Je, toyota IST inafaa kwa safari za mkoani?

Hahahah mkuu chombo kikiwa na engine..unaenda nacho popote usiogope kikubwa service..halafu unatembea mwendo laini wa 50-80kph unafika vizuri tu. Pikipiki inatoboa mwanza vizuri tu(kitachomchosha devera ni makalio kuwaka moto kutokana na umbo la kiti cha pikipiki) sasa gari inashindwa vipi.
 
Mi huwa natoka nayo DAR to Kampala DAR gari yeyote inafika ila Sema siku zinaongezeka dar kampala huwa natumia siku tatu nikitoka Kampala asubuhi nalala tinde then napumzika kuepuka tochi naondoka tinde jion kuitafuta Dom obvious nafika usiku mnene then nalala Dom to DAR masaa kumi tu Kampala dar ni Wastani km 1800 IST ulaji wake wa wese inakwenda km 13-16 kwa Lita
 
Mi huwa natoka nayo DAR to Kampala DAR gari yeyote inafika ila Sema siku zinaongezeka dar kampala huwa natumia siku tatu nikitoka Kampala asubuhi nalala tinde then napumzika kuepuka tochi naondoka tinde jion kuitafuta Dom obvious nafika usiku mnene then nalala Dom to DAR masaa kumi tu Kampala dar ni Wastani km 1800 IST ulaji wake wa wese inakwenda km 13-16 kwa Lita
Upo sahihi kabisa
 
Mimi nilisafiri na Passo Piston3 kutoka Dar mpaka Mwanza nilitoka Dar saa 9 kama na nusu nikaingia Mwanza saa 2 usiku wala sikupata tatizo lolote njiani wala sikupigwa Tochi ilikuwa mwaka jana mwezi wa 10 na niliendesha mwenyewe muda wote wa safari.
Kabisa woga wao tu vits piston 3 nimepiga nayo singida na kurudi tu vizuri,hakuna hata kugusa maji sijui wala oil imepungua na speed nzuri tu 100 max 120 nimefika vizuri na siku ya kurudi nimetoka 12 asubuhi nimefika dar 10 jioni na iko shwari tu sijaona hayo maswala ya feni kuzingua
 
Iyo gari inafika hata south africa ukitaka. Mbona kuna gari kibao (In transit) kama IST, Noah, na nyinginie kbao zinasafiri toka Bongo hadi zimbabwe, Zambia, Malawi, DRC, Rwanda na Burundi. Sasa itakuwa hapo Usukumani
 
Endapo utafika na kuzima gari hapo hapo ambayo imetoka safari ya mbali hali hiyo inaweza kisababisha piston kung'ang'ania kwenye block kumbuka piston zinakuwa zinapishana nyingine zinapanda juu na nyingine zinashuka chini gari iapokuwa inatembea au kupinda cylinder head kumbuka chuma aina ya cast ambacho ndhicho hutengenezea vitu hivi nilivyovitaja vinataboa ya kutanuka vinapopata joto sana na vinatabia kusinyaa kwa ghafla vinapopata baridi hivyo huweza kubana piston vinaposinyaa kwa ghafla au sleav kupinda au hata camshaft kupinda au main na con kulika kwa urahisi ambazo ndizo zinashikilia cam shaft kwa kuwa vyuma vyote vinakuwa na moto sana na unapozima gari kwa ghafla unasababisha oil kushuka kwa kasi kwenye sample kwani inakuwa imeyeyuka sana na ni ya moto hivyo inauwezo wa kupita kwa kasi kwenye matundu yake na kushuka chini na kumbuka wakati huo ukizima gari oil pump ambayo kazi yake ni kupandisha oil juu hadi kwenye cylinder head ili vyuma vyote nilivyovutaja vipate oil ili vilainike vitakosa oil kwani nayo oil pump itazima kwa ghafla na hata kama feni ilikuwa inapuliza nayo itazima kwa gahfla na ndio maana huweza kuleta madhara makubwa kwenye injini. Na sio tu unapofika mwisho wa safari unashauriwa kuzima gari bali hata unapotaka kusafiri safari ya mbali unashauriwa uwashe gari yako kwa dakika 15 kwanza uiache ingurume ili kuweka uwiano sawa wa joto kwenye injini yako ili iweze kukabili safari unayotaka kwenda sio vyema unapotaka kusafiri safari ya mbali hapo hapo unawasha gari na kianza safari yako. Kama una swali zaidi karibu mkuu
Duh... hizi shule za siku hizi si mchezo....
 
Napingana nawewe kwenye swala LA 70kph kwann kwanza kabisa hizo gari wasingetoa na speed limit ya 160.wangetoa speed 90 kama ilivyokuwa kwa Volkswagen na Peugeot za zaman.2.barabara Japan na nchi za wenzetu zilizoendelea hatuwezi jifanananisha hata kidogo.cc tunatembea30. 50. Ukibonyeza kidogo 50 hiyo.wenzetu kunamahali huruhusiwi kuendesha chini ya 120kph.

Hili LA kuzima gari baada ya kutoka safari ndefu nakubaliana na wewe.ila nakuuliza MFANO nimetoka mbeya nakuja dar nimefika chalinze gari haItembei tena ule mwendo niliokuwa nao kutoka mbeya -chalinze, sasa natembea 70, 60,20 nafika kimara sasa ndio kusimama na kusogea he nikifika sinza kuna haja ya kuacha gari silence?
Kuna tofauti kubwa sana kwenye uzimaji wa gari kwa engine za petroli na za dizeli zinapokuwa zimetembea mwendo mrefu....

Sijui kwanini watu hawapendi kujifunza...
 
Kabisa woga wao tu vits piston 3 nimepiga nayo singida na kurudi tu vizuri,hakuna hata kugusa maji sijui wala oil imepungua na speed nzuri tu 100 max 120 nimefika vizuri na siku ya kurudi nimetoka 12 asubuhi nimefika dar 10 jioni na iko shwari tu sijaona hayo maswala ya feni kuzingua
Kabisa mkuu well saidi, uwoga wake tuu ! Hizi machine zipo vizuri kabisa.
 
Nimetoka na kavitz kangu Arusha to Dar halafu nikarudi Arusha.Hakuna kupumzika ni mwendo tu.
 
Gari yoyote yenye piston 4 na kuendelea unaenda nayo popote unapofikiria kwenda. Nilitumia siku mbili tu kutoka dar paka kigali na hio ist bila hata kufungua bonet.
 
Unajua nimegundua watanzania wengi ni wageni kwenye hii taluuma ya magari.
Toyota probox ni mashine hasa ,usikaone kadogo hako kagari .Unaweza kusafiri nako km 1600 huku kamebeba kg450 kwenye buti na abiria watano.
Wengi wetu hatufahamu mkuu, humu ndio sehem y kujuzana n kupata maarifa zaidi, nmeona hii story nikaogopa maana unaweza ua gari kwakua tuu huelewi, shukrani mleta huu uzi
 
Back
Top Bottom