Je, kwa Wakristo yawezekana kumbatiza mtoto ambaye amezaliwa pasipo wazazi kufunga ndoa?

Tatizo mmekaririshwa na wachungaji kuwa ubatizo ni LAZIMA kumwagiwa maji. Yesu alibatizwa akiwa na umri wa miaka kadiri ya 30, kwa hiyo na ninyi mnasubiri ifike miaka hiyo ndio mbatizwe? Kwa nini mnabatizwa mkiwa na umri wa miaka 20, au 23, au 25 au 27?
Yohana Mbatizaji alisema,
7Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye nguvu zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake. 8Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.” Marko 1:7-8
Sisi Roman Catholics tunatoa Sakramenti ya Ubatizo (kuondoa dhambi ya asili) kwa umri wa watoto wachanga, na watakapokua wanakuja kurudia kiapo cha ubatizo kupitia Sakramenti ya Kipaimara (mapaji ya Roho Mtakatifu), kukamilisha alichosema Yohana Mbatizaji kuwa "lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu"
Wabatizeni Watoto wadogo

Tatizo mmekaririshwa na wachungaji kuwa ubatizo ni LAZIMA kumwagiwa maji. (Ubatizo lazima uwe wa kuzamishwa majini wala sio kumwagiwa maji. refer the word baptizmo la kilatini) Yesu alibatizwa akiwa na umri wa miaka kadiri ya 30, kwa hiyo na ninyi mnasubiri ifike miaka hiyo ndio mbatizwe? Kwa nini mnabatizwa mkiwa na umri wa miaka 20, au 23, au 25 au 27? (hili ni fundisho la kibiblia kubatizwa wakati watu wameshaelewa na kuamini sio kufata mafundisho ya kipagani. ref Marko 16:15-16: 15. Akawaambia, “Nendeni ulimwenguni kote, mkawahubirie watu wote Habari Njema. 16. Ye yote atakayeamini na kubatizwa ataokolewa),
Yohana Mbatizaji alisema,
“7Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye nguvu zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake. 8Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.” Marko 1:7-8 (hapa umequote tu biblia lakini hatuoni hoja. hakuna panaposema ukawabatize watoto. hilo fungu linawahusu watu wanaotubu, kuamini na kubatizwa na hao ni watu wazima na sio watoto)
Sisi Roman Catholics tunatoa Sakramenti ya Ubatizo (kuondoa dhambi ya asili) kwa umri wa watoto wachanga, na watakapokua wanakuja kurudia kiapo cha ubatizo kupitia Sakramenti ya Kipaimara (mapaji ya Roho Mtakatifu), kukamilisha alichosema Yohana Mbatizaji kuwa "lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu" (hakuna kitu kinachoitwa dhambi ya asili ndugu. hayo ni mapokeo ya kipagani na hayapo kibiblia. biblia ndio neno la Mungu linalofundisha mapenzi ya mungu sio kitabu kingine)
Wabatizeni Watoto wadogo (Msifanye ushetani huu mtapotea. watoto wako salama hata watakapo tambua baya na jema)
 
Tatizo tu umeshindwa kujua kipi ni sahihi na kipi ni haramu. Ungeanza kwanza kufikiri nje ya ndoa kwa dini si sahihi basi. Hakuna mtu haramu kwenye vitabu hivi. Uharamu unaletwa na matendo na mienendo ya mtu.

Mtu hawi haramu bali ayafanyayo. Ukizini jua uzinzi ni haramu
Kwa hiyo anaruhusiwa kurithi na kutumia ubin wa baba? Kama sio kwa nini?
 
(Ubatizo lazima uwe wa kuzamishwa majini wala sio kumwagiwa maji. refer the word baptizmo la kilatini)
Kwa nini una refer kutoka katika dictionary ya Kilatini, na si katika biblia ambayo imesema lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.” Marko 1:7-8
 
watoto wadogo hawabatizwi, soma biblia yote mwanzo mwisho utaona!!!!! unafikiri Mariam alikua mjinga asimbatize Yesu akiwa mtoto???

Mkuu nakuongezea maarifa. Ninayo katekismu yenyewe nimekupigia picha uone kama kiingereza kina shida nitakutafutia kwa kiswahili. Ona picha za kama ushahidi uliodai.
View attachment 591453 View attachment 591454
hii sio biblia mkuu....Jibu swali moja tu direct....unafikiri kwa nini Yesu alibatizwa akiwa mtu mzima?
 
Kwa nini una refer kutoka katika dictionary ya Kilatini, na si katika biblia ambayo imesema lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.” Marko 1:7-8

kwani wewe ukitaka kufahamu maana ya neno fulani kwenye biblia usilolijua unafanyaje? watu wa kawaida wanatafuta kwenye vyanzo vinavyoelezea maana ya neno kwa sababu biblia inataja tu ubatizo. history na vitabu vingine vya kutafsiri vinakubaliana kuwa ubatizo ni kuzamisha. ubatizo unatokana na neno la kilatini au kiyunani linalomaanisha kuzamisha majini ambao uliutumia Yohana mbatizaji. sasa kubatiza kwa Roho Mtakatifu sio kumwagia mtoto maji. hizo zilikuwa taratibu za kibabeli za kuwaingiza watoto wakiwa wadogo katika ibada za kitamaduni za kibabeli kabla urumi haujaanza kutawala. Roho mtakatifu anabatiza kwa mtu kuamini, kutubu na kuzamishwa majini ikionyesha kukana mahusiano yake mapotovu na kupokea imani ya Kristo
 
yaani hapa uko sahihi tu kuwa ukatoliki ni sawa na ibada za mizimu ambazo kila kabila zipo na ni wazi kuwa ni za kishetani. wakristo huongozwa na biblia
Biblia ipi? Iliyokuwa compiled na wakatoliki? Kuudharau ukatoliki huku ukikubali biblia ni sawa na kupenda chakula ila unadai vyombo vyote vilivyotumika kuandaa chakula hicho vinakuchefua.
 
Inawezekana lakini wao wakatoliki wala hawaitumii,
Hapo kwenye red! Maana yake bado hutaki kuamini....umeshupaza shingo...utavunjika...kamata ukweli huo....

Unamaanisha nini unaposema hawatumii...?? Kutumia kivipi..? Kukariri ndio unaita matumizi...? Nifafanulie hapo

wala hawana time na huyo christo mwenyewe,
Hizi shutuma ni kubwa sana....Yesu Kristo ndio kichwa cha Kanisa....Sasa sijui ulikuwa unamaanisha nini hapa..??

wao wanadili na mama maria
Upunguze kusema uongo.....Bikira Maria ni Mama wa huyo Kristo...Maria anapewa heshima ya juu kabisa....ni wa kwanza kati ya Watakatifu wote..

, ambaye mpaka leo wanamuita bikira ( serious!!!).
Ni kweli...Maria ni Bikira hata leo...ni bikira wa Daima....

eti yeye ndo awaombee kwa mungu
Bikira maria kama Walivyo Wayakatifu wengine kazi yao ni kutuombea.....Rejea
Ufunuo wa Yohana 5:8
Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele za Mwana-Kondoo, kila mmoja wao ana kinubi, na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni maombi ya watakatifu.
watoto kitu ambacho kwenye bibilia hakuna kabisa
Kama hakuna nioneshe ni wapi kwenye Biblia pamesema tubatize watu wazima....???
, kusujudia sanamu nayo kwenye bibilia hakuna kabi
Tumalizane kabisa kwenye Ubatizo kwanza, mambo ya Sanamu nitakujibu....Tuwekane Sawa hapa kwenye ubatizo kwanza....utahamisha mada kama si kuvuruga
 
kwani wewe ukitaka kufahamu maana ya neno fulani kwenye biblia usilolijua unafanyaje? watu wa kawaida wanatafuta kwenye vyanzo vinavyoelezea maana ya neno kwa sababu biblia inataja tu ubatizo. history na vitabu vingine vya kutafsiri vinakubaliana kuwa ubatizo ni kuzamisha. ubatizo unatokana na neno la kilatini au kiyunani linalomaanisha kuzamisha majini ambao uliutumia Yohana mbatizaji. sasa kubatiza kwa Roho Mtakatifu sio kumwagia mtoto maji. hizo zilikuwa taratibu za kibabeli za kuwaingiza watoto wakiwa wadogo katika ibada za kitamaduni za kibabeli kabla urumi haujaanza kutawala. Roho mtakatifu anabatiza kwa mtu kuamini, kutubu na kuzamishwa majini ikionyesha kukana mahusiano yake mapotovu na kupokea imani ya Kristo
Nimekusoma vizuri ila nimetambua vyanzo vyako vya elimu ya dini ni finyu. Umetaja Roho Mtakatifu ila unasahau Roho Mtakatifu alitumwa kufundisha na kufunua yote ambayo Kristu hakueleweka. Hata huyo Roho Mtakatifu alipobatiza hakuzamisha kwenye maji. Unafikiri hakubatiza? Hata hivyo Kristu alisharuhusu kanisa kuruhusu chochote chenye lengo la kuwafanya wote wawe wanafunzi wake. Alikabidhi funguo kwa Petro, kwa hiyo kila lililojema lililoruhusiwa na mitume na waandamizi wao kama halizuii watu kumjua Mungu basi ujue Mwenyezi hana objection nalo.
 
HATA KIPINDI CHA YESU SIJAONA/SIKIQ SEHEMU WATOTO WANABATIZWA
NIMESOMA TU AKISEMA " WAACHENI WATOTO WADOGO WAJE KWANGU MAANA UFALME WA MBINGU NI KWA AJILI YA WATU KAMA WAO"
Sababu watoto ni PURE...haijalishi wamebatizwa au LA!
Kubatizwa watoto kulianzia Roma
Ubatizo kama ubatizo una maana gani...?
Tifautisha mazingira ya wakati ule wa Yesu na Sasa....

Tungekuwa tunafuata hivyo hakika ingetupasa kwenda Mto Jordan kwenda kubatizwa...maana Yesu si alibatizwa Jordan...? Si tunafuata Yesu aliyoyafanya.....Ndiposa tunarudi kwenya dhima na mantiki ya Ubatizo...." Kwanini Ubatizo"

Ubatizo sio Show ya twangapepeta
 
Watoto hubarikiwa na si kubatizwa,wakubatizwa ni yule anaye tambua tendo zima la ubatizo lina maana gani hasa katika maisha yake.
Kubariki ni nini..? Unabariki ili iweje..? Ubatizo ni nini...? Kwanini ubatizo..?

Ubatizo ni hatua muhimu ya kuingizwa ktk ushirika wa Watakatifu.....hatua hiyo haina ubaguzi...kila aliye na pumzi anahitaji...


Vipi mtoto sio kiumbe chenye pumzi...??
 
... ubatizo unatokana na neno la kilatini au kiyunani linalomaanisha kuzamisha majini ambao uliutumia Yohana mbatizaji. sasa kubatiza kwa Roho Mtakatifu sio kumwagia mtoto maji. hizo zilikuwa taratibu za kibabeli za kuwaingiza watoto wakiwa wadogo katika ibada za kitamaduni za kibabeli kabla urumi haujaanza kutawala. Roho mtakatifu anabatiza kwa mtu kuamini, kutubu na kuzamishwa majini ikionyesha kukana mahusiano yake mapotovu na kupokea imani ya Kristo
Kwa hiyo nyie mnaamini katika ubatizo wa Yohana wa maji mengi au wa Yesu Kristu wa Maji na Roho?
NB: Wakati ukijibu hili, zingatia kwamba ulianza ubatizo wa Yohana mbatizaji, halafu Yohana huyo akasema unakuja ubatizo wa Roho. Yesu akaja kusema mbatizwe kwa Maji na Roho. Sisis Wakatoliki tunabatiza katika maji (ubatizo watoto wadogo) na roho (kipaimara watoto waliokua)
Yohana 3:5
Yesu akamwambia, “Ninakuambia hakika, kama mtu hakuzaliwa kwa maji na kwa Roho hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu.
 
Mtoto ni nyani sio..? Mungu anangalia umri sio

Mtoto mdogo hana uwezo wa kumwamini Yesu au kutokumwamini , pia hana uwezo wa kutubu dhambi zake kisha abatizwe..... umri unakua kigezo kikubwa kwasababu mtu mzima anaweza akafanya haya maamuzi pasipo kulazimishwa..
 
Inawezekana lakini wao wakatoliki wala hawaitumii, wala hawana time na huyo christo mwenyewe, wao wanadili na mama maria, ambaye mpaka leo wanamuita bikira ( serious!!!). eti yeye ndo awaombee kwa mungu ( nimeweka all in lowercase kwa kumaanisha kabisa). wanabatiza watoto kitu ambacho kwenye bibilia hakuna kabisa, kusujudia sanamu nayo kwenye bibilia hakuna kabisa
Mkuu, kwa watu ambao mmezaliwa kwa wazazi wa Kiprotestanti au Kisabato, kwa vyovyote vile mtakuwa mmekaririshwa kuwa Wakatoliki wao hawaijali Biblia, wao ni Bikira Maria tu, wao wanaabudu sanamu nk. Lazima wawaambie hivyo ili kufanya justification ya kujitenga kwao (to protest against). Hata katika tafiti, lazima utafute udhaifu (research gap) ili uonyeshe umuhimu wa research yako. Kwa hiyo, wazazi hao wangewapa nafasi muidadisi Catholic church kwa akili zenu binafsi bila kushikiwa, hakika usingeandika hayo hapo juu. Kwa kuwa hoja yako ni kwamba wakatoliki hawatumii Biblia, sioni haja ya kuendelea na wewe maana hadi nikubadilishe mtazamo, pengine server itajaa. Wazazi wenu na wachungaji wenu wanataka kuhalalisha Protests zilizofanyika, that's why waingereza walisema "give a dog a bad name and hang him"
 
Mtoto mdogo


Mtoto mdogo hana uwezo wa kumwamini Yesu au kutokumwamini , pia hana uwezo wa kutubu dhambi zake kisha abatizwe..... umri unakua kigezo kikubwa kwa sababu mtu mzima anaweza akafanya haya maamuzi pasipo kulazimishwa.. .
Kuanzia miaka mingapi, mbona hamsemi? Maana Yesu alibatizwa na miaka 30. Semeni wazi kuwa mnasubiri miaka 30 au la
 
Kwa hiyo anaruhusiwa kurithi na kutumia ubin wa baba? Kama sio kwa nini?
Kwani mtu akikatazwa kufanya jambo fulani ndio yeye anakuwa haramu?

Mfano huruhusiwi kuingia na viatu msikitini, au msababato huruhusiwi kula nguruwe, hapo mtu aliyekatazwa sio haramu bali haramu ni lile katazo (kilichosababisha katazo)

Kama kweli muelewa nadhani umenielewa. Mtu hawi haramu (soma vitabu vya dini ujuavyo hukuti mtu haramu) bali matendo au maneno au mawazo. Mtu hawi haramu ila anaweza kufanya mambo yaliyoharamishwa.

Uislam hautambui mkristo kama mrithi hata kama alifunga ndoa ya kikristo, je unadhani hapo mtu ni haramu? Wakati huo kumbuka ikiwa watu wamefunga ndoa kanisani baadae wakawa waislamu hawatakiwi tena kufunga ndoa (ya kiislamu) kwa mujibu wa Uislamu.
 
Kwani mtu akikatazwa kufanya jambo fulani ndio yeye anakuwa haramu?

Mfano huruhusiwi kuingia na viatu msikitini, au msababato huruhusiwi kula nguruwe, hapo mtu aliyekatazwa sio haramu bali haramu ni lile katazo (kilichosababisha katazo)

Kama kweli muelewa nadhani umenielewa. Mtu hawi haramu (soma vitabu vya dini ujuavyo hukuti mtu haramu) bali matendo au maneno au mawazo. Mtu hawi haramu ila anaweza kufanya mambo yaliyoharamishwa.

Uislam hautambui mkristo kama mrithi hata kama alifunga ndoa ya kikristo, je unadhani hapo mtu ni haramu? Wakati huo kumbuka ikiwa watu wamefunga ndoa kanisani baadae wakawa waislamu hawatakiwi tena kufunga ndoa (ya kiislamu) kwa mujibu wa Uislamu.
Kwa nini akatazwe kutumia jina la baba yake wakati waliozaliwa ndani ya ndoa wanaruhusiwa? Mfano wako ungekua sawa kama kuna watu wapo exceptional kufanya kwenye hayo mambo, kama kungekua kuna waislamu wanaruhisiwa kuingia na viatu au kuna wasabato wanaruhusiwa kula nyama na wengine hawaruhusiwi
 
Back
Top Bottom