walishindwa kuweka sawa lakini ukiwapa muda maswali yote ya auditor yana majibu
Auditor akishapewa document zake basi wananchi mtasubiri Audit ya mwaka mwingine na mtapiga kelele tena za wizi zilizozoeleka miaka nenda rudi
Zamani enzi zetu auditor alidhibitiwa kwa kulambishwa asali na kupewa mapochopocho mfano gunia la mchele, gunia la mahindi, na wakati mwingine anakabidhiwa mrembo, Baada ya week zake za Audit anarudi kwenye Familia yake na full gunia za mchele na mapochopocho hapo tegemea hati safi
Ukisikia watu wamepata hati chafu ujue kamati ya fitina na Majungu haikujipanga vizuri, Waliojipanga vizuri auditor hawezi toa hati chafu
Laiti kama watu wangejua maana ya auditing Tanzania wasingepiga kelele eti kuna wizi unafanyika kila mwaka
Hakuna uwizi unafanyika kila mwaka bali kuna mapungufu ya internal control za taasisi husika
Mtapiga kelele kila mwaka lakini tiba ya mambo haya ni katiba mpya
Katiba yetu kuna mahala inajichanganya sana na kuna muda watu hawajui mwisho wa mamlaka yao
Kuna watu wanaambiwa toa pesa hiyo ya barabara ikajenga shule ya kata, Akija auditor anaona kuna makosa lakini huyu mtumishi ameamrishwa
Bila katiba mpya itakayotofautisha mamlaka ya wanasiasa na Serikali basi tegemea report ya CAG ile ile na wanaosomewa ni wale wale na wezi ni wale wale (Nukuu ya Tundu Lisu)