Je, Israel ilichangia bila kukusudia kuunda kundi la Hamas?

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,331
33,142
Hamas supporters march through the streets of Nablus in the occupied West Bank on 15 December 2023

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo kuhusu taarifa
  • Author,Na Laith Issam
  • Nafasi,BBC News Arabic
  • 9 Januari 2024
Madai kwamba vuguvugu la Hamas ulikuwa mradi wa Israel yamekuwa yakisambazwa kwenye vyombo vya habari na wasomi - tangu wapiganaji hao wawaue na kuwateka nyara Waisraeli tarehe 7 Oktoba. Kuna ukweli gani nyuma ya madai hayo?
Wanachama wengi wa Hamas wanakataa madai hayo kama wanavyokataa maafisa wa ngazi za juu wa Israel. Lakini madai hayo yaliwahi kusemwa hadharani na Rais wa zamani wa Misri, Hosni Mubarak.
Pia, Seneta wa chama cha Republican katika Bunge la Marekani alipata kutoa madai hayo na vilevile yamejadiliwa na maafisa wa usalama wa ndani wa Israel, Shin Bet.
A masked Hamas gunman on horseback with other masked Hamas fighters on hoseback and a large croud nearby

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Udugu wa Kiislamu​

Mapambano ya muda mrefu ya Hamas yana mizizi yake katikati ya miaka ya 1940 katika maeneo ya Wapalestina, wakati matawi ya kwanza ya Muslim Brotherhood yalipoanzishwa huko Gaza, Jerusalem na miji mingine.
Baada ya vita vya Waarabu na Israel vya mwaka 1967, vijana wa Muslim Brotherhood hawakuridhika na viongozi wao wa kidini na kisiasa.
Nyaraka za Muslim Brotherhood (udugu wa kiislamu) zinaonyesha vuguvugu hilo lililenga zaidi kuwa na harakati za kielimu, kitamaduni, kijamii na kiroho, na sio shughuli za kijeshi.
Sayyid Qutb behind bars, sipping from a cup

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Muslim Brotherhood ilitokana na mwanazuoni wa Kiislamu Sayyid Qutb, aliyeuwawa Egypt1966

Msemaji wa Hamas​

Msemaji wa kwanza wa vuguvugu la Hamas, Ibrahim Ghosheh, anasema katika kitabu chake, The Red Minaret, kulikuwa na maswali mengi miongoni mwa vijana wa chama cha Muslim Brotherhood.
"Kwani haikutoa suluhisho la wazi juu ya mustakabali wa Palestina, na haikutoa wito wa kuanza kwa harakati za wanajihadi wa Kiislamu," anaandika.
Hilo liliwafanya vijana wa Brotherhood - ambao walitaka kupigana na Israeli - kuunda kile kundi lao ndani ya kikundi. Walipanga kujizatiti bila viongozi wa Brotherhood kujua.
Uniformed armed men running through water

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Mwishoni mwa miaka ya 1960, vijana kutoka Muslim Brotherhood walifanya mashambulizi dhidi ya Israel chini ya mwanvuli wa Fatah

Makubaliano yalifanywa na vuguvugu la Fatah - lililoongozwa kwa miaka mingi na Yasser Araft - kutoa mafunzo kwa wanachama hao wa Brotherhood.
Uamuzi wa kuzindua Hamas ulikuja baada ya Muslim Brotherhood kupitia changamoto kubwa - ikiwa ni pamoja na kuasi kwa wanachama wengi.
Hamas men kneeling in front of a Palestinian flag

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Wafuasi wa Hamas huko Gaza 1992

'Israel iliunda Hamas kukabiliana na PLO'​

Rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak alikuwa miongoni mwa walioibua tuhuma hii. Anasikika katika video akisema mbele ya wanajeshi miongo kadhaa iliyopita, "Israel iliunda Hamas ili kufanya kazi dhidi ya Chama cha Ukombozi wa Palestina (PLO)."
Yasser Arafat standing with armed men

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Kambi ya Fatah huko Jordan, 1970 - Yasser Arafat na wenzake walianzisha vuguvugu la Fatah 1965 kupambanana Israel

Ron Paul, ambaye aligombea urais wa Marekani mwaka 1988, alisema Bungeni mwaka 2009, "ukirejea katika historia, utakuta Israel ilichochea na kusaidia kuunda Hamas, kwa lengo la kukabiliana na Yasser Arafat."
Hassan Asfour, waziri wa zamani na mjumbe wa Palestina katika mazungumzo ya Oslo mwaka 1993, aliiambia televisheni ya BBC mwaka 2023, "Hamas ilizinduliwa kwa makubaliano ya baadhi ya nchi za Kiarabu na Israel - ukiwa ni mradi wa Marekani ili iwe mbadala wa PLO."
David Ben-Gurion, one of Israel's founders, and Israeli Army Chief of Staff Yitzhak Rabin with soldiers in front of the Dome of the Rock, in occupied East Jerusalem

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
David Ben-Gurion, mmoja wa waanzilishi wa taifa la Israel akiwa na Mkuu wa Jeshi la srael, Yitzhak Rabin na wanajeshi baada ya ushindi dhidi ya Waarabu 1967

Je, Israel iliifadhili Hamas?​

Mwaka 1981, gazeti la New York Times lilichapisha mahojiano na gavana wa kijeshi wa wakati huo wa Israel huko Gaza, Yitzhak Segev, ambaye alisema, "watu wenye imani kali ya Kiislamu wanapokea baadhi ya misaada ya Israel. Serikali ya Israel ilinipa bajeti na serikali ya kijeshi inatoa msaada katika misikiti.”
Alisema: "Fedha hizi zinalenga kuimarisha kikosi kinachoshindana na vuguvugu la Ukombozi wa Palestina (PLO)."
Katika mahojiano yaliyochapishwa hivi karibuni na Shirika la Utangazaji la Israel, Yaakov Perry, afisa wa zamani wa Shin Bet, alisema: “Nilikuwa mkuu wa shirika hilo kuanzia 1988 hadi 1995. Nilishuhudia kuibuka kwa vuguvugu la Hamas, na ninakumbuka tathmini yetu ilikuwa - hili ni kundi la kijamii tu. Likifanya kazi ya kutoa mahitaji kwa watu. Lakini watu wengi Israel waliishutumu Shin Bet kusaidia shughuli za kisiasa za Hamas kama mbadala wa PLO, lakini hilo si kweli."
Women kneeling and reading books

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Wanawake wakisoma katika kambi ya wakimbizi ya Nuseirat, Gaza 1970

Mwanzilishi wa Hamas, Sheikh Ahmed Yassiin alisema Israel - ilitoa mishahara ili kujaribu kurejesha maisha ya kawaida kwa watu baada ya kuikalia Gaza.
"Nilikuwa nikipokea lira 240 za Kiisraeli kwa mwezi kwa ajili ya kazi yangu ya ualimu na lira 40 kwa ajili ya kazi yangu kama mhubiri msikitini."
Mtafiti katika Taasisi ya Truman ya Chuo Kikuu cha Hebrew huko Jersulam na afisa wa zamani wa ujasusi wa Israel katika miaka ya 1970, Roni Shaked ameiambia BBC, "Israel haikuwahi kuwafadhili Waislam. Ilitoa leseni kwa taasisi kufanya kazi, lakini haikutoa fedha."
Roni Shaked anasema "hilo linaweza kuwa liliwezesha harakati ya Kiislamu ya Muslim Brotherhood (kabla Hamas kuzaliwa) kukua, lakini Israel haikuwa inaunga mkono harakati zao zisizo na vurugu hapo awali"
An Israeli solder in a Gaza street while civilians walk nearby

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Mwanajeshi wa Israel akipiga doria Gaza 1973

Waandishi wa Israel Ehud Yaari na Zeev Schiff wanasema katika kitabu chao cha Intifada cha mwaka 1990, “Israel ilijidanganya kuhusu uwezo wa kuwadhibiti Waislamu wa siasa kali na kuwatumia ili kuudhoofisha ushawishi wa Harakati ya Ukombozi wa Palestina. Israel imejifunza lakini imechelewa mno.”
Wokmen carrying rocks in baskets on their heads

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Khan Yunis kusini mwa Gaza 1969

Kupambana na Israel​

Armed men talk to a masked gunman

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Fatah wakizungumza na mpiganaji wa Hamas aliyefunika uso huko Gaza 1993

Mabadiliko makubwa katika mbinu ya mapambano ya Muslim Brotherhood dhidi ya Israel yalitokea mwaka 1983. Katika mkutano wa Jordan, iliamua "kuruhusu wanachama wake katika Ukingo wa Magharibi na Gaza kuandaa harakati za kijeshi," kwa mujibu wa tawasifu ya msemaji wa kwanza wa Hamas, Ibrahim Ghosheh.
Mwaka mmoja baadaye, Israel iliwakamata wanachama wote wa kijeshi huko Gaza, waliokuwa wakiongozwa na Ahmed Yassin na kupata silaha 80 katika nyumba yake.
in front of the Dome of the Rock, in occupied East Jerusalem.

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Wa mbele-kuanzia kulia: Ramadan Shalah (mwanzilishi mwenza wa Islamic Jihad), Ahmed Jibril (wa PLO), Hassan Nasrallah (Kiongozi wa Hezbollah), Khaled Mashal (kiongozi wa Hamas 1996 - 2017) na Sheikh Ahmed Yassin (mwanzilishi wa Hamas)

Lakini Yassin aliachiliwa miezi michache baadaye mwaka 1985 kama sehemu ya makubaliano makubwa ya kuwaachilia wanajeshi watatu wa Israel waliotekwa.
Ahmed Yassin alianza tena jukumu la kuongoza harakati za kijeshi takribani mwaka mmoja baada ya kuachiliwa kwake.
Ahmed Yassin sittingh next to Israeli guards

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Ahmed Yassin alirudi kuendelea kuongoza wapiganaji wa Kipalestina baada ya mwaka mmoja

Je, Hamas ni zao la Israel yenyewe?​

Israel haikuitengeneza Hamas, bali vuguvugu la Muslim Brotherhood na mzozo wa Palestina na Israel ndio sababu kuu ya kuundwa Hamas.
Huenda kukawa na jambo la kujadili iwapo Israel ililifumbia macho vuguvugu hilo wakati wa kuanzishwa kwake, au pengine Israel ilijaribu kuitumia Hamas kwa maslahi yake wakati inachipua na kupata nguvu miongoni mwa Wapalestina.
Imetafsiriwa na Rashid Abdallah na kuhaririwa na Ambia Hirsi
chanzo.BBC
 
Hamas supporters march through the streets of Nablus in the occupied West Bank on 15 December 2023

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo kuhusu taarifa
  • Author,Na Laith Issam
  • Nafasi,BBC News Arabic
  • 9 Januari 2024
Madai kwamba vuguvugu la Hamas ulikuwa mradi wa Israel yamekuwa yakisambazwa kwenye vyombo vya habari na wasomi - tangu wapiganaji hao wawaue na kuwateka nyara Waisraeli tarehe 7 Oktoba. Kuna ukweli gani nyuma ya madai hayo?
Wanachama wengi wa Hamas wanakataa madai hayo kama wanavyokataa maafisa wa ngazi za juu wa Israel. Lakini madai hayo yaliwahi kusemwa hadharani na Rais wa zamani wa Misri, Hosni Mubarak.
Pia, Seneta wa chama cha Republican katika Bunge la Marekani alipata kutoa madai hayo na vilevile yamejadiliwa na maafisa wa usalama wa ndani wa Israel, Shin Bet.
A masked Hamas gunman on horseback with other masked Hamas fighters on hoseback and a large croud nearby

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Udugu wa Kiislamu​

Mapambano ya muda mrefu ya Hamas yana mizizi yake katikati ya miaka ya 1940 katika maeneo ya Wapalestina, wakati matawi ya kwanza ya Muslim Brotherhood yalipoanzishwa huko Gaza, Jerusalem na miji mingine.
Baada ya vita vya Waarabu na Israel vya mwaka 1967, vijana wa Muslim Brotherhood hawakuridhika na viongozi wao wa kidini na kisiasa.
Nyaraka za Muslim Brotherhood (udugu wa kiislamu) zinaonyesha vuguvugu hilo lililenga zaidi kuwa na harakati za kielimu, kitamaduni, kijamii na kiroho, na sio shughuli za kijeshi.
Sayyid Qutb behind bars, sipping from a cup

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Muslim Brotherhood ilitokana na mwanazuoni wa Kiislamu Sayyid Qutb, aliyeuwawa Egypt1966

Msemaji wa Hamas​

Msemaji wa kwanza wa vuguvugu la Hamas, Ibrahim Ghosheh, anasema katika kitabu chake, The Red Minaret, kulikuwa na maswali mengi miongoni mwa vijana wa chama cha Muslim Brotherhood.
"Kwani haikutoa suluhisho la wazi juu ya mustakabali wa Palestina, na haikutoa wito wa kuanza kwa harakati za wanajihadi wa Kiislamu," anaandika.
Hilo liliwafanya vijana wa Brotherhood - ambao walitaka kupigana na Israeli - kuunda kile kundi lao ndani ya kikundi. Walipanga kujizatiti bila viongozi wa Brotherhood kujua.
Uniformed armed men running through water

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Mwishoni mwa miaka ya 1960, vijana kutoka Muslim Brotherhood walifanya mashambulizi dhidi ya Israel chini ya mwanvuli wa Fatah

Makubaliano yalifanywa na vuguvugu la Fatah - lililoongozwa kwa miaka mingi na Yasser Araft - kutoa mafunzo kwa wanachama hao wa Brotherhood.
Uamuzi wa kuzindua Hamas ulikuja baada ya Muslim Brotherhood kupitia changamoto kubwa - ikiwa ni pamoja na kuasi kwa wanachama wengi.
Hamas men kneeling in front of a Palestinian flag

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Wafuasi wa Hamas huko Gaza 1992

'Israel iliunda Hamas kukabiliana na PLO'​

Rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak alikuwa miongoni mwa walioibua tuhuma hii. Anasikika katika video akisema mbele ya wanajeshi miongo kadhaa iliyopita, "Israel iliunda Hamas ili kufanya kazi dhidi ya Chama cha Ukombozi wa Palestina (PLO)."
Yasser Arafat standing with armed men

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Kambi ya Fatah huko Jordan, 1970 - Yasser Arafat na wenzake walianzisha vuguvugu la Fatah 1965 kupambanana Israel

Ron Paul, ambaye aligombea urais wa Marekani mwaka 1988, alisema Bungeni mwaka 2009, "ukirejea katika historia, utakuta Israel ilichochea na kusaidia kuunda Hamas, kwa lengo la kukabiliana na Yasser Arafat."
Hassan Asfour, waziri wa zamani na mjumbe wa Palestina katika mazungumzo ya Oslo mwaka 1993, aliiambia televisheni ya BBC mwaka 2023, "Hamas ilizinduliwa kwa makubaliano ya baadhi ya nchi za Kiarabu na Israel - ukiwa ni mradi wa Marekani ili iwe mbadala wa PLO."
David Ben-Gurion, one of Israel's founders, and Israeli Army Chief of Staff Yitzhak Rabin with soldiers in front of the Dome of the Rock, in occupied East Jerusalem's founders, and Israeli Army Chief of Staff Yitzhak Rabin with soldiers in front of the Dome of the Rock, in occupied East Jerusalem

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
David Ben-Gurion, mmoja wa waanzilishi wa taifa la Israel akiwa na Mkuu wa Jeshi la srael, Yitzhak Rabin na wanajeshi baada ya ushindi dhidi ya Waarabu 1967

Je, Israel iliifadhili Hamas?​

Mwaka 1981, gazeti la New York Times lilichapisha mahojiano na gavana wa kijeshi wa wakati huo wa Israel huko Gaza, Yitzhak Segev, ambaye alisema, "watu wenye imani kali ya Kiislamu wanapokea baadhi ya misaada ya Israel. Serikali ya Israel ilinipa bajeti na serikali ya kijeshi inatoa msaada katika misikiti.”
Alisema: "Fedha hizi zinalenga kuimarisha kikosi kinachoshindana na vuguvugu la Ukombozi wa Palestina (PLO)."
Katika mahojiano yaliyochapishwa hivi karibuni na Shirika la Utangazaji la Israel, Yaakov Perry, afisa wa zamani wa Shin Bet, alisema: “Nilikuwa mkuu wa shirika hilo kuanzia 1988 hadi 1995. Nilishuhudia kuibuka kwa vuguvugu la Hamas, na ninakumbuka tathmini yetu ilikuwa - hili ni kundi la kijamii tu. Likifanya kazi ya kutoa mahitaji kwa watu. Lakini watu wengi Israel waliishutumu Shin Bet kusaidia shughuli za kisiasa za Hamas kama mbadala wa PLO, lakini hilo si kweli."
Women kneeling and reading books

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Wanawake wakisoma katika kambi ya wakimbizi ya Nuseirat, Gaza 1970

Mwanzilishi wa Hamas, Sheikh Ahmed Yassiin alisema Israel - ilitoa mishahara ili kujaribu kurejesha maisha ya kawaida kwa watu baada ya kuikalia Gaza.
"Nilikuwa nikipokea lira 240 za Kiisraeli kwa mwezi kwa ajili ya kazi yangu ya ualimu na lira 40 kwa ajili ya kazi yangu kama mhubiri msikitini."
Mtafiti katika Taasisi ya Truman ya Chuo Kikuu cha Hebrew huko Jersulam na afisa wa zamani wa ujasusi wa Israel katika miaka ya 1970, Roni Shaked ameiambia BBC, "Israel haikuwahi kuwafadhili Waislam. Ilitoa leseni kwa taasisi kufanya kazi, lakini haikutoa fedha."
Roni Shaked anasema "hilo linaweza kuwa liliwezesha harakati ya Kiislamu ya Muslim Brotherhood (kabla Hamas kuzaliwa) kukua, lakini Israel haikuwa inaunga mkono harakati zao zisizo na vurugu hapo awali"
An Israeli solder in a Gaza street while civilians walk nearby

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Mwanajeshi wa Israel akipiga doria Gaza 1973

Waandishi wa Israel Ehud Yaari na Zeev Schiff wanasema katika kitabu chao cha Intifada cha mwaka 1990, “Israel ilijidanganya kuhusu uwezo wa kuwadhibiti Waislamu wa siasa kali na kuwatumia ili kuudhoofisha ushawishi wa Harakati ya Ukombozi wa Palestina. Israel imejifunza lakini imechelewa mno.”
Wokmen carrying rocks in baskets on their heads

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Khan Yunis kusini mwa Gaza 1969

Kupambana na Israel​

Armed men talk to a masked gunman

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Fatah wakizungumza na mpiganaji wa Hamas aliyefunika uso huko Gaza 1993

Mabadiliko makubwa katika mbinu ya mapambano ya Muslim Brotherhood dhidi ya Israel yalitokea mwaka 1983. Katika mkutano wa Jordan, iliamua "kuruhusu wanachama wake katika Ukingo wa Magharibi na Gaza kuandaa harakati za kijeshi," kwa mujibu wa tawasifu ya msemaji wa kwanza wa Hamas, Ibrahim Ghosheh.
Mwaka mmoja baadaye, Israel iliwakamata wanachama wote wa kijeshi huko Gaza, waliokuwa wakiongozwa na Ahmed Yassin na kupata silaha 80 katika nyumba yake.
in front of the Dome of the Rock, in occupied East Jerusalem.

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Wa mbele-kuanzia kulia: Ramadan Shalah (mwanzilishi mwenza wa Islamic Jihad), Ahmed Jibril (wa PLO), Hassan Nasrallah (Kiongozi wa Hezbollah), Khaled Mashal (kiongozi wa Hamas 1996 - 2017) na Sheikh Ahmed Yassin (mwanzilishi wa Hamas)

Lakini Yassin aliachiliwa miezi michache baadaye mwaka 1985 kama sehemu ya makubaliano makubwa ya kuwaachilia wanajeshi watatu wa Israel waliotekwa.
Ahmed Yassin alianza tena jukumu la kuongoza harakati za kijeshi takribani mwaka mmoja baada ya kuachiliwa kwake.
Ahmed Yassin sittingh next to Israeli guards

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Ahmed Yassin alirudi kuendelea kuongoza wapiganaji wa Kipalestina baada ya mwaka mmoja

Je, Hamas ni zao la Israel yenyewe?​

Israel haikuitengeneza Hamas, bali vuguvugu la Muslim Brotherhood na mzozo wa Palestina na Israel ndio sababu kuu ya kuundwa Hamas.
Huenda kukawa na jambo la kujadili iwapo Israel ililifumbia macho vuguvugu hilo wakati wa kuanzishwa kwake, au pengine Israel ilijaribu kuitumia Hamas kwa maslahi yake wakati inachipua na kupata nguvu miongoni mwa Wapalestina.
Imetafsiriwa na Rashid Abdallah na kuhaririwa na Ambia Hirsi
chanzo.BBC
Wayahudi wa mrengo mkali wa kulia wakiwemo Netanyahu walichangia kwa makusudi kabisa kuundwa na kulipa nguvu kundi la Hamas ili kuharibu kabisa mpango wa muda mrefu wa suluhisho la kuwa na mataifa mawili.
 
Wayahudi wa mrengo mkali wa kulia wakiwemo Netanyahu walichangia kwa makusudi kabisa kuundwa na kulipa nguvu kundi la Hamas ili kuharibu kabisa mpango wa muda mrefu wa suluhisho la kuwa na mataifa mawili.
Ila leo wanataka kulifuta
Hamas endelea kutwanga hizo kunguru za kizayuni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom