Je, ni Sahihi Kumjua mtu kupitia mtu?

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Aug 6, 2020
3,520
6,503
Jana nikiwa nimejipumzisha zangu nikajisikia kusikiliza Redio kidogo basi mara nyingi ikitokea Nataka kusikiliza matangazo ya Redio basi Tbc Taifa ndio sehemu muafaka kwangu Kule huwa napata kitu roho inapenda,maana hizi Redio za niaje niaje mtu wangu na collection ya miziki Yao ya kamata kiuno sijui shika bega aah zinaniboa Sana.

Basi nikakuta miongoni mwa mambo yaliyo kuwa yanajadiliwa katika kipindi kile ni pamoja na msemo unao wataka wasikilizaji kutoa maoni kuhusu "kumjua mtu kupitia mtu"

Ni msemo ambao unamaanisha kwamba ukitaka kumjua mtu basi utamjua kupitia labda rafiki yake wa karibu au mtu wake wa karibu ambaye wanafahamiana Sana. Ni kweli hiyo na njia moja ya kumfahamu mtu na kupata taarifa zake mbali mbali lakini Kwa maoni yangu unaweza vile vile usipate taarifa zake sahihi kutokana na mambo kadhaa.

Kwa mfano huenda unataka upate taarifa za ETUGRUL BEY kupitia Mokiti lakini kumbe hapo awali walikuwa marafiki Wazuri Sana,lakini baadae wakaja kutofautiana na kugombana kwahiyo utakapoenda Kwa Mokiti utake taarifa za ETUGRUL BEY lazima atatoa taarifa hasi na mbaya ili kumchafua mhusika kwasababu wameshakuwa mahasimu tayar.

Lakini kuna mazingira mengine,huenda unatafuta taarifa za Mademoiselle Kwa mfano labda unataka kumpa dili Fulani au kuna maslahi fulani anaweza faidika nayo Kwa kuulizia taarifa zake Kwa Kalpana kama best yake ni mfano tu,basi kuna uwezekano mkubwa Kalpana asitoe taarifa sahihi ili huyo mlengwa asifaidike na Jambo Fulani, jamani natoa mifano Tu hapa Kwa kutumia Id zenu sio kwamba ndio mko hivyo.

Kwahiyo Kwa kifupi wakati mwingine ni sahihi kumjua mtu kupitia mtu lakini na wakati mwingine inaweza kuwa kinyume chake kabisa,kwahiyo cha msingi wakati unataka kumjua mtu kupitia mtu basi jitahidi na Kwa upande mwingine kufanya utafiti wako binafsi halafu linganisha na data utazopata kutoka Kwa mtu wake wa karibu halafu upate majibu sahihi.

Ni hayo Tu!

Mamndenyi
baby zu
To yeye
 
Ni kweli kabisa mkuu ETUGRUL BEY ...ila mimi hata mtu aniudhi vipi ukitaka reference yake nitakupa iliyo halisi....haina haja ya kumchafua mtu eti kisa mlipishana wakati sivyo alivyo..maana hata ww mwenyewe sio mkamilifu una makando kando kibao...

Lakini hii yakumjua mtu kupitia kwa mtu/watu kuna muda/mara nyingi ina work kama watatokea watu 5 wakasema tabia hyo hyo basi ni kweli ndivyo ulivyo..
 
Ni kweli kabisa mkuu ETUGRUL BEY ...ila mimi hata mtu aniudhi vipi ukitaka reference yake nitakupa iliyo halisi....haina haja ya kumchafua mtu eti kisa mlipishana wakati sivyo alivyo..maana hata ww mwenyewe sio mkamilifu una makando kando kibao...

Lakini hii yakumjua mtu kupitia kwa mtu/watu kuna muda/mara nyingi ina work kama watatokea watu 5 wakasema tabia hyo hyo basi ni kweli ndivyo ulivyo..
Kwanza hongera madam kama uko hivyo hakika mko wachache Sana

Pili umeeleza vizur kabisa nakubaliana na wewe ukiona story ya watu wengi inafanana ujue ni kweli.

Shukran sana
 
Ndio maana serikalini kuna kitengo cha vetting na due delligence.
Watu wanasomea hizi kazi,nje ya hapo utakuwa unafanya umbea na majungu
 
Kumjua mtu kupitia watu haimaanishi kuwa ukaulize hao watu juu ya huyo mtu, hapana. Bali ni utamjua mtu kutokana na aina ya watu anaojihusisha nao, ila hao watu anaojihusisha nao huna sababu ya kuwauliza juu ya huyo mtu.

Yaani kupitia mahusiano ya mtu na watu utaweza kufahamu mitizamo yake, mawazo yake, imani yake, tamaduni anayoifuata, n.k japo navyo sio lazima vikafanana na vya hao watu.

Kwa ufupi kumjua mtu ni kazi ngumu sana inayoweza kuchukua miaka, mfano mzunguko wa mtu wapo washikaji wanaonunua malaya, wapo wanaopiga gambe, wapo wazee wa kubeti, wapo wa ibada, na kuna wale wanaopenda wadada wenye misambwanda ili basi tu waiangalie wakitembea.

Mtu kumjua ni kazi sana
 
Kumjua mtu kupitia watu haimaanishi kuwa ukaulize hao watu juu ya huyo mtu, hapana. Bali ni utamjua mtu kutokana na aina ya watu anaojihusisha nao, ila hao watu anaojihusisha nao huna sababu ya kuwauliza juu ya huyo mtu.

Yaani kupitia mahusiano ya mtu na watu utaweza kufahamu mitizamo yake, mawazo yake, imani yake, tamaduni anayoifuata, n.k japo navyo sio lazima vikafanana na vya hao watu.

Kwa ufupi kumjua mtu ni kazi ngumu sana inayoweza kuchukua miaka, mfano mzunguko wa mtu wapo washikaji wanaonunua malaya, wapo wanaopiga gambe, wapo wazee wa kubeti, wapo wa ibada, na kuna wale wanaopenda wadada wenye misambwanda ili basi tu waiangalie wakitembea.

Mtu kumjua ni kazi sana
Chief asante Kwa maoni yako nimekupata vizur sana
 
Ni kweli kabisa mkuu ETUGRUL BEY ...ila mimi hata mtu aniudhi vipi ukitaka reference yake nitakupa iliyo halisi....haina haja ya kumchafua mtu eti kisa mlipishana wakati sivyo alivyo..maana hata ww mwenyewe sio mkamilifu una makando kando kibao...

Lakini hii yakumjua mtu kupitia kwa mtu/watu kuna muda/mara nyingi ina work kama watatokea watu 5 wakasema tabia hyo hyo basi ni kweli ndivyo ulivyo..
Mkuu ikatokea huyo mtu alikudhulumu na anatakiwa apewe kazi labda bank utacomment vipi?

Sent from my Nokia C2 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu ikatokea huyo mtu alikudhulumu na anatakiwa apewe kazi labda bank utacomment vipi?

Sent from my Nokia C2 using JamiiForums mobile app
Nimesema nitatoa kile kitu halisi kinachomhusu..yani kama anatabia mbaya nitasema kama nzuri nitasema..hapa nimesema sitamkandia mtu kisa tuu labda tumetofautina na najua sio tabia zake ila kisa tuu tumetofautiana basi nimsagie kunguni..
 
Back
Top Bottom