January - ni kweli tuna tatizo la umeme lakini usimwagie petroli kwenye moto unaowaka

Jibaba Bonge

JF-Expert Member
May 6, 2008
1,246
401
Nimashangazwa sana na msimamo wa Janauary Makamba kunga'ng'ania kuendelea na mkataka feki wa Dowans, ambao kwa kiasi kikubwa umeleta tafrani katika nchi yetu. Sijui kama na yeye anatekeleza malengo ya mafisadi kama yule Makamba mwingine anavyofanya.
Hivi uelewa wa January kuhusu tatizo la umeme umeishia kwenye mitambo ya Dowans?! kwa nini hiyo energy ya kufikiri asiitumie kutafuta permanent solution, kwa mfano, ya kuwa na mitambo yetu wenyewe ambayo bei yake haitakuwa inflated kama ilivyofanywa hii ya Richmond / Dowans ili kupandisha unit price ya umeme na capacity charge ili kuwanyonya watanzania?

January usiijiingize kichwa kichwa kwenye ufisadi huu wa Richmond / Dowans na ubunge usikuvimbishe kichwa hadi kutaka kupasuka.
 
Makamba jr=Makamba sr !!!!! sasa amekuwa msemaji wa dowans!!! wenye shida ya umeme ni sisi sio wao wenye majenereta kila kona ya nyumba, wasituongezee mzigo wa gharama hizi za sukari na unga zinatutosha jamani !! mnyonge mnyongeni lakini haki zetu mtupee !!! acha tukae gizani tuuuu
 
kuna watu walikuwa wanamsifia sana huyu january, yaani huyu jamaa inaonekana hana "political feelings" kabisa. angekuwa nazo angekaa mbali sana na huyu alhadawi na sio kuongea statement za kumtetea
 
Wabongo bwana... unafiki tupu, mtu ukiibiwa Taa ya gari, mwenyewe unajipeleka gerezani kununua mali wako kwa aliyekuibia.... Sasa hili la Dowans mnijifanya mnauchunguuuu...... Accept the inevitable we need electricity NOW!!!!
 
Wabongo bwana... unafiki tupu, mtu ukiibiwa Taa ya gari, mwenyewe unajipeleka gerezani kununua mali wako kwa aliyekuibia.... Sasa hili la Dowans mnijifanya mnauchunguuuu...... Accept the inevitable we need electricity NOW!!!!

Bado huna ushawishi wa hoja zako...kuibiwa taa ya 50,000 sio sawa na kuibiwa 96bn
 
kuna watu walikuwa wanamsifia sana huyu january, yaani huyu jamaa inaonekana hana "political feelings" kabisa. angekuwa nazo angekaa mbali sana na huyu alhadawi na sio kuongea statement za kumtetea

"Like father like son" Usitegemee jipya na la maana.
 
Wabongo bwana... unafiki tupu, mtu ukiibiwa Taa ya gari, mwenyewe unajipeleka gerezani kununua mali wako kwa aliyekuibia.... Sasa hili la Dowans mnijifanya mnauchunguuuu...... Accept the inevitable we need electricity NOW!!!!

Two wrongs do not make it right. Hilo la kuibiwa taa ya gari na kwenda kuinunua tena ni udhaifu katika uwezo wetu wa kufuatilia haki zetu na miundombinu ya kuwezesha kuzitambua haki zetu. Na hii haina maana kuwa tukubali kuwa hiyo ni sahihi...
 
Mpaka tutakapostuka kuwa bwana mdogo nae ni 'kijana' wao, tushaibiwa!
 


Defiant Gaddafi vows to fight on

In televised speech, Libyan leader blames youths inspired by regional events for uprising and vows to die a 'martyr'. ( 23-Feb-2011 )

SWALI HUMU: UTAMADUNI WA KURITHISHA WATOTO WA WAKUBWA
UKUBWA TANZANIA CHANZO CHAKE NI WAPI???


Nani anayejua hasa darasa la huyu King of Kings?

Kwa mtaji wa hutuba aliyoitao hivi majuzi ni mara mia angjinyamazia tu hivyo tungeendelea kumfikiria mstaarabu fulani hivi. Kwa kujiunga kwake jeshini akiwa na umri wa miaka 12 (child soldier) wala hatuhitaji kuuliza kama 'ALIONEWA SANA YEYE', 'AKADHALILISHWA SANA GADDAFI' hivyo kuja kupata kamwanya wa kuongoza nchi kwa mtindo wake mwenyewe hivi sasa anarudishia ngumi kwa jamii nzima ya Libya.

Tujifunze kitu basi na sisi hapa kwamba wale tuliowahi kuwaondoa kwenye nyadhifa fulani hapa nyumbani kufuatia kashfa iliyogoma kwisha katikati yetu hadi leo, nao wakija tu kupata urais wa nchi hii mtindo wao wenyewe na tusifikirie matendo yao kutofautiana sana na ya huyu nduli hapa.

Hakika shule iliomuingia mtu na kutulia ndani mwake ni muhimu zaidi tena sana kuliko shule ya kupitia hata kama madarasa yako ni mengi kimahesabu vidoleni.

Kanali Gaddafi ajikaanga kwa ulimi wake mwenyewe. Na watoto wake , masikini ya Mungu, ndio kabisaa wanaamini taifa zima la Libya ni kama shamba binafsi la ukoo kwa baba yao.

Nikitazama ya Ben Ali wa Tunisia, nikamgeukia Hosni Mubarak wa Misri na kumtaza mzee huyu ambaye kimawazo ni 'chipukizi' tu, na mwenendo mzima wa ushiriki wa familia zao katika mambo ya utawala wa nchi, Wa-Tanzania wenzangu NAPATA MAJIBU KUBWA SANA HAPA HAPA NYUMBANI kwamba ni kwa nini kati ya marais wetu wote wanne ni wawili tu kati yao ambao waonekana kupenda saana KUWARITHISHA UKUBWA WA TAIFA HILI kimtindo!!

Endapo Hussein Mwinyi hatojiuzulu ya Gongolamboto kwa kiburi tu kama ya watoto wa marais niliotangulia kuwataja kaskazini mwa bara hili basi huenda hata UKUBWA WA ZANZIBAR unaotazamiwa kwake ukagoma lakini ya Muungano ndio kabisaaaa wa kusikia tu redioni.

Je, inamaana wazee wengine akina Salim Ahmed Salim, Sinde Warioba, Mwalimu Nyerere, Phili Mangula, Joseph Rwegasira, Salmin Amour, Seif Shariff Hamad, Duni Haji Duni, Bibi Titi, Mama Mongela, Edith Mnuo, Dr Slaa, Prof Mwandosya, Prof Baregu, Mzee Kisumo, Edwin Mtei, Kambona, na wengine wengi tu ... wao hawana watoto wa kuwea nao kutamani kuwarithisha UKUBWA???

Mfano mzuri hebu angalia anavyoshiriki kuifanyi udalali nchi ya January Makamba, kijana mdogo mwenetu, ambaye angelihitaji kwa wivu zaidi ustawi mzuri wa Tanania. Katika hili tayari Vijana wa Tanzania TUMEWASOMA MCHEZO MZIMA na majibu tunayo!!!
 
Huyu January pale alipoanza kwa kuandikia barua serikali juu ya umeme na hatimaye kupewa huo uwenyekiti nilishahisi jambo
 
Two wrongs do not make it right. Hilo la kuibiwa taa ya gari na kwenda kuinunua tena ni udhaifu katika uwezo wetu wa kufuatilia haki zetu na miundombinu ya kuwezesha kuzitambua haki zetu. Na hii haina maana kuwa tukubali kuwa hiyo ni sahihi...

In the meantime people are losing jobs that feed, clothe and shelter hundreds due to power cuts effect on Companies.... I say better the devil you know... I hard pill to swallow i know....
 
Cottoneyejoe...nahofia uwezo wako wa kufikiri,,,tuambie unawezaje kufananisha kifo na usingizi au ndo walewale???january ni mamluki aliyebatizwa na kula kiapo cha utii ktk kuhujumu nchi..na sasa anaelekea kuwa adui no 1 wa tz
 
January makamba is still a novice and inexperienced politician.we would advise him to correctly understand the conteporary politics of this country.anything short of that will be tantamount to putting himself in a melting pot.be careful young makamba.
 
Cottoneyejoe...nahofia uwezo wako wa kufikiri,,,tuambie unawezaje kufananisha kifo na usingizi au ndo walewale???january ni mamluki aliyebatizwa na kula kiapo cha utii ktk kuhujumu nchi..na sasa anaelekea kuwa adui no 1 wa tz

Nina applaud patriotism yako... but i honestly dont care anymore... just want electricity no matter who is dishing it... problem with TZ is too much blah blah with no alternatives.... Wabongo ndio mnachojua.... Even when they do find other alternatives u will have something else too wap about... its wat u r good at, wapping but not coming up with viable SHORT TERM ALTERNATIVES.....
 
Back
Top Bottom