Tatizo la Maji na Umeme ni matokeo ya kutegemea chanzo kimoja kwa miaka yote ya uhai wa Tanzania, Serikali ya awamu ya sita imeamua kulimaliza

Robert S Gulenga

JF-Expert Member
Jan 3, 2013
2,161
1,493
Hakuna asiye jua kuwa kwa sasa kuna shida ya Maji na Umeme kwa baadhi ya maeneo hasa Mkoa wa Dar Es Salaam, tatizo ambalo kwa kiasi kikubwa limechangiwa na upungufu wa mvua ambazo zilitakiwa ziwe zimeanza kunyesha toka mwezi September ili kuweza kujaza mito ambayo inamwaga maji yake katika mito inayotumika kama chanzo cha maji yanayotumika nyumbani na viwandani mfano Ruvu. Aidha, mabwawa yanayotumika kuzalisha umeme nayo yamepungua kina na hivyo kusababisha upungufu wa uzalishaji umeme.

Kwa miaka yote toka Tanganyika kupata uhuru na baadaye Tanzania kuzaliwa (baada ya Muungano wa Zanzibar na Tanganyika) tumekuwa tukitegemea mito na mabwawa kama chanzo kikuu cha maji yanayotumika nyumbani na viwandani, pia mabwawa kama chanzo cha uzalishaji umeme, ambavyo vyote vinategemea uwepo wa mvua za kutosha. Mabadiliko ya hali ya hewa duniani kote yamesababisha upungufu mkubwa wa mvua, hivyo kufanya mito na mabwawa mengi kukosa maji ya kutosha kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na viwandani.

Tatizo hili halijaanza jana wala juzi, tatizo hili ni matokeo ya kuwa na chanzo kimoja, hata kama Serikali ingekuwa inaongozwa na Chadema au ACT au chama chochote nje ya CCM hakuna namna ambayo wangeweza kutatua tatizo hili kwa siku mbili au ndani ya mwezi mmoja.

Serikali ya Awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutambua kuwa maji na umeme ni uhai kwa kila Mtanzania, imefanya juhudi za haraka na makusudi ili kuondoa tatizo hili, Serikali imepeleka fedha nyingi kuhakikisha miradi ambayo ilikuwa haijakamilika inakamilika na kuweza kutoa huduma kwa Mkoa wa Dar Es Salam. Serikali imeendelea kuchukua hatua za muda mfupi na za muda mrefu kuhakikisha changamoto hii inatatuliwa moja kwa moja.

Watanzania kwa umoja wetu, tuendelee kuiunga mkono Serikali yetu katika jitihada za kutatua changamoto za maji na umeme.

Tumuunge mkono Waziri wa Maji na Umwagiliaji -Juma Aweso pamoja na Wataalamu wake, ni muda sasa umefika kuanza kuangalia namna ya kufanya bahari kuwa chanzo kikuu cha maji yakutumika nyumbani na viwandani, Dunia iko mbali na Teknolojia iko mbali. Mito na mabwawa sio chanzo cha kuaminika tena katika dunia hii ambayo mabadiliko ya hali ya hewa na athari zake si jambo la kuuliza tena.

Tumuunge mkono waziri wa Nishati -January Makamba pamoja na Wataalamu wake wakati huu wakipambana kuhakikisha tunapata vyanzo vya uhakika vya umeme. Kwa miaka yote tumekuwa tukitegemea maji kama ndio chanzo chetu cha uzalishaji wa umeme. Mheshimiwa January Makamba, pamoja na spana zote unazopigwa ambazo pengine hustahili kabisa, Mwenyezi Mungu atakulipa kwa kadri utakavyoiwezesha Tanzania kutoka katika umeme wa kutegemea chanzo cha maji, kwa namna mabadiliko ya hali ya hewa yalivyo nachelea kusema baada ya miaka 10 ijayo maji itakuwa ngumu saana kutumika kama chanzo cha kuzalisha umeme.

Mungu Ibariki Tanzania.

Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.
 
Hakuna asiye jua kuwa kwa sasa kuna shida ya Maji na Umeme kwa baadhi ya maeneo hasa Mkoa wa Dar Es Salaam, tatizo ambalo kwa kiasi kikubwa limechangiwa na upungufu wa mvua ambazo zilitakiwa ziwe zimeanza kunyesha toka mwezi September ili kuweza kujaza mito ambayo inamwaga maji yake katika mito inayotumika kama chanzo cha maji yanayotumika nyumbani na viwandani mfano Ruvu. Aidha, mabwawa yanayotumika kuzalisha umeme nayo yamepungua kina na hivyo kusababisha upungufu wa uzalishaji umeme.

Kwa miaka yote toka Tanganyika kupata uhuru na baadaye Tanzania kuzaliwa (baada ya Muungano wa Zanzibar na Tanganyika) tumekuwa tukitegemea mito na mabwawa kama chanzo kikuu cha maji yanayotumika nyumbani na viwandani, pia mabwawa kama chanzo cha uzalishaji umeme, ambavyo vyote vinategemea uwepo wa mvua za kutosha. Mabadiliko ya hali ya hewa duniani kote yamesababisha upungufu mkubwa wa mvua, hivyo kufanya mito na mabwawa mengi kukosa maji ya kutosha kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na viwandani.

Tatizo hili halijaanza jana wala juzi, tatizo hili ni matokeo ya kuwa na chanzo kimoja, hata kama Serikali ingekuwa inaongozwa na Chadema au ACT au chama chochote nje ya CCM hakuna namna ambayo wangeweza kutatua tatizo hili kwa siku mbili au ndani ya mwezi mmoja.

Serikali ya Awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutambua kuwa maji na umeme ni uhai kwa kila Mtanzania, imefanya juhudi za haraka na makusudi ili kuondoa tatizo hili, Serikali imepeleka fedha nyingi kuhakikisha miradi ambayo ilikuwa haijakamilika inakamilika na kuweza kutoa huduma kwa Mkoa wa Dar Es Salam. Serikali imeendelea kuchukua hatua za muda mfupi na za muda mrefu kuhakikisha changamoto hii inatatuliwa moja kwa moja.

Watanzania kwa umoja wetu, tuendelee kuiunga mkono Serikali yetu katika jitihada za kutatua changamoto za maji na umeme.

Tumuunge mkono Waziri wa Maji na Umwagiliaji -Juma Aweso pamoja na Wataalamu wake, ni muda sasa umefika kuanza kuangalia namna ya kufanya bahari kuwa chanzo kikuu cha maji yakutumika nyumbani na viwandani, Dunia iko mbali na Teknolojia iko mbali. Mito na mabwawa sio chanzo cha kuaminika tena katika dunia hii ambayo mabadiliko ya hali ya hewa na athari zake si jambo la kuuliza tena.

Tumuunge mkono waziri wa Nishati -January Makamba pamoja na Wataalamu wake wakati huu wakipambana kuhakikisha tunapata vyanzo vya uhakika vya umeme. Kwa miaka yote tumekuwa tukitegemea maji kama ndio chanzo chetu cha uzalishaji wa umeme. Mheshimiwa January Makamba, pamoja na spana zote unazopigwa ambazo pengine hustahili kabisa, Mwenyezi Mungu atakulipa kwa kadri utakavyoiwezesha Tanzania kutoka katika umeme wa kutegemea chanzo cha maji, kwa namna mabadiliko ya hali ya hewa yalivyo nachelea kusema baada ya miaka 10 ijayo maji itakuwa ngumu saana kutumika kama chanzo cha kuzalisha umeme.

Mungu Ibariki Tanzania.

Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.
awamu ya 5 walikuwa wanatumia vyanzo gani
 
awamu ya 5 walikuwa wanatumia vyanzo gani
Kadri miaka inavyosonga ndivyo tatizo la madiliko ya hali ya hewa linavyozidi kuwa kubwa, miaka minne iliyopita kiwango cha mvua sio sawa na kiwango cha mvua cha mwaka jana, idadi ya watu waliokuwepo miaka minne iliyopita sio sawa na sasa, Kuna kuongezeka kwa shughuli za uchumi etc. Mahitaji ya maji na umeme kwa leo ni makubwa zaidi ukilinganisha na miaka minne iliyopita,
 
Bandiko zuri Ila nakurekebisha. Maji sio chanzo kiiubwa Cha kuzalisha umeme hapa Tz. Umeme unaozalishwa na maji ni 33% tu. Gesi ndio chanzo kikuu 65%
 
Ngoja niwe mpole tu, yanayoendelea yapi hayo mkuu? Ukiyataja nitakujibu vibesen xxx

..Tatizo ni CCM kuwa wazembe na kubweteka.

..Uwepo wao madarakani hautegemei kura za wananchi.

..Chama kinachotegemea kura za wananchi hakiwezi KUBWETEKA kama CCM na kutokuwa na mikakati ya dharura kukabiliana na changamoto za huduma muhimu kama umeme, na maji.
 
Kadri miaka inavyosonga ndivyo tatizo la madiliko ya hali ya hewa linavyozidi kuwa kubwa, miaka minne iliyopita kiwango cha mvua sio sawa na kiwango cha mvua cha mwaka jana, idadi ya watu waliokuwepo miaka minne iliyopita sio sawa na sasa, Kuna kuongezeka kwa shughuli za uchumi etc. Mahitaji ya maji na umeme kwa leo ni makubwa zaidi ukilinganisha na miaka minne iliyopita,

Ni makosa makubwa sana kuendelea kutegemea umeme wa maji.
Maji yanazidi kuwa adimu. Mvua nazo zinaendelea kuwa za mashaka.
Tunalo jua tena la kutosha. Tuna geothermal zones. Tuna upepo na mawimbi ya baharini.
Lakini sote tumekaa tunadanganywa kuwa umeme wa maji ndo suluhuhisho! UONGO!

Kuhusu maji kwa matumizi ya mbalimbali nadhani hapa vinakosekana vitu vitatu: Elimu, Teknolojia na Utashi.
1. Ardhini kuna maji. Tuchimbe visima virefu!
2. Baharini kuna maji. Tuyabadilishe yafae kwa matumizi!
3. Angani kuna maji mengi.
Tuamke tuache kudanganyana!
 
..Tatizo ni CCM kuwa wazembe na kubweteka.

..Uwepo wao madarakani hautegemei kura za wananchi.

..Chama kinachotegemea kura za wananchi hakiwezi KUBWETEKA kama CCM na kutokuwa na mikakati ya dharura kukabiliana na changamoto za huduma muhimu kama umeme, na maji.
JokaKuu ndio maana Serikali imepeleka fedha nyingi kuchimba mabwawa ili kuondoa tatizo hili, nafikiri ni muhimu kuiamini Serikali hii inaweza ondoa kabisa tatizo la maji kwa kuja na vyanzo mbadala
 
Ni makosa makubwa sana kuendelea kutegemea umeme wa maji.
Maji yanazidi kuwa adimu. Mvua nazo zinaendelea kuwa za mashaka.
Tunalo jua tena la kutosha. Tuna geothermal zones. Tuna upepo na mawimbi ya baharini.
Lakini sote tumekaa tunadanganywa kuwa umeme wa maji ndo suluhuhisho! UONGO!

Kuhusu maji kwa matumizi ya mbalimbali nadhani hapa vinakosekana vitu vitatu: Elimu, Teknolojia na Utashi.
1. Ardhini kuna maji. Tuchimbe visima virefu!
2. Baharini kuna maji. Tuyabadilishe yafae kwa matumizi!
3. Angani kuna maji mengi.
Tuamke tuache kudanganyana!
Uko sahihi mkuu Jp Omuga kwa sasa na tunakoelekea umeme wa maji si suluhisho tena
 
Mvua zimeanza kunyesha kwa wingi sasa, hivyo tatizo la maji limemalizwa na Mungu na siyo awamu ya sita
Mkuu Algore ni kweli mvua zimeanza kunyesha baadhi ya sehemu, lakini bado mito na mabwawa yanayotegemewa hayajapata maji, Serikali inatambua umuhimu wa kuongeza vyanzo vipya
 
Uko sahihi mkuu Jp Omuga kwa sasa na tunakoelekea umeme wa maji si suluhisho tena
Na huo ndo ukweli. Tutafute energy mix ili tuwe ma uhakika zaidi.
Kingine tuachane na mtandao wa kitaifa (national grid). Tuwekeze kwenye Mini grids za kimkakati. Majanga yatokanayo na mabadiliko ya tabianchi yanazidi kuongezeka. Tusipokuwa werevu zipo nyakati tutakosa umeme nchi nzima
 
Hakuna asiye jua kuwa kwa sasa kuna shida ya Maji na Umeme kwa baadhi ya maeneo hasa Mkoa wa Dar Es Salaam, tatizo ambalo kwa kiasi kikubwa limechangiwa na upungufu wa mvua ambazo zilitakiwa ziwe zimeanza kunyesha toka mwezi September ili kuweza kujaza mito ambayo inamwaga maji yake katika mito inayotumika kama chanzo cha maji yanayotumika nyumbani na viwandani mfano Ruvu. Aidha, mabwawa yanayotumika kuzalisha umeme nayo yamepungua kina na hivyo kusababisha upungufu wa uzalishaji umeme.

Kwa miaka yote toka Tanganyika kupata uhuru na baadaye Tanzania kuzaliwa (baada ya Muungano wa Zanzibar na Tanganyika) tumekuwa tukitegemea mito na mabwawa kama chanzo kikuu cha maji yanayotumika nyumbani na viwandani, pia mabwawa kama chanzo cha uzalishaji umeme, ambavyo vyote vinategemea uwepo wa mvua za kutosha. Mabadiliko ya hali ya hewa duniani kote yamesababisha upungufu mkubwa wa mvua, hivyo kufanya mito na mabwawa mengi kukosa maji ya kutosha kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na viwandani.

Tatizo hili halijaanza jana wala juzi, tatizo hili ni matokeo ya kuwa na chanzo kimoja, hata kama Serikali ingekuwa inaongozwa na Chadema au ACT au chama chochote nje ya CCM hakuna namna ambayo wangeweza kutatua tatizo hili kwa siku mbili au ndani ya mwezi mmoja.

Serikali ya Awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutambua kuwa maji na umeme ni uhai kwa kila Mtanzania, imefanya juhudi za haraka na makusudi ili kuondoa tatizo hili, Serikali imepeleka fedha nyingi kuhakikisha miradi ambayo ilikuwa haijakamilika inakamilika na kuweza kutoa huduma kwa Mkoa wa Dar Es Salam. Serikali imeendelea kuchukua hatua za muda mfupi na za muda mrefu kuhakikisha changamoto hii inatatuliwa moja kwa moja.

Watanzania kwa umoja wetu, tuendelee kuiunga mkono Serikali yetu katika jitihada za kutatua changamoto za maji na umeme.

Tumuunge mkono Waziri wa Maji na Umwagiliaji -Juma Aweso pamoja na Wataalamu wake, ni muda sasa umefika kuanza kuangalia namna ya kufanya bahari kuwa chanzo kikuu cha maji yakutumika nyumbani na viwandani, Dunia iko mbali na Teknolojia iko mbali. Mito na mabwawa sio chanzo cha kuaminika tena katika dunia hii ambayo mabadiliko ya hali ya hewa na athari zake si jambo la kuuliza tena.

Tumuunge mkono waziri wa Nishati -January Makamba pamoja na Wataalamu wake wakati huu wakipambana kuhakikisha tunapata vyanzo vya uhakika vya umeme. Kwa miaka yote tumekuwa tukitegemea maji kama ndio chanzo chetu cha uzalishaji wa umeme. Mheshimiwa January Makamba, pamoja na spana zote unazopigwa ambazo pengine hustahili kabisa, Mwenyezi Mungu atakulipa kwa kadri utakavyoiwezesha Tanzania kutoka katika umeme wa kutegemea chanzo cha maji, kwa namna mabadiliko ya hali ya hewa yalivyo nachelea kusema baada ya miaka 10 ijayo maji itakuwa ngumu saana kutumika kama chanzo cha kuzalisha umeme.

Mungu Ibariki Tanzania.

Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.
Huu upumbavu mtaacha lini?,
 
Back
Top Bottom