Kaa la Moto
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 7,903
- 1,053
- Thread starter
- #61
Mchukia fisadi asante sana kwa picha ila atleast kuna maendeleo kidogo nilikuwa kigoma mwaka 2005 pale kwenye makumbusho ya livingstone hakukuwa na nyumba nzuri namna hii!kulikuwa na kijumba kibaya baya tu!nakumbuka kulikuwa na babu anaelezea historia ya hapo yaani kakariri maneno maana aliongea maneno yale yale nilivyokuwa huko 2004!endelea kutuwekea maphotos ina maana Gungu hukufika?mbona sijaona picha
First lady,
Kwa siku zote nilizokuwa KG nakwambia nilikua tight vibaya sana. Muda wa kupumua na kulala nao nilikuwa naupata kwa shida. Ukichukulia ukweli kwamba hata kelele za usiku zilikuwa zikinisumbua sana.
Nilisikia kuna eneo linaitwa Gungu lakini sikubahatika kufika huko.
Nilikwenda KG kuona kama nitapata uwezekano wa kufungua kabiashara kangu fulani KG lakini ninasita sana kwa sababu bila ya power, na maji katanisumbua sana. Itanilazimu niingie gharama nyingi zaidi kwa ajili ya kuweka generator na kuweka tanki na kukodi magari ya kunibebea maji kila mara. Gharama zitaongezeka sana na cost of production might be higher too. Bado natafakari niende KG au niache.
Nadhani itanilazimu nipate tena muda wa kurudi kustudy zaidi mazingira ya kuwekeza huko.
Yule mzee wa pale makumbusho bado yupo pale pale na ndiye anayetoa historia ya pale. Na jengo ni lile lile linaloendelea kutumika unaweza kuliona ndani katika picha limejaa nyufa. Hata hivyo kwa sababu wanajenga lingine hatuwezi kushusha lawama zaidi.