ndugu zangu poleni na majukumu ya maisha. Naomba msaada wenu wa kila hali ninatatizo la kuumwa tumbo hii ni mara yangu ya tatu ndani ya miezi 6. Tumbo linaanza taratibu kuuma na ndani ya masaa 2-3 baadaye maumivu yanaongezeka kwenye kitovu huwezi kulala na mwisho wake kutapika sana bila kwenda haja. Sijapata nini kinachosababisha mpaka sasa maana mara ya kwanza nilifikiria chakula nilichokuwa nimekula, mara ya pili sikuapata jibu ila hii ya juzi naona sasa ni ungonjwa ambao unanyemelea kwa kasi sana maana nilienda hospital nikapigwa X-ray,na Ultrasound pamoja na kuchuliwa na damu lakini mwishoni Doctor aliniambia may be ni appendicitis. na alishauri nifanye upasuaji lakini kulinga na mazigira yalivyo hapa sikutaka kufanya operation maana watu wengi waliofanyiwa operation kabla ya kutibu tatizo wanaongeza matatizo ndani ya miili yao. Baada ya kumuomba Doctor kama kunanjia nyingine nje ya operation akashauri waniwekea drip 6 na nikae siku 3 kama sijapata nafuu niende kufanyiwa upasuaji.niliendelea siku zilizofuata nilikuwa nawekewa drip 2 kila siku kwa siku 3 zaidi. Kweli sasa niko okay! lakini swali langu huu ugonjwa unatoakana na nini na kweli ni appendicitis ( kidole tumbo) au ni ugonjwa mwingine?
na kama appendicitis kuna dawa gani za kutumia nje ya operation? au ni operation tu?
Natanguliza shukrani zangu kwa msaada wenu na Mungu awabariki sana.
na kama appendicitis kuna dawa gani za kutumia nje ya operation? au ni operation tu?
Natanguliza shukrani zangu kwa msaada wenu na Mungu awabariki sana.