mwankuga
JF-Expert Member
- Aug 30, 2010
- 334
- 120
"Nafurahi kwamba asili yangu ni kijiji hiki kidogo masikini,nataka kusema hili kwa ajili ya historia,najisikia fahari kuzaliwa katika familia masikini na naahidi kwamba nitaishi maisha ya kimasikini na nitakufa nikiwa masikini".
Maneno hayo hapo juu yalitamkwa na mjamaa wa Kiarabu Abdul Nasser(rais wa kwanza wa Misri) akihutubia wananchi kijiji kwao.Nimenukuu maneno hayo kwa makusudi sana ili kuonyesha taswira ya kile nitakachokiandika katika makala hii.
Maneno hayo yanaweza kulaaniwa vikali na vijana wengi toka barani Afrika,wanaopenda kuwa matajiri wa haraka pasipo hata kufanya kazi kwa bidii na maarifa.Ukimuuliza kijana wa Afrika katika maisha yake angependa awe nani,haraka angesema,nyumba nzuri,gari nzuri,mke mzuri n.k.Ukimuuliza zaidi anapenda afanye kazi gani,bila shaka angetaja,uhasibu,uanasheria,udaktari,uinjinia n.k
Bila shaka kazi ya ualimu au pengine ukulima haiwezi kutajwa na jibu lake ni jepesi sana,vijana au Waafrika wengi wanapenda sana shughuli za utanashati na si za kuchafua mikono kama wakulima.Kazi za mikono na jasho hazipendwi kabisa batrani Afrika.Wakulima si tu wanapuuzwa na kudharauliwa bali pia wananyanyaswa na kukandamizwa na kikundi kidogo cha watu.
Katika hali ya joto kama Dar suti au makati hayabanduki kwenye miili ya maofisa,utathani pengine nchi kama Tanzania hamna shida kabisa,mbwembwe za mahakimu na mawakili wa serikali na wakujitegemea,ungethani pengine ndani ya mahakama kuna haki,utakuwa unajidanganya.
Askari wa barabarani ni mzaha mtupu wako tayari wapate Tshs 500 toka kwa makondakta kwa gharama ya vifo.Hapa Tanzania twaweza hasa kutangaza kuwa ajali za barabarani ni janga la kitaifa.Tumepoteza ndugu wengi kwa ajali za barabarani,lakini sijaona hatua madhubuti zikichuliwa na wateule wetu.
Kifupi kuna matatizo mengi katika maisha yetu ya kila siku,na pengine kutokana na uelewa wangu mdogo,sijaona hatua zozote zikichukuliwa.Nani anaweza kuwa kama Abdul Nasser wa sasa,nani aweza kuwa kama wana halisi wa Afrika kama Nyerere,nani ana uchungu na maisha ya watanzania,nani anaumizwa toka moyoni na hali za masikini waliotapakaa kote Tanzania.
Vipi wenzangu mnaonaje?naomba mnisaidie nimchague nani kuwa rais wa Tanzania,atakaye kuwa tayari kunywa mvinyo na sifongo na watanzania wote.Kwa kweli naomba msaada ndugu zangu.
Maneno hayo hapo juu yalitamkwa na mjamaa wa Kiarabu Abdul Nasser(rais wa kwanza wa Misri) akihutubia wananchi kijiji kwao.Nimenukuu maneno hayo kwa makusudi sana ili kuonyesha taswira ya kile nitakachokiandika katika makala hii.
Maneno hayo yanaweza kulaaniwa vikali na vijana wengi toka barani Afrika,wanaopenda kuwa matajiri wa haraka pasipo hata kufanya kazi kwa bidii na maarifa.Ukimuuliza kijana wa Afrika katika maisha yake angependa awe nani,haraka angesema,nyumba nzuri,gari nzuri,mke mzuri n.k.Ukimuuliza zaidi anapenda afanye kazi gani,bila shaka angetaja,uhasibu,uanasheria,udaktari,uinjinia n.k
Bila shaka kazi ya ualimu au pengine ukulima haiwezi kutajwa na jibu lake ni jepesi sana,vijana au Waafrika wengi wanapenda sana shughuli za utanashati na si za kuchafua mikono kama wakulima.Kazi za mikono na jasho hazipendwi kabisa batrani Afrika.Wakulima si tu wanapuuzwa na kudharauliwa bali pia wananyanyaswa na kukandamizwa na kikundi kidogo cha watu.
Katika hali ya joto kama Dar suti au makati hayabanduki kwenye miili ya maofisa,utathani pengine nchi kama Tanzania hamna shida kabisa,mbwembwe za mahakimu na mawakili wa serikali na wakujitegemea,ungethani pengine ndani ya mahakama kuna haki,utakuwa unajidanganya.
Askari wa barabarani ni mzaha mtupu wako tayari wapate Tshs 500 toka kwa makondakta kwa gharama ya vifo.Hapa Tanzania twaweza hasa kutangaza kuwa ajali za barabarani ni janga la kitaifa.Tumepoteza ndugu wengi kwa ajali za barabarani,lakini sijaona hatua madhubuti zikichuliwa na wateule wetu.
Kifupi kuna matatizo mengi katika maisha yetu ya kila siku,na pengine kutokana na uelewa wangu mdogo,sijaona hatua zozote zikichukuliwa.Nani anaweza kuwa kama Abdul Nasser wa sasa,nani aweza kuwa kama wana halisi wa Afrika kama Nyerere,nani ana uchungu na maisha ya watanzania,nani anaumizwa toka moyoni na hali za masikini waliotapakaa kote Tanzania.
Vipi wenzangu mnaonaje?naomba mnisaidie nimchague nani kuwa rais wa Tanzania,atakaye kuwa tayari kunywa mvinyo na sifongo na watanzania wote.Kwa kweli naomba msaada ndugu zangu.