Je, Kuna mpango wowote wa kuibadilisha Dar es salaam kuwa New City?

Venus Star

JF-Expert Member
Dec 6, 2018
19,708
59,872
UTANGULIZI
Kwa sasa dunia inabadilika sana, kila nchi inaweka mipango ya kuibadili miji mikokwe na kuwa miji ya kisasa. Kwa upande wa Dar es salaam, mji huu umekuwa ni wa zamani zana lakini miundombinu iliyo mingi bado ni ya kizamani kama mji ulivyo.

Tukianza na mfumo wa maji taka, tangu mji ujengwe hakuna jitihada zozote za kubadilisha miundo mbinu ya maji taka. Ndio maana mvua kidogo tu ikinyesha kunakuwa na mafuriko kila kona.

Upangiliaji wa Nyumba na majengo. Jiji na Dar es salaam ni kati ya miji iliyopangiliwa ovyo ovyo hapa duniani. Ujenzi wa nyumba ni holela hakuna hata plan yoyote. Kwahiyo mji umekuwa na makazi yasiyo na maana. Yakitokea majanga kama moto, kupata barabara ya kukufikisha moto ulipotokea inakuwa ni shida.

MPANGO WA KUJENGA NEW DAR ES SALAAM CITY
Kuweza kubadika bandika mipango ndani ya Dar es salaam, haitasaidia chochote. Maana tayari watu zaidi ya 7m wanaishi ndani ya Dar es salaam. Lazima kuwepo na juhudi za maana kuanzisha CIty Mpya ili kuwahamisha watu wote walipo Posta na Kariakoo kwenda kwenye mji huo mpya.


1694078045595.png

Tunaweza kabisa tukaanzisha Dar es salaam New city kule Kiembeni Forest iliyopo Bagamoyo.


1694078246300.png

GHARAMA ZA KUJENGA MJI MPYA WA DAR ES SALAAM
NImefanya utafiti kwa kuangalia miji mbalimbali mipya inayojengwa duniani na gharama zake.

1. King Abdullah Economic City
Huu mji upo Saudia Arabia. Mji huu mpya upo na ukubwa wa 173 km² yaani ni zaidi ya ukubwa wa Dar es salaam.

Gharama za kujenga mji huo mpya inakadiliwa kuwa $55 billion. Na unategemewa kuwa na wakazi 1.8 million.
Tayari First Stage ilikamilika mwaka 2010.


1694078745288.png

2. Dholera city - India
Huu nao ni mji unaojenga India na upo katika hatua za mwisho kabisa. Gharama zake ni $30 billion.


1694079192233.png

KWANINI TUJENGE MJI WA DAR ES SALAAM MPYA
Kwa sasa mji wa Dar es salaam ni vigumu sana kurekebisha maana uharibifu uliofanyika ni mkubwa sana. Cha msingi ni kuwahamisha watu na kubomoa majengo kisha kuujenga upya. Lakini hiyo hatua ya kubomoa majengo lazima tujenge Mji mwingine mzuri wa kuwavutia watu waende huko.

Ile posta inatakiwa kuvunjwa vunjwa na kujenga upya.

Kuweka budget ya $55 billion kwa mpango wa mika 20 siyo mbaya.

Je, inawezekana kwetu?
 
Kwa serikali ipi kwanza ya kuwaza mipango ya miaka 20-30 mbele 🤔🤔 hii hii ya kutuambia tuhamie Burundi🤔🤔 hii hii ya wizi ulio tukuka na hakuna yeyote anaeshikwa hata kishikizo cha shati🤔🤔 Kila mmoja anaeingia pale anawaza yeye na familia yake, hayo mengine japo mazuri kabisa lakini yatabaki kua kama ndoto ya jinamizi linalo tisha 🚶🚶🚶
 
UTANGULIZI
Kwa sasa dunia inabadilika sana, kila nchi inaweka mipango ya kuibadili miji mikokwe na kuwa miji ya kisasa. Kwa upande wa Dar es salaam, mji huu umekuwa ni wa zamani zana lakini miundombinu iliyo mingi bado ni ya kizamani kama mji ulivyo.

Tukianza na mfumo wa maji taka, tangu mji ujengwe hakuna jitihada zozote za kubadilisha miundo mbinu ya maji taka. Ndio maana mvua kidogo tu ikinyesha kunakuwa na mafuriko kila kona.

Upangiliaji wa Nyumba na majengo. Jiji na Dar es salaam ni kati ya miji iliyopangiliwa ovyo ovyo hapa duniani. Ujenzi wa nyumba ni holela hakuna hata plan yoyote. Kwahiyo mji umekuwa na makazi yasiyo na maana. Yakitokea majanga kama moto, kupata barabara ya kukufikisha moto ulipotokea inakuwa ni shida.

MPANGO WA KUJENGA NEW DAR ES SALAAM CITY
Kuweza kubadika bandika mipango ndani ya Dar es salaam, haitasaidia chochote. Maana tayari watu zaidi ya 7m wanaishi ndani ya Dar es salaam. Lazima kuwepo na juhudi za maana kuanzisha CIty Mpya ili kuwahamisha watu wote walipo Posta na Kariakoo kwenda kwenye mji huo mpya.

View attachment 2741865

Tunaweza kabisa tukaanzisha Dar es salaam New city kule Kiembeni Forest iliyopo Bagamoyo.

View attachment 2741869

GHARAMA ZA KUJENGA MJI MPYA WA DAR ES SALAAM
NImefanya utafiti kwa kuangalia miji mbalimbali mipya inayojengwa duniani na gharama zake.
1. King Abdullah Economic City
Huu mji upo Saudia Arabia. Mji huu mpya upo na ukubwa wa 173 km² yaani ni zaidi ya ukubwa wa Dar es salaam.
Gharama za kujenga mji huo mpya inakadiliwa kuwa $55 billion. Na unategemewa kuwa na wakazi 1.8 million.
Tayari First Stage ilikamilika mwaka 2010.

View attachment 2741885

2. Dholera city - India
Huu nao ni mji unaojenga India na upo katika hatua za mwisho kabisa. Gharama zake ni $30 billion.

View attachment 2741889

KWANINI TUJENGE MJI WA DAR ES SALAAM MPYA
Kwa sasa mji wa Dar es salaam ni vigumu sana kurekebisha maana uharibifu uliofanyika ni mkubwa sana. Cha msingi ni kuwahamisha watu na kubomoa majengo kisha kuujenga upya. Lakini hiyo hatua ya kubomoa majengo lazima tujenge Mji mwingine mzuri wa kuwavutia watu waende huko.

Ile posta inatakiwa kuvunjwa vunjwa na kujenga upya.

Kuweka budget ya $55 billion kwa mpango wa mika 20 siyo mbaya.

Je, inawezekana kwetu?
Ukijenga mji upya matatizo na umasikini wa wananchi utaisha au ni kwa manufaa ya viongozi wanaojinufaisha kwa kodi za wananchi?
 
Ukijenga mji upya matatizo na umasikini wa wananchi utaisha au ni kwa manufaa ya viongozi wanaojinufaisha kwa kodi za wananchi?
Duh!!! Haya mawazo sasa. Hakuna nchi isiyo na maskini duniani. Mpango wa kujenga mji unaenda sambamba na kupinguza umaskini.

China ipo na miji mingi tu iliyopangiliwa lakini siyo kwamba hakuna maskini china.

Haya mawazo ya kufikiria kitu kimoja tu ndio upuuzi mkubwa sana.

Ndio maana serikali ipo na wizara tofauti tofauti. Asante.
 
Tatizo la nchi yetu porojo ni nyingi sana huku vitendo ni haba!

Hilo jambo uliloshauri mleta mada ni jambo zuri ila sidhani serikali ipo tayari.
Sijui katiba ndio itakuwa mkombozi wetu.
 
UTANGULIZI
Kwa sasa dunia inabadilika sana, kila nchi inaweka mipango ya kuibadili miji mikokwe na kuwa miji ya kisasa. Kwa upande wa Dar es salaam, mji huu umekuwa ni wa zamani zana lakini miundombinu iliyo mingi bado ni ya kizamani kama mji ulivyo.

Tukianza na mfumo wa maji taka, tangu mji ujengwe hakuna jitihada zozote za kubadilisha miundo mbinu ya maji taka. Ndio maana mvua kidogo tu ikinyesha kunakuwa na mafuriko kila kona.

Upangiliaji wa Nyumba na majengo. Jiji na Dar es salaam ni kati ya miji iliyopangiliwa ovyo ovyo hapa duniani. Ujenzi wa nyumba ni holela hakuna hata plan yoyote. Kwahiyo mji umekuwa na makazi yasiyo na maana. Yakitokea majanga kama moto, kupata barabara ya kukufikisha moto ulipotokea inakuwa ni shida.

MPANGO WA KUJENGA NEW DAR ES SALAAM CITY
Kuweza kubadika bandika mipango ndani ya Dar es salaam, haitasaidia chochote. Maana tayari watu zaidi ya 7m wanaishi ndani ya Dar es salaam. Lazima kuwepo na juhudi za maana kuanzisha CIty Mpya ili kuwahamisha watu wote walipo Posta na Kariakoo kwenda kwenye mji huo mpya.



Tunaweza kabisa tukaanzisha Dar es salaam New city kule Kiembeni Forest iliyopo Bagamoyo.



GHARAMA ZA KUJENGA MJI MPYA WA DAR ES SALAAM
NImefanya utafiti kwa kuangalia miji mbalimbali mipya inayojengwa duniani na gharama zake.

1. King Abdullah Economic City
Huu mji upo Saudia Arabia. Mji huu mpya upo na ukubwa wa 173 km² yaani ni zaidi ya ukubwa wa Dar es salaam.

Gharama za kujenga mji huo mpya inakadiliwa kuwa $55 billion. Na unategemewa kuwa na wakazi 1.8 million.
Tayari First Stage ilikamilika mwaka 2010.



2. Dholera city - India
Huu nao ni mji unaojenga India na upo katika hatua za mwisho kabisa. Gharama zake ni $30 billion.



KWANINI TUJENGE MJI WA DAR ES SALAAM MPYA
Kwa sasa mji wa Dar es salaam ni vigumu sana kurekebisha maana uharibifu uliofanyika ni mkubwa sana. Cha msingi ni kuwahamisha watu na kubomoa majengo kisha kuujenga upya. Lakini hiyo hatua ya kubomoa majengo lazima tujenge Mji mwingine mzuri wa kuwavutia watu waende huko.

Ile posta inatakiwa kuvunjwa vunjwa na kujenga upya.

Kuweka budget ya $55 billion kwa mpango wa mika 20 siyo mbaya.

Je, inawezekana kwetu?
Dar haina watu mil 7 ni milioni 5.3
 
UTANGULIZI
Kwa sasa dunia inabadilika sana, kila nchi inaweka mipango ya kuibadili miji mikokwe na kuwa miji ya kisasa. Kwa upande wa Dar es salaam, mji huu umekuwa ni wa zamani zana lakini miundombinu iliyo mingi bado ni ya kizamani kama mji ulivyo.

Tukianza na mfumo wa maji taka, tangu mji ujengwe hakuna jitihada zozote za kubadilisha miundo mbinu ya maji taka. Ndio maana mvua kidogo tu ikinyesha kunakuwa na mafuriko kila kona.

Upangiliaji wa Nyumba na majengo. Jiji na Dar es salaam ni kati ya miji iliyopangiliwa ovyo ovyo hapa duniani. Ujenzi wa nyumba ni holela hakuna hata plan yoyote. Kwahiyo mji umekuwa na makazi yasiyo na maana. Yakitokea majanga kama moto, kupata barabara ya kukufikisha moto ulipotokea inakuwa ni shida.

MPANGO WA KUJENGA NEW DAR ES SALAAM CITY
Kuweza kubadika bandika mipango ndani ya Dar es salaam, haitasaidia chochote. Maana tayari watu zaidi ya 7m wanaishi ndani ya Dar es salaam. Lazima kuwepo na juhudi za maana kuanzisha CIty Mpya ili kuwahamisha watu wote walipo Posta na Kariakoo kwenda kwenye mji huo mpya.



Tunaweza kabisa tukaanzisha Dar es salaam New city kule Kiembeni Forest iliyopo Bagamoyo.



GHARAMA ZA KUJENGA MJI MPYA WA DAR ES SALAAM
NImefanya utafiti kwa kuangalia miji mbalimbali mipya inayojengwa duniani na gharama zake.

1. King Abdullah Economic City
Huu mji upo Saudia Arabia. Mji huu mpya upo na ukubwa wa 173 km² yaani ni zaidi ya ukubwa wa Dar es salaam.

Gharama za kujenga mji huo mpya inakadiliwa kuwa $55 billion. Na unategemewa kuwa na wakazi 1.8 million.
Tayari First Stage ilikamilika mwaka 2010.



2. Dholera city - India
Huu nao ni mji unaojenga India na upo katika hatua za mwisho kabisa. Gharama zake ni $30 billion.



KWANINI TUJENGE MJI WA DAR ES SALAAM MPYA
Kwa sasa mji wa Dar es salaam ni vigumu sana kurekebisha maana uharibifu uliofanyika ni mkubwa sana. Cha msingi ni kuwahamisha watu na kubomoa majengo kisha kuujenga upya. Lakini hiyo hatua ya kubomoa majengo lazima tujenge Mji mwingine mzuri wa kuwavutia watu waende huko.

Ile posta inatakiwa kuvunjwa vunjwa na kujenga upya.

Kuweka budget ya $55 billion kwa mpango wa mika 20 siyo mbaya.

Je, inawezekana kwetu?
Kwa uchumi tulionao ni afadhali hizo pesa zitengwe kupima miji yote Tanzania ili kuzuia makazi holela miaka ijayo
 
Kwa uchumi tulionao ni afadhali hizo pesa zitengwe kupima miji yote Tanzania ili kuzuia makazi holela miaka ijayo
Duh!! Baada ya kupima kinafuta kitu gani sasa mzee. Wakati tayari Dar city center pabovu.
 
Elimu ya maendeleo endelevu kwa viongozi wengi wa Tanzania ni tia maji tia maji,D'salam ni miongoni mwa majiji ya hovyo barani Africa yaani Sisi waafrika hata masuala ya mipango miji tumeshindwa sijui tunaweza kufanya nini Cha maana.

Ngoja tuone Magufuli city hapo kwenye kijiji Cha Dodoma.
 
UTANGULIZI
Kwa sasa dunia inabadilika sana, kila nchi inaweka mipango ya kuibadili miji mikokwe na kuwa miji ya kisasa. Kwa upande wa Dar es salaam, mji huu umekuwa ni wa zamani zana lakini miundombinu iliyo mingi bado ni ya kizamani kama mji ulivyo.

Tukianza na mfumo wa maji taka, tangu mji ujengwe hakuna jitihada zozote za kubadilisha miundo mbinu ya maji taka. Ndio maana mvua kidogo tu ikinyesha kunakuwa na mafuriko kila kona.

Upangiliaji wa Nyumba na majengo. Jiji na Dar es salaam ni kati ya miji iliyopangiliwa ovyo ovyo hapa duniani. Ujenzi wa nyumba ni holela hakuna hata plan yoyote. Kwahiyo mji umekuwa na makazi yasiyo na maana. Yakitokea majanga kama moto, kupata barabara ya kukufikisha moto ulipotokea inakuwa ni shida.

MPANGO WA KUJENGA NEW DAR ES SALAAM CITY
Kuweza kubadika bandika mipango ndani ya Dar es salaam, haitasaidia chochote. Maana tayari watu zaidi ya 7m wanaishi ndani ya Dar es salaam. Lazima kuwepo na juhudi za maana kuanzisha CIty Mpya ili kuwahamisha watu wote walipo Posta na Kariakoo kwenda kwenye mji huo mpya.



Tunaweza kabisa tukaanzisha Dar es salaam New city kule Kiembeni Forest iliyopo Bagamoyo.



GHARAMA ZA KUJENGA MJI MPYA WA DAR ES SALAAM
NImefanya utafiti kwa kuangalia miji mbalimbali mipya inayojengwa duniani na gharama zake.

1. King Abdullah Economic City
Huu mji upo Saudia Arabia. Mji huu mpya upo na ukubwa wa 173 km² yaani ni zaidi ya ukubwa wa Dar es salaam.

Gharama za kujenga mji huo mpya inakadiliwa kuwa $55 billion. Na unategemewa kuwa na wakazi 1.8 million.
Tayari First Stage ilikamilika mwaka 2010.



2. Dholera city - India
Huu nao ni mji unaojenga India na upo katika hatua za mwisho kabisa. Gharama zake ni $30 billion.



KWANINI TUJENGE MJI WA DAR ES SALAAM MPYA
Kwa sasa mji wa Dar es salaam ni vigumu sana kurekebisha maana uharibifu uliofanyika ni mkubwa sana. Cha msingi ni kuwahamisha watu na kubomoa majengo kisha kuujenga upya. Lakini hiyo hatua ya kubomoa majengo lazima tujenge Mji mwingine mzuri wa kuwavutia watu waende huko.

Ile posta inatakiwa kuvunjwa vunjwa na kujenga upya.

Kuweka budget ya $55 billion kwa mpango wa mika 20 siyo mbaya.

Je, inawezekana kwetu?
Watu wenye akili kubwa kama hizo wapo?Watu wanaenda World Bank kuomba pesa za kuchimbia mitaro Uswahilini na sasa wanataka kujenga Garden ya kisasa pale Jangwani!
Wameiacha Wilaya za Kigamboni, Bagamoyo na Mkuranga nazo zinajengwa kwa mtindo wa Kiswazi!
Imagine Jiji strategic kama Dar unamuweka mtu kama Chalamila eti awe Boss!
 
Sie tanzania tunakosa visionary leaders ndio maana vitu kama iv hatuoni umuhimu wake

Uwekezaji kama huo unaweza kuleta tija kiuchumi kwa kuongeza ajira maradufu na kuongeza idadi ya watalii

Ndugu yetu kagame amejitahidi sana kwenye hili sie sijui tunakwama wapi?

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Unaelewea kwamba kuna wananchi wengi wa Tanzania hata maji safi ya bomba bado ni shida kwao??
 
Back
Top Bottom