Jumanne Mkota
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 2,917
- 1,660
Wanabodi wote Salaam sana
wiki moja tu iliyopita wabunge wetu waliwashutumu mawaziri kwa ubadhirifu mkubwa akiwemo waziri wa Kilimo ushirika Prof. Maghembe. Lakini wakati huo huo serikali ilikiri rasmi kupitia kwa nwaziri mkuu kuwa imepinda (haina fedha) sasa sikieni kioja hiki,. Jana nilishindwa kukipost kwani nilikuwa nafuatilia kwa undani mambo fulani ili nije na habari kamili.
Baada ya matokeo ya darasa la Saba ya 2011 kutoka yaligubikwa na udanganyifu mkubwa hasa hapa Wilaya ya Mwanga ambayo kwa mara ya kwanza ilikuwa ya kwanza kimkoa ikiipita kwa mbali manispaa ya Moshi huku ikiacha watoto 315 wakifutiwa matokeo hayo.
Jana Tarehe 26/04/2012 walimu hao waliotengeneza mazingira ya udanganyifu walipongezwa kwa kitendo hicho cha kuzalisha wajinga kwa kupelekwa hifadhi ya wanyama ya tarangire.
LEO TAREHE 27/04/2012 SHULE KARIBU ZOTE ZA MSINGI WILAYA YA MWANGA ZIMEFUNGWA. KISA WALIMU WAMECHOKA WAMERUDI USIKU MWINGI SAA 9.00 USIKU WENGINE NDO WANAFIKA SASA HIVI(JIPE).
fedha zilizotumika ni Tsh 48,000,000/= huku usafiri wenyewe ukitekekeza tsh 30,000,0000 ambazo wanalipwa madiwani wenye mabasi hayo (Enea Mrutu, Fihiri Mvungi na Mfanyabiashara Saidi Mssangi wa Sahara coach) huku tenderer ambaye ambaye ameidhinishwa na Tender bodi ya Halamshauri Amiri Mbaga akiwekwa pembeni na tenda hiyo haikutangazwa popote. (WAMEPEANA MADIWANI) kitu ambacho ni kinyume cha sheria madiwani kufanya Biashara na HALMSHAURI WANAZOONGOZA.
Walimu hao ambao waliosafiri jana ni walimu 776 na wao kila siku wanalia kuwa shule hazina Chaki, karatasi na vitendea kazi vingine kama maandalio nk. walimu hao kwa sasa hivi wananunua chaki kwa fedha za mishahara yao. kwani wazazi na wanachi tunajua fika ufisadi unaofanyika Halmashauri hii hivyo hakuna mzazi aliyepo tayari kuchanga.
kinachouma zaidi fedha hizo ni za serikali kwani zimekwapuliwa kutoka fedha za MFUKO WA JIMBO ambazo kazi yake si Entertiment . Fedha hizo ni kwa ajili ya kufanyia miradi mbali mbali ya maendeleo.
kibaya zaidi na madiwani pia wamejiumuishwa kwenye safari hiyo ili kuziba na kuzuiya kabisa mijadala inayoweza kuibuka wakati wananchi tutakapohoji ufisadi huo.
Profesa Maghembe ndiye alikuwa Tour Guide huko tarangire na walichokiona huko ni Mbuni tu. Hii ni safari ya pili kwani ya Kwanza ilfanyika kipindi kile cha ucahaguzi na walimu kuishia kuona Nguchiro tu.
naomba
wiki moja tu iliyopita wabunge wetu waliwashutumu mawaziri kwa ubadhirifu mkubwa akiwemo waziri wa Kilimo ushirika Prof. Maghembe. Lakini wakati huo huo serikali ilikiri rasmi kupitia kwa nwaziri mkuu kuwa imepinda (haina fedha) sasa sikieni kioja hiki,. Jana nilishindwa kukipost kwani nilikuwa nafuatilia kwa undani mambo fulani ili nije na habari kamili.
Baada ya matokeo ya darasa la Saba ya 2011 kutoka yaligubikwa na udanganyifu mkubwa hasa hapa Wilaya ya Mwanga ambayo kwa mara ya kwanza ilikuwa ya kwanza kimkoa ikiipita kwa mbali manispaa ya Moshi huku ikiacha watoto 315 wakifutiwa matokeo hayo.
Jana Tarehe 26/04/2012 walimu hao waliotengeneza mazingira ya udanganyifu walipongezwa kwa kitendo hicho cha kuzalisha wajinga kwa kupelekwa hifadhi ya wanyama ya tarangire.
LEO TAREHE 27/04/2012 SHULE KARIBU ZOTE ZA MSINGI WILAYA YA MWANGA ZIMEFUNGWA. KISA WALIMU WAMECHOKA WAMERUDI USIKU MWINGI SAA 9.00 USIKU WENGINE NDO WANAFIKA SASA HIVI(JIPE).
fedha zilizotumika ni Tsh 48,000,000/= huku usafiri wenyewe ukitekekeza tsh 30,000,0000 ambazo wanalipwa madiwani wenye mabasi hayo (Enea Mrutu, Fihiri Mvungi na Mfanyabiashara Saidi Mssangi wa Sahara coach) huku tenderer ambaye ambaye ameidhinishwa na Tender bodi ya Halamshauri Amiri Mbaga akiwekwa pembeni na tenda hiyo haikutangazwa popote. (WAMEPEANA MADIWANI) kitu ambacho ni kinyume cha sheria madiwani kufanya Biashara na HALMSHAURI WANAZOONGOZA.
Walimu hao ambao waliosafiri jana ni walimu 776 na wao kila siku wanalia kuwa shule hazina Chaki, karatasi na vitendea kazi vingine kama maandalio nk. walimu hao kwa sasa hivi wananunua chaki kwa fedha za mishahara yao. kwani wazazi na wanachi tunajua fika ufisadi unaofanyika Halmashauri hii hivyo hakuna mzazi aliyepo tayari kuchanga.
kinachouma zaidi fedha hizo ni za serikali kwani zimekwapuliwa kutoka fedha za MFUKO WA JIMBO ambazo kazi yake si Entertiment . Fedha hizo ni kwa ajili ya kufanyia miradi mbali mbali ya maendeleo.
kibaya zaidi na madiwani pia wamejiumuishwa kwenye safari hiyo ili kuziba na kuzuiya kabisa mijadala inayoweza kuibuka wakati wananchi tutakapohoji ufisadi huo.
Profesa Maghembe ndiye alikuwa Tour Guide huko tarangire na walichokiona huko ni Mbuni tu. Hii ni safari ya pili kwani ya Kwanza ilfanyika kipindi kile cha ucahaguzi na walimu kuishia kuona Nguchiro tu.
naomba