Emmanuel_mtui
Member
- Apr 10, 2012
- 56
- 13
Samahani wana jamvi kama nitakuwa nimeingiza thread hii mahala ambapo siyo mahala pake, ila leo nilikuwa nimepanda daladala kukatokea mabishano yaliyo nishawisha mimi kwashirikisha ninyi tupate maoni.
Kuna mtu alisema kuna binadamu wanakufa kwa kujitakia, au kupenda wao, akitumia mfano m2 unajua kuna magonjwa na unafanya ngono zembe.
Mwingine akaulioza kwani wote walioathirika wanakufa kabla au baada ya kujua wameathirika,? Mwingine akasema mbona wanakufa kwa ajali na tunasema freemason.
Kwamuda huo nikawa nimefika kituo changu cha kushuka nikaacha mjadala unanaendelea, wadau nini maoni yenu mkizingatia kuwa, kama ni ajali wapo waliopata ajali za kutisha na bado wapo hai, wapo waliougua na kuteseka sana bado wapo, na tulio wafahamu wazima au wenye uwezo walmekufa.
Nawakilisha
Kuna mtu alisema kuna binadamu wanakufa kwa kujitakia, au kupenda wao, akitumia mfano m2 unajua kuna magonjwa na unafanya ngono zembe.
Mwingine akaulioza kwani wote walioathirika wanakufa kabla au baada ya kujua wameathirika,? Mwingine akasema mbona wanakufa kwa ajali na tunasema freemason.
Kwamuda huo nikawa nimefika kituo changu cha kushuka nikaacha mjadala unanaendelea, wadau nini maoni yenu mkizingatia kuwa, kama ni ajali wapo waliopata ajali za kutisha na bado wapo hai, wapo waliougua na kuteseka sana bado wapo, na tulio wafahamu wazima au wenye uwezo walmekufa.
Nawakilisha
Wana JF,
Jana nilikutana na mchungaji mmoja nikamuuliza swali kuwa ajali yoyote duniani inatokea kwa mapenzi ya Mungu au ni laana , hakunipa jibu zuri ila ilionekana naye hajui vizuri kwa kuwa alinijibu ni mapenzi ya Mungu, ni kamuuliza kama ni mapenzi ya Mungu iweje watu wapangiwe kifo cha pamoja, iweje mtoto mdogo ambaye ana hata zambi moja afe?
Mbona sasa waliosababisha wanatiwa nguvuni na kufungwa? Hata vifo vya Albino watu wanatafutia utajiri , kweli albino amepangiwa hivyo?
Tukafika mbali kuwa mbona nchi nyingi tajiri duniani kama Norway, Sweden Uswis watu hawafi kiasi hiki hao Mungu hawapendi? kwa kweli mjadala ulivunjika bila kupata majibu.
Nakaribisha maoni , ya kuridhisha na majibu yenye ukweli. Ila tuzingatie kuwa katika biblia Adam alipewa onyo asile tunda la katikati ya bustanini lenye mvuto sana kwani akila atakufa.