Ndugu wana JF,
Naandika kuuliza swali nikiwa na simanzi kubwa rohoni.
Nimempoteza rafiki yangu katika mazingira tatanishi. Rafiki yangu hivi karibuni aliweka bayana nia yake ya kugombea ubunge Kwimba. Aliamua kufanya hivyo baada ya kuombwa na kushawishiwa na wazee pamoja na vijana jimboni. Baada ya kutafajali alikubali na kuweka bayana msimamo wake. Suala la Ubunge kwake sasa ilikuwa ni suala la muda na kukamilisha utaratibu tu! Ghafla rafiki yangu amekutwa na mauti ambayo kuja kwake ni tata zaidi ya kifo cha Amina Chifupa.
Binafsi sikuwa nimeitwa au kuombwa na yeyote nikagombee. Lakini nilikuwa ninataka nikagombee kwa dhati ya kulitumikia jimbo langu na taifa langu. Tatizo linalonipata sasa ni hii sayansi inayowamautisha ghafla wenye nia na Ubunge au Uongozi Mkubwa wa Kisiasa.
Sijawahi kwenda kwa mpiga ramli au kuchanjiwa. Sasa, je:
Naandika kuuliza swali nikiwa na simanzi kubwa rohoni.
Nimempoteza rafiki yangu katika mazingira tatanishi. Rafiki yangu hivi karibuni aliweka bayana nia yake ya kugombea ubunge Kwimba. Aliamua kufanya hivyo baada ya kuombwa na kushawishiwa na wazee pamoja na vijana jimboni. Baada ya kutafajali alikubali na kuweka bayana msimamo wake. Suala la Ubunge kwake sasa ilikuwa ni suala la muda na kukamilisha utaratibu tu! Ghafla rafiki yangu amekutwa na mauti ambayo kuja kwake ni tata zaidi ya kifo cha Amina Chifupa.
Binafsi sikuwa nimeitwa au kuombwa na yeyote nikagombee. Lakini nilikuwa ninataka nikagombee kwa dhati ya kulitumikia jimbo langu na taifa langu. Tatizo linalonipata sasa ni hii sayansi inayowamautisha ghafla wenye nia na Ubunge au Uongozi Mkubwa wa Kisiasa.
Sijawahi kwenda kwa mpiga ramli au kuchanjiwa. Sasa, je:
- Inawezekana kweli mgombea kusimama katika siasa za kiwango hicho bila kinga na asimautishwe?
- Ni wapi zinapatikana kinga za ulinzi zenye viwango (ISO) vya uhakika?