JB na Skendo mpya ya kuiba mawazo ya Movie ya ''Ladies Vs Ricky Bahl"

"Kwanza kabisa ningeanza kwa salam kwenu nyote na naamini muwazima wa afya.
Nimeamua kuandika ujumbe huu baada ya kuona na kupigiwa simu chache kuhusu "SKENDO" wa filamu Mzee wa Swagga kuwa imekopiwa.
Nijibu jibu fupi bila kusita kuwa kweli Story imekopiwa na original Story inaitwa Ladies Vs Ricky Bahl na mimi ndiye niliyemshauri JB kuichukua Story hiyo yenye maudhui ya kuvutia. Nataka nieleze sababu ya kufanya hivyo ila kabla sijaeleza sababu ningependa kuwaambia wale wote wanaotumia skendo hii kuyarefusha mambo haya kuwa kwenye ulimwengu wa filamu ni jambo la kawaida duniani watu kuchukua maudhui ya story na kuyatengeneza katika mazingira yao endapo maudhui hayo yataelimisha au kukosoa au kufurahisha kuhusu jambo..watakaoendelea kulalamika baada ya ujumbe huu ni dhahiri wanania zao nyingine na si kujenga.
Kwanza kabisa mimi ndiye mwandishi mkuu wa filamu za JB kuanzia enzi za DJ Ben, Dereva Taxi, Nakwenda kwa Mwanangu, Shikamoo Mzee, Bado Natafuta mpaka hii Mzee wa Swagga na hizo nyingine zote zikiwa ni original scripts kutoka kwenye ubongo wangu.
Filamu anazofanya JB ni Romantic Comedies na Inspirational Comedies kwa hiyo yeye huwa anapenda maudhui ya kuentertain zaidi yani filamu zenye kuchangamsha na kuburudisha tofauti na waigizaji wengine kama Single Mtambalike anayependelea filamu za ugentleman zaidi (haya ni kutokana na kukaa nao na kuzungumza nao na kuwafahamu kwa kina).
Sasa kuhusu Mzee wa Swagga:
JB alitengeneza filamu mfululizo zenye maudhui tofauti na alizozoeleka, kama Hukumu ya Ndoa, Mikono Salama ambazo sikuziandika mimi na nakiri kuwa hazikufanya vizuri sana sokoni.
Sababu ya filamu hizi kuandikwa na watu wengine ni sababu nilikuwa nashughulika na Script ya filamu yangu mwenyewe niliyoproduce mwaka jana October inayoitwa SAFARI YA GWALU (bado haijatoka mpaka mwezi wa 3 mwishoni), aliyoigiza Gabo kama kijana anayerudi shule ya msingi baada ya kupigika na maisha.
Filamu hii imenichukua mwaka mzima kuanzia kuiandika mpaka kuja kuproduce, kuandika ilianza January-march 2014 hivyo sikupata nafasi kumuandikia JB tangu tulipotoa BADO NATAFUTA na CHARLE MVUVI (bado haijatoka).
Baada ya filamu hizi mbili (Hukumu ya Ndoa na Mikono Salama);JB alinieleza angetamani nimuandalie Filamu na Mzee Majuto wakati huo wakiwa safarini kwenda Uturuki ili wakashoot Uturuki iwe filamu kali. Wakati nikiandaa filamu hiyo mshtuko mkubwa ukaja kwa misiba ya mfululizo ya wana Tasnia wenzetu iliyopelekea Safari ya JB na Mzee Majuto ya Uturuki kufa na hivyo kufanya hata script niliyoandaa kukosa msisimko tena.
Baada ya matatizo JB alitaka filamu inayofanana na Senior Bachelor, DJ Ben na Nakwenda kwa Mwanangu, akiigiza kama mburudishaji zaidi na kwa kuwa sikuwa na Idea mpya kwenye kichwa na muda ulikuwa unaenda sana na anahitajika kupeleka filamu yake kwa msambazaji ikabidi nitafute story itakayofanana na JB mburudishaji tunayemfahamu muda mrefu;
kwa ninavyomuelewa vizuri JB labda kuliko waandishi wengi wanavyomuelewa hiyo haikuwa ngumu kutafuta wazo la kumfaa na ndipo tukaipata Ladies Vs Rick Bahl, JB aliipenda ila sote tulikuwa na wasiwasi kwani JB ni muoga sana wa kuandikwa vibaya, nikamwambia jambo ambalo nataka niwaeleze nanyi leo. Jambo ambalo lilimfanya JB kukubali niandike script mpya kupitia kisa kile na kuiproduce...
Ukweli ni kuwa duniani kote (masoko ya filamu yote namaanisha) watu wanapoona maudhui ya story ya nchi au taifa jingine kuwavutia wanaweza kuchukua maudhui hayo na kuyatumia kutengeneza filamu za maudhui yale kwenye mazingira yao. Kuna Filamu nyingi hapa Tanzania na Nigeria na Bollywood Hata Hollywood zimefanyika hivyo na si dhambi.
Kama Tanzania tazama filamu Ya BEST MAN ya Hemedi na Yussuf Mlela, ni copy ya BEST MAN ya Morris Chestnut na Taye Diggs...
Nollywood filamu Ya GUARDIAN ANGEL ya Ramsey Noah ni copy ya Filamu HATYA ya Bollywood ya Govindah...
Pia filamu za ROMEO AND JULIET developed kutoka kwa William Shakespears plays zimekopiwa Bollywood kwenye filamu iliyoleta Mabadiliko makubwa Bollywood ya QAYAMAT SE QAYAMAT TAK kama nasema uongo mtu aziangalie na kuja kunikosoa na nitaleta dazeni ya filamu zilizokopiwa kutoka nchi na nchi.
Ila nataka kuuliza swali, mbona nyingine zilizokopiwa hapa Tanzania toka nje hazikuzungumziwa kama Mzee wa Swagga?
Nadhani jibu ni moja tu: sababu JB ameitendea haki filamu hiyo. Ila tusiende huko !
Jambo jingine (nadhani ndio la msingi zaidi), mnapokaa kulaumu mjue kazi ya kuwapa watazamaji kitu wanachotaka kila siku na kuwafanya wakupende si suala dogo, tunaumiza vichwa mchana na usiku.
JB si kwamba namfagilia sababu namuandikia ila huwa anaumia sana kutafuta story mpya na ukweli hata mimi nateseka sana kutengeneza vitu vipya na ukitazama mtu huyu mmoja atengeneze filamu 6 au 7 kwa mwaka na zote mzipende na kufurahia inahitaji kujitoa kwa hali ya juu.
Nikiwa kama mwandishi kihalali nahitaji kuandika script 2 tu kwa mwaka ili nitoe vitu vikali, unapoelemewa na mzigo ni rahisi kuharibu kazi na kwa kuwa tunajitahidi (mimi na JB) kuwapa mnachopenda basi huwa tunatafuta kila njia kutowakwaza mashabiki, naomba mtuhurumie nasi kwani mazingira ya kazi ni magumu mno.
Kwa haya niliyoandika ningependa kuwaambia tusiwe watu wa kulaumu na kuhukumu, mimi kuproduce filamu yangu mwaka jana kumepunguza kujitoa kwangu kuandaa filamu kali za JB, mimi ndiye wa kulaumiwa na si JB.
Na kwa niaba ya mashabiki wa JB nawaomba radhi kama kwa namna moja au nyingine mmejisikia vibaya ila kwa niliyoeleza mtaungana nami kuwa si dhambi kufanya hivyo inapobidi na tushirikiane kupeleka gurudumu hili mbele.
Nikiwa kama mwandishi bora wa script (Kama nilivyotambuliwa na ZIFF, JULY 2014 kupitia Filamu ya "SHIKAMOO MZEE") natambua jukumu langu kama mwandishi simkingii kifua JB bali nasimamia kile ninachokifanya kama Professional.
Naomba tuache kuongea na tushirikiane kuboresha filamu zetu."

Daniel Manege

Unasema sio wewe ulieandika haya? Kwa hiyo ni coincidence tu huyo mwandishi Daniel Manege naye kaandaa filamu ya safari ya Gwalu jina linaloendana na id yako ya jf?
 
Upo sahihi Boss,

Hii stori ilikuwepo hapa kwenye "JB na Scandal mpya ya kuiba mawazo ya Movie ya ''Ladies Vs Ricky Bahl"

Mi nimefanya kuleta upande wa pili wa stori toka kwa muandishi wa husika,
ndio maana hiyo stori imekaa kama nanukuu tu.

Hivyo kwa kuweka kumbukumbu sahihi Mimi si Daniel Manege ila ni mjumbe wa JF kama ilivyo wewe.

Punguza munkari Boss!

Mwambie utetezi wake ni dhaifu kabisa....mwambie kwanini aliandika mtunzi wa story ni JB?
Kwanini haku acknowladge?
Kwanini JB mwenyewe haoneshi kukubali kosa anajifanya kukomaza shingo huku akijua inaweza vunjika?

Muulize kwa hiyo anajaribu kusema kukopi na kupaste ni jambo la kawaida?Muulize ni movie ngapi hadi sasa amekopi na kupaste?

Muulize tusinge baini alipanga kusema ukweli lini?
Mwambie akaandike utetezi mwingine!
 
Hilo ni angalizo zuri,
Ila tujue pia tasnia yetu idara zake nyingi sio makini hivyo kuna makosa mengine muandika script au muigizaji mkuu yanakuwa sio yao moja kwa moja....
Ila ndio hivyo goli mkifungwa linakuwa ni kosa la timu nzima

Ina maana story za kuigiza zimekwisha? Mbona kuna watu waandika script vizuri hawawapi tenda?
 
"Kwanza kabisa ningeanza kwa salam kwenu nyote na naamini muwazima wa afya.
Nimeamua kuandika ujumbe huu baada ya kuona na kupigiwa simu chache kuhusu "SKENDO" wa filamu Mzee wa Swagga kuwa imekopiwa.
Nijibu jibu fupi bila kusita kuwa kweli Story imekopiwa na original Story inaitwa Ladies Vs Ricky Bahl na mimi ndiye niliyemshauri JB kuichukua Story hiyo yenye maudhui ya kuvutia. Nataka nieleze sababu ya kufanya hivyo ila kabla sijaeleza sababu ningependa kuwaambia wale wote wanaotumia skendo hii kuyarefusha mambo haya kuwa kwenye ulimwengu wa filamu ni jambo la kawaida duniani watu kuchukua maudhui ya story na kuyatengeneza katika mazingira yao endapo maudhui hayo yataelimisha au kukosoa au kufurahisha kuhusu jambo..watakaoendelea kulalamika baada ya ujumbe huu ni dhahiri wanania zao nyingine na si kujenga.
Kwanza kabisa mimi ndiye mwandishi mkuu wa filamu za JB kuanzia enzi za DJ Ben, Dereva Taxi, Nakwenda kwa Mwanangu, Shikamoo Mzee, Bado Natafuta mpaka hii Mzee wa Swagga na hizo nyingine zote zikiwa ni original scripts kutoka kwenye ubongo wangu.
Filamu anazofanya JB ni Romantic Comedies na Inspirational Comedies kwa hiyo yeye huwa anapenda maudhui ya kuentertain zaidi yani filamu zenye kuchangamsha na kuburudisha tofauti na waigizaji wengine kama Single Mtambalike anayependelea filamu za ugentleman zaidi (haya ni kutokana na kukaa nao na kuzungumza nao na kuwafahamu kwa kina).
Sasa kuhusu Mzee wa Swagga:
JB alitengeneza filamu mfululizo zenye maudhui tofauti na alizozoeleka, kama Hukumu ya Ndoa, Mikono Salama ambazo sikuziandika mimi na nakiri kuwa hazikufanya vizuri sana sokoni.
Sababu ya filamu hizi kuandikwa na watu wengine ni sababu nilikuwa nashughulika na Script ya filamu yangu mwenyewe niliyoproduce mwaka jana October inayoitwa SAFARI YA GWALU (bado haijatoka mpaka mwezi wa 3 mwishoni), aliyoigiza Gabo kama kijana anayerudi shule ya msingi baada ya kupigika na maisha.
Filamu hii imenichukua mwaka mzima kuanzia kuiandika mpaka kuja kuproduce, kuandika ilianza January-march 2014 hivyo sikupata nafasi kumuandikia JB tangu tulipotoa BADO NATAFUTA na CHARLE MVUVI (bado haijatoka).
Baada ya filamu hizi mbili (Hukumu ya Ndoa na Mikono Salama);JB alinieleza angetamani nimuandalie Filamu na Mzee Majuto wakati huo wakiwa safarini kwenda Uturuki ili wakashoot Uturuki iwe filamu kali. Wakati nikiandaa filamu hiyo mshtuko mkubwa ukaja kwa misiba ya mfululizo ya wana Tasnia wenzetu iliyopelekea Safari ya JB na Mzee Majuto ya Uturuki kufa na hivyo kufanya hata script niliyoandaa kukosa msisimko tena.
Baada ya matatizo JB alitaka filamu inayofanana na Senior Bachelor, DJ Ben na Nakwenda kwa Mwanangu, akiigiza kama mburudishaji zaidi na kwa kuwa sikuwa na Idea mpya kwenye kichwa na muda ulikuwa unaenda sana na anahitajika kupeleka filamu yake kwa msambazaji ikabidi nitafute story itakayofanana na JB mburudishaji tunayemfahamu muda mrefu;
kwa ninavyomuelewa vizuri JB labda kuliko waandishi wengi wanavyomuelewa hiyo haikuwa ngumu kutafuta wazo la kumfaa na ndipo tukaipata Ladies Vs Rick Bahl, JB aliipenda ila sote tulikuwa na wasiwasi kwani JB ni muoga sana wa kuandikwa vibaya, nikamwambia jambo ambalo nataka niwaeleze nanyi leo. Jambo ambalo lilimfanya JB kukubali niandike script mpya kupitia kisa kile na kuiproduce...
Ukweli ni kuwa duniani kote (masoko ya filamu yote namaanisha) watu wanapoona maudhui ya story ya nchi au taifa jingine kuwavutia wanaweza kuchukua maudhui hayo na kuyatumia kutengeneza filamu za maudhui yale kwenye mazingira yao. Kuna Filamu nyingi hapa Tanzania na Nigeria na Bollywood Hata Hollywood zimefanyika hivyo na si dhambi.
Kama Tanzania tazama filamu Ya BEST MAN ya Hemedi na Yussuf Mlela, ni copy ya BEST MAN ya Morris Chestnut na Taye Diggs...
Nollywood filamu Ya GUARDIAN ANGEL ya Ramsey Noah ni copy ya Filamu HATYA ya Bollywood ya Govindah...
Pia filamu za ROMEO AND JULIET developed kutoka kwa William Shakespears plays zimekopiwa Bollywood kwenye filamu iliyoleta Mabadiliko makubwa Bollywood ya QAYAMAT SE QAYAMAT TAK kama nasema uongo mtu aziangalie na kuja kunikosoa na nitaleta dazeni ya filamu zilizokopiwa kutoka nchi na nchi.
Ila nataka kuuliza swali, mbona nyingine zilizokopiwa hapa Tanzania toka nje hazikuzungumziwa kama Mzee wa Swagga?
Nadhani jibu ni moja tu: sababu JB ameitendea haki filamu hiyo. Ila tusiende huko !
Jambo jingine (nadhani ndio la msingi zaidi), mnapokaa kulaumu mjue kazi ya kuwapa watazamaji kitu wanachotaka kila siku na kuwafanya wakupende si suala dogo, tunaumiza vichwa mchana na usiku.
JB si kwamba namfagilia sababu namuandikia ila huwa anaumia sana kutafuta story mpya na ukweli hata mimi nateseka sana kutengeneza vitu vipya na ukitazama mtu huyu mmoja atengeneze filamu 6 au 7 kwa mwaka na zote mzipende na kufurahia inahitaji kujitoa kwa hali ya juu.
Nikiwa kama mwandishi kihalali nahitaji kuandika script 2 tu kwa mwaka ili nitoe vitu vikali, unapoelemewa na mzigo ni rahisi kuharibu kazi na kwa kuwa tunajitahidi (mimi na JB) kuwapa mnachopenda basi huwa tunatafuta kila njia kutowakwaza mashabiki, naomba mtuhurumie nasi kwani mazingira ya kazi ni magumu mno.
Kwa haya niliyoandika ningependa kuwaambia tusiwe watu wa kulaumu na kuhukumu, mimi kuproduce filamu yangu mwaka jana kumepunguza kujitoa kwangu kuandaa filamu kali za JB, mimi ndiye wa kulaumiwa na si JB.
Na kwa niaba ya mashabiki wa JB nawaomba radhi kama kwa namna moja au nyingine mmejisikia vibaya ila kwa niliyoeleza mtaungana nami kuwa si dhambi kufanya hivyo inapobidi na tushirikiane kupeleka gurudumu hili mbele.
Nikiwa kama mwandishi bora wa script (Kama nilivyotambuliwa na ZIFF, JULY 2014 kupitia Filamu ya "SHIKAMOO MZEE") natambua jukumu langu kama mwandishi simkingii kifua JB bali nasimamia kile ninachokifanya kama Professional.
Naomba tuache kuongea na tushirikiane kuboresha filamu zetu."

Daniel Manege

Duuh! mkuu hilo jina lako la pili kule kwetu huwezi kulitamka!
 
Upo sahihi Boss,

Hii stori ilikuwepo hapa kwenye "JB na Scandal mpya ya kuiba mawazo ya Movie ya ''Ladies Vs Ricky Bahl"

Mi nimefanya kuleta upande wa pili wa stori toka kwa muandishi wa husika,
ndio maana hiyo stori imekaa kama nanukuu tu.

Hivyo kwa kuweka kumbukumbu sahihi Mimi si Daniel Manege ila ni mjumbe wa JF kama ilivyo wewe.

Punguza munkari Boss!

Umeeleweka mkuu tena bora daniel amejitetea sema humu jf kimekuwa kama kijiwe cha wahuni na mafundi wa kushushua wenzao. Mleta mada amem quote mwandishi wa hiyo muvi sasa mtu mnamuattack mleta mada its not fair.
 
Mwambie utetezi wake ni dhaifu kabisa....mwambie kwanini aliandika mtunzi wa story ni JB?
Kwanini haku acknowladge?
Kwanini JB mwenyewe haoneshi kukubali kosa anajifanya kukomaza shingo huku akijua inaweza vunjika?

Muulize kwa hiyo anajaribu kusema kukopi na kupaste ni jambo la kawaida?Muulize ni movie ngapi hadi sasa amekopi na kupaste?

Muulize tusinge baini alipanga kusema ukweli lini?
Mwambie akaandike utetezi mwingine!

Tena asituchefue tukaanza kupekua na movie nyingine za kihindi maana hyo sio movie ya kwanza kuiba hyo, Regina nae aliiba tukamchunia kimya hii nayo tena kaiba, tatizo wanaona wote wanaoangalia bongo movie ni matahira kam wao
 
Umeeleweka mkuu tena bora daniel amejitetea sema humu jf kimekuwa kama kijiwe cha wahuni na mafundi wa kushushua wenzao. Mleta mada amem quote mwandishi wa hiyo muvi sasa mtu mnamuattack mleta mada its not fair.

Huu utetezi ulipaswa kuletwa na JB toka mwanzo si kusubiri mbeleko! hata hivyo utetezi wako ni moja ya utetezi dhaifu kabisa! Kilicho wafanya waandike mtunzi ni JB?
 
Kwahiyo ndio kusema hizo mikitu yenu mnayoigiza ni copy za original ili mayaya waelewe Holywood world?basi igizeni Tekken 1 maana mtaani kwangu mayaya wanaipenda
 
Huu utetezi ulipaswa kuletwa na JB toka mwanzo si kusubiri mbeleko! hata hivyo utetezi wako ni moja ya utetezi dhaifu kabisa! Kilicho wafanya waandike mtunzi ni JB?

Imekuwa utetezi wangu tena mm ndo manege acheni hizo angalau amejaribu kujitokeza na kujieleza mbona mnakuwa hivyo. Tena wewe rutta ungetulia maana huwa mtetezi sana wa mafisadi.
 
Ukweli ni kuwa duniani kote (masoko ya filamu yote namaanisha) watu wanapoona maudhui ya story ya nchi au taifa jingine kuwavutia wanaweza kuchukua maudhui hayo na kuyatumia kutengeneza filamu za maudhui yale kwenye mazingira yao. Kuna Filamu nyingi hapa Tanzania na Nigeria na Bollywood Hata Hollywood zimefanyika hivyo na si dhambi.
Hakuna kitu kwamba eti ni jambo la kawaida duniani kutumia maudhui ya filamu nyingine... huu ni uongo usio na maana yoyote vinginevyo kusingekuwa na suala la hati miliki kwenye filamu! Jana hapa nimetoa mifano mingi kwamba, hata script, achilia mbali filamu, nazo zinakuwa copyrighted, so how come tena mtu apoteze gharama zake ku-copy right material yake halafu iwe avaialble to anybody??

Kinachokubalika kwenye filamu ni kuchukua wazo/idea na sio maudhui/content na hata katika ku-copy right, huwezi ku-copy right wazo/idea ingawaje unaweza kuuza wazo/idea! Unaruhusiwa kuchukua kasehemu kadogo sana kafilamu, tena kasikofika hata dakika moja kisha ukaka-develop... kwamba kale kasehemu, kanakuwa ni idea ambayo unai-develop into a new script... hilo linakubalika lakini sio kuchukua madakika kadhaa ya filamu husika au scenes kadhaa za script husika halfu watu waseme hiyo inakubalika... hakuna kitu kama hicho na ukiona kimefanyika basi fahamu wamekubaliana! Mathalani, Hollywood huwa wananunua indie movies (filamu zinazotengenezwa na vimapuni vidogo/indie companies) na kuzi-develop into major movies! Hizi indie movies hawazinunui sokoni au supermarket bali wanazinunua kutoka kwa wamiliki... yaani, assume Producer ameiona filamu ya Mzee wa Swaga ya JB na ameipenda! Hapo ana-opt kufanya biashara na JB na kuinunua movie husika kwa thousands or millions of dollars kisha yeye anaenda kuitengeneza upya! Katika mazingira kama haya, mahudhui/content inaweza kufanana lakini pia kunakuwa na makubaliano mtu kama JB atapata nini akitokea third part akaipenda the same film lakini kutokea kwa new producer/mmiliki!!! Wakati wanauziana, haya yanakuwa tayari wameshayaweka sawa manake anaweza kutokea mwingine akataka kutumia hayo mahudhui kutengeneza series! Je, JB alifanya kitu kama hicho? Na more important, hata kama huyo producer amenunua filamu kwa JB lazima kwenye filamu yake mpya atoe credit... je, JB amefanya hilo jambo?

Hapa wanatetea ujinga na wala hawaelekei ikiwa wanafahamu hizi habari za filamu at higher level.
 
Anasema anaumia mno na kuumiza akili katika kutunga story! warumi umemwelewa huyu mvivu? Sasa anataka kazi yake iwe nyepesi....! Sipendi kuangalia movie ya bollywood version ya kibongo tena bila credit kwa vile ulitingwa! Uli na matingo jobha

Amatingo ghikufuma kughu gwe mwanike!?
Wakati mtu kawaomba msamaha!!

Itapendeza mwamko huu tuuonyeshe kwenye filamu zote basi....
Pia inafurahisha kwamba movie hii imefuatiliwa sana
 
Last edited by a moderator:
Amatingo ghikufuma kughu gwe mwanike!?
Wakati mtu kawaomba msamaha!!

Itapendeza mwamko huu tuuonyeshe kwenye filamu zote basi....
Pia inafurahisha kwamba movie hii imefuatiliwa sana

Mr Gwalu, unaweza wewe na Jb mkatutafsiria white house down kibongo movie halafu JB ndio anamuokoa kikwete dhidi ya magaidi wa amboni au panya road?
 
Mr Gwalu, unaweza wewe na Jb mkatutafsiria white house down kibongo movie halafu JB ndio anamuokoa kikwete dhidi ya magaidi wa amboni au panya road?

Hahahahaha maatope ndugu yangu acha kunishikia chini bana...
Ila huu ukali inabidi muwe nao kwenye movie zote aisee.
Dogo amejitetea na amekubali lawama

Ila hivi ni vitu vya kawaida sema tu kamba hukatikia pembamba
 
Last edited by a moderator:
Umeeleweka mkuu tena bora daniel amejitetea sema humu jf kimekuwa kama kijiwe cha wahuni na mafundi wa kushushua wenzao. Mleta mada amem quote mwandishi wa hiyo muvi sasa mtu mnamuattack mleta mada its not fair.

Ahsante Queen Kyusa,
Watu wanaongozwa na hisia hata kutulia hamna basi ni rahisi hata kutokuona kuwa mhusika amewaomba msamaha!!
 
Last edited by a moderator:
Amatingo ghikufuma kughu gwe mwanike!?
Wakati mtu kawaomba msamaha!!

Itapendeza mwamko huu tuuonyeshe kwenye filamu zote basi....
Pia inafurahisha kwamba movie hii imefuatiliwa sana

Kuomba msamaha ndio mwisho wa mjadala? JB ana jadiliwa kwa kuwa kitu kama hiki hakikutegemewa kifanywe na yeye.
 
Kuomba msamaha ndio mwisho wa mjadala? JB ana jadiliwa kwa kuwa kitu kama hiki hakikutegemewa kifanywe na yeye.

Sio lazima mjadala ufungwe Rutta,
Ila mjadala unaweza ukabadili muelekeo sasa...
Huyo Miss niliyekuwa namjibu alisema kuwa "ndi na matingo" (kinyakyusa) akimaanisha malingo...
Naamini alikuwa akimaanisha Daniel,
Hivyo nikamjibu, malingo yanatokea wapi wakati mtu ameomba msamaha...
 
Unasema sio wewe ulieandika haya? Kwa hiyo ni coincidence tu huyo mwandishi Daniel Manege naye kaandaa filamu ya safari ya Gwalu jina linaloendana na id yako ya jf?

Mkuu naomba nikuhakikishie kuwa aliye present ujumbe huo yaani JouneGwalu sio Dan Manege, nje ya JF wote nawafahamu, hata shughuli zao ni tofauti.

Kidogo nipo tofauti na wengi kwa sababu kwanza namuona Script writer ni mtu unayeelewa uzito wa hili suala. Naamini alinuia vema kuandaa epistle hiyo kama sehemu ya confesion ya kutumia idea ya mtu ktk kazi yake pasipo prior owners acknowledgement.

Pamoja na udhaifu huo amekiri, na ninadhani sasa huu uwe msingi wa kujenga ushirika na wasanii wa filamu Tanzania ili kuongeza ideas ambazo hazijatumika.

Kwa Pamoja tunaweza.
 
Kijana anajikana ! hii inadhihirisha uongo kwenu jad
maelezo yako yanadai una filamu inaitwa safari ya gwalu, id yako je
 
Back
Top Bottom