Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Je kutanguliza maslahi ya chama badala ya taifa ndani ya bunge kunaweza kutafsiriwa kama hujuma dhidi ya umoja wa kitaifa ? Je anayewashawishi wawakilishi wa wananchi ambao wengi wao hawana chama, kutetea maslahi ya chama kuliko ya taifa anatenda kosa la jinai. Je mbunge aliyeapa kuiwajibisha serikali kulinda katiba kwa kuhakikisha utawala wa sheria, haki na usawa, anapoamua kutanguliza na kulinda maslahi ya kikundi katika jamii, anatimiza wajibu ?
Naomba mchango kutoka kwenu bila jazba na papara kuhusu swala hili. Hawa wana tofauti gani na wanaotumia rasilimali za taifa kujinufaisha wao wenyewe na watu wao. Imebidi niseme hili baada ya serikali kukaa kimya bila kukemea kauli iliyotolewa na gwiji wa siasa ndani ya CCM, Kingunge Ngomable Mwiru akitaka wabunge wa CCM kutanguliza maslahi ya chama kuliko taifa. Je yawezekana mahakama na vyombo vya dola pia vinafanya hivyo ?
Kutanguliza maslahi ya chama mbele ya taifa ni kuleta vurugu na kuhatarisha amani, utulivu, umoja wa kitaifa na kuchochea utawala usiojali haki na usawa. Ninaamini haya ni mtendo yanayoweza kutafsiriwa kama ya kuvunja amani na hivyo kuwa kosa mbele ya sheria au mnasemaje ?
Naomba mchango kutoka kwenu bila jazba na papara kuhusu swala hili. Hawa wana tofauti gani na wanaotumia rasilimali za taifa kujinufaisha wao wenyewe na watu wao. Imebidi niseme hili baada ya serikali kukaa kimya bila kukemea kauli iliyotolewa na gwiji wa siasa ndani ya CCM, Kingunge Ngomable Mwiru akitaka wabunge wa CCM kutanguliza maslahi ya chama kuliko taifa. Je yawezekana mahakama na vyombo vya dola pia vinafanya hivyo ?
Kutanguliza maslahi ya chama mbele ya taifa ni kuleta vurugu na kuhatarisha amani, utulivu, umoja wa kitaifa na kuchochea utawala usiojali haki na usawa. Ninaamini haya ni mtendo yanayoweza kutafsiriwa kama ya kuvunja amani na hivyo kuwa kosa mbele ya sheria au mnasemaje ?