Je, leo ni uhuru wa Tanzania Bara au Tanganyika?

Kafanye mambo yako upunguze umaskini wako na wa familia yako
Nimengalia mchango wako kwenye uzi wa Maxmello wa Jf kuhusu dr Mpango na nyuzi nyingine, nimegundua wewe kama si mcheza singeli basi ni mhudumu wa baa na huna exposure na mambo ya Tanganyika au la basi hata kujiunga ni muuza simu alikuunga jf bila wewe kujua na hujui kusoma, na kama unajua kusoma basi wewe ni mtoto wa mwenyekiti wa kitongoji ambapo wewe na familia yenu mnaishi kwa fedha za TASAF na una amini bila serikali hakuna uhai.
 
Serikali, Wananchi, Madaktari, mawaziri mpaka 2023 hawajui wao ni wenyeji wa nchi ipi, kuna wanaojiita ni Tanzania Bara, Tanzania, Tanganyika na wengine wanajiita ni Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Chawa Haki Ngowi anamripoti Samia kwamba tuna adhimisha uhuru wa Tanzania Bara [Uhuru wa Zanzibar ulikuwa lini?]

Waziri wa Maji Jumaa Aweso na naibu wake Meriprisca Mahundi ni wasoshalisti wanatuambia ni uhuru wa Tanganyika, hii ni kweli na huyu pepo ameshaiona. Hawa ndio mashujaa wa Taifa hili.

Wana JF, 9-12- ni uhuru wa nchi gani?

Angalia wizara yalivyojichanganya juzi;

View attachment 2840186
View attachment 2840159
View attachment 2840166
View attachment 2840167

09-12-2023 Tanganyika inasherehekea miaka 62 ya uhuru wa bendera toka kwa mkoloni wa Kiingereza.

Nakumbuka wakati tunapata uhuru Hayati Bwana Kambarage Nyerere, baba wa Taifa alisema, pamoja na uhuru huo, bado kama nchi tulikuwa na kazi ya kufanya kuendelea na mapambano dhidi ya maadui watatu wa nchi yetu ambao ni:

1. UJINGA
2. UMASKINI
3. MARADHI

Inasikitisha sana kuona ni wachache sana ambao wanafaidika na matunda ya uhuru huu "bandia" kutokana na kwamba viongozi wetu kwa sehemu kubwa wameshindwa kutuongoza vyema katika kukabiliana na maadui hao watatu wa Taifa letu.
Watu wachache waliokula asali ya "uhuru " wa bendera inajumuisha "wandani wa serikali " walioziwa nyumba za Serikali na uncle Ben kwa bei ya Passo, yaani nyumba ya Masaki -ukubwa ni eka na nusu anauziwa Waziri kwa milioni nne, tena analipa kwa instalment, baada tu ya kununua anakata robo heka akauza kwa bilioni mbili.

Kwa wakazi wa Dar -kutoka Posta[Upanga magharibi] mpaka Mwenge -Maeneo ya St Peters pale akina Zakhia Meghji wamenunua, Fatma Magimbi, Jaji Kaganda amenunua pale pembeni ya Puma enerrgy, Nyumba zote Seifee Hospitals, zile Yard zote mnaziona ni nyumba za serikali watu wamegawiwa, hii laana tuspotubu na hawa watu kurudishiwa fedha na nyumba kurudishwa serikalini basi hakika

Imefikia hatua wale tunaowaamini kutuongoza, wanakwenda kutumikia matumbo yao na ya familia zao pamoja na marafiki zao. Na kwa bahati mbaya sana wakishapewa dhamana, wanafanya kila linalowezekana kuhakikisha wanabaki kwenye nafasi hizo hata baada ya kustaafu!

Maisha yanazidi kuwa magumu kwa watu wa hali ya chini huku viongozi na wafanyabiashara wakubwa wakizidi kujilimbikizia ukwasi pasipo kujali maumivu ya wananchi wenzao.

Mbunge mmoja wa mkoa wa Pwani anafanya biashara na serikali, ana kampuni ya catering, anahudumia shughuli nyingi na ni conflict of interest.

kamati ya Bunge zinakodisha mabasi ya mbunge wa Morogoro kwa hela ya juu sana, watu wanakula matunda ya "uhuru wa bendera".


Hivyo kama Taifa, tunahitaji kubadili uelekeo, tufanye kila linalowezekana kuwaondoa madarakani viongozi hawa na badala yake tuweke wazalendo watakaokuwepo kwa ajili ya kusimamia maslahi ya wananchi wote kwa ujumla na kuhakikisha kila mwananchi anafaidi keki ya Taifa. Na hili kulifanikisha hilo, tunapaswa kufanya kila linalowezekana tupate Katiba mpya.

Katiba Mpya itatusaidia kuwadhibiti viongozi wetu na kuwafanya watutumikie kwa uzalendo na uadilifu, watake wasitake!
HAKUNA NCHI YA TANZANIA BARA

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
 
Wadau hivi karibunu NCHI yetu ilikuwa inasherehekia MIAKA 62 YA UHURU.

Kitu cha kushangaza nilichokisoma na kusikia katika Vyombo vya Habari Yakiwemo Magazeti Vituo vya TV na Mitandao mbalimbali ya Kijamii na kulikuwa na TANGAZO lisemalo "MIAKA 62 ya UHURU wa TANZANIA BARA".Ukweli nilishikwa na MSHANGAO MKUBWA nakujiuliza

1. TANZANIA BARA ni NCHI gani hiyo iliuopata Uhuru wake Miaka 62 iliyopita? na iko wapi na inapakana na Nchi zipi?

2. HATA Vitabu na Makala mbalimbali zinasema NCHI iliyopata Uhuru Mwaka 1961 ilikuwa inaitwa TANGANYIKA.

3. MUUNGANO wetu ulikuwa wa NCHI ya TANGANYIKA na ZANZIBAR na kama kulikuwa na Nchi iliyopata Uhuru Mwaka 1961 inaitwa TANZANIA BARA kwanini huo MUUNGANO haukuwa wa Nchi ya TANZANIA BARA na ZANZIBAR?

USHAURI kwa Wahusika
Tuache kupotosha UKWELI kwa VIZAZI vya Sasa na Vijazo

HAKUNA NCHI inaitwa TANZANIA BARA na huo Mwaka 1961 kulikuwa na NCHI ya TANGANYIKA Nchi ambayo ndio ilipata UHURU.
 
Wenye akili timamu wote hatutishwi na huo upotoshaji wa wazi kutoka kwa watawala wa CCM. Tanganyika ndiyo nchi iliyopata uhuru wake tarehe 9/12/1961 kutoka kwa watawala wa Kiingereza.

Na ilipofika tarehe 26/04/1964, iliungana na kanchi kanyonyaji (kakupe) kanakoitwa Zanzibar, na kubadilisha jina la Tanganyika kuwa Tanzania.
 
Wadau Tarehe 9Desemba 1961 Nchi ya TANGANYIKA ilipata UHURU wake kutoka kwa Mkoloni Mwingereza.
Tarehe 9 Desemba 2023 Vyombo vingi vya TANZANIA vitangaza na kuandika Leo ni Miaka 62 YA UHURU wa TANZANIA BARA.
Najiuliza je ni sahihi?
Je Nchi ya TANZANIA BARA ipo wapi je mwaka 1961 ilikuwepo mpaka ikapewa Huo UHURU?
Kwanini VIONGOZI wetu wanasema ni Nchi ya TANZANIA BARA?Je wanasema kweli au Wanapotosha?
 
Ni upotoshaji mkubwa kwa sababu hakuna wala haikuwahi kuwepo nchi yoyote katika dunia hii iliyowahi kuitwa Tanzania Bara.
 
Wadau Tarehe 9Desemba 1961 Nchi ya TANGANYIKA ilipata UHURU wake kutoka kwa Mkoloni Mwingereza.
Tarehe 9 Desemba 2023 Vyombo vingi vya TANZANIA vitangaza na kuandika Leo ni Miaka 62 YA UHURU wa TANZANIA BARA.
Najiuliza je ni sahihi?
Je Nchi ya TANZANIA BARA ipo wapi je mwaka 1961 ilikuwepo mpaka ikapewa Huo UHURU?
Kwanini VIONGOZI wetu wanasema ni Nchi ya TANZANIA BARA?Je wanasema kweli au Wanapotosha?

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
Tumelewa mvinyo wa 'muungano' na kisha tunajichanganya. Niliwahi kuona kitabu cha shule ya msingi, kimeandikwa kuwa "TANZANIA ILIPATA UHURU MWAKA 1961" Hili ni kosa kubwa, na tunapotosha kizazi kijacho. Tusione aibu kuitaja Tanganyika, kwani ni pande la ardhi ambalo bado lipo.. Mbona tuna 'Tanganyika Law Society', kwani hii inawakilisha wapi?
 
Tumelewa mvinyo wa 'muungano' na kisha tunajichanganya. Niliwahi kuona kitabu cha shule ya msingi, kimeandikwa kuwa "TANZANIA ILIPATA UHURU MWAKA 1961" Hili ni kosa kubwa, na tunapotosha kizazi kijacho. Tusione aibu kuitaja Tanganyika, kwani ni pande la ardhi ambalo bado lipo.. Mbona tuna 'Tanganyika Law Society', kwani hii inawakilisha wapi?
Nchi imejaa wahuni hii

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
 
Kuna mambo yanashangaza sana.

Ni halali mtu wa Unguja na Pemba kujitambulisha kwamba ni Mzanzibari ila ni haramu kwa mtu wa Tanganyika kujitambulisha kuwa ni Mtanganyika.

Ukithubutu kujitambulisha wewe unatoka Tanganyika inakuwa nongwa unaweza kuingia matatizoni seriously huu ni upumbavu wa kiwango cha juu.

Mbona Wanzanzibari wanajitambulisha kama Wanzanzibari na kuonekana ni sawa tu?

Kwahiyo Tanganyika yetu inafichwa kwa sababu gani? Kwa manufaa ya nani wakati ndo nchi kubwa zaidi katika huu Muungano?
 
Mpaka sasa sijafahamu ni kwa nini baadhi ya makada wa ccm wanatuletea huu upotoshaji.

Tarehe 09/12 kila mwaka tunaadhimisha Uhuru wa Tanganyika wa mwaka 1961.

Halafu tarehe 12/01 kila mwaka Wazanzibari wanaadhimisha siku ya Mapinduzi yao ya mwaka 1965.

Na tarehe 26/04 kila mwaka ndiyo kuna maadhimisho ya huu Muungano wetu wa kidwanzi (Muungano wa changu changu, chako changu), kati ya Tanganyika na Zanzibar wa mwaka 1964! Na huu ndiyo uliokuja kuzaa hili jina la Tanzania.

Kwa hiyo kama wansiasa wanataka kuifuta Tanganyika, basi waifute poa na Zanzibar. Yaani kuwepo Tanzania Bara na Tanzania Visiwani! Na siyo hizi porojo za kuifuta Tanganyika kwa kuiita Tanzania Bara, huku Zanzibar ikibakia na utambulisho wake wa awali. Huu upuuzi ndiyo unaosababisha hata Muungano wenyewe uonekane ni wa kidwanzi.

Naunga mkono hoja.

Ni ujinga kuendelea kuiita Zanzibar jina lake la awali alafu Tanganyika jina lake linakufa tukilazimishwa kuiita Tanzania Bara.

Kuweka uhalisia wa Muungano ni vema iwepo Tanzania Bara na Tanzania Visiwani vinginevyo ni ufala kuitambua Zanzibar
 
Back
Top Bottom