Jamani hii imekaa vip?

firstcollina

JF-Expert Member
Aug 8, 2009
349
21
Mheshimiwa anapokanusha kauli yake mwenyewe juu ya ongezeko la mishahara kwa 100% kwa wafanyakazi wa kima cha chini.
Wadau naombeni mnieleweshe, maana nahisi sielewi kitu hapa, anapodai alimaanisha ni wafanyakazi wa ndani, mashambani na....... Khaaa!
Hivi wafanyakazi wa kima cha chini ni wapi?!!!!
Kuna nii hapa waungwana hebu tuelimishane. Mbona inasemekana makampuni ya madini yamechimba kibesi juu ya kauli hiyo then ndio...... mambo flani tunayoyaona!​

*****Totaly :target:confused*****
 
huyu Mheshimiwa mbabaishaji wakati anaongea na waandishi wa habari kila jicho lilikuwa likimtizama sasa anaanza kuleta Pumba zake hapa ..viongozi wetu wamekaa kitaperi tu
 
Kinachoshangaza zaidi endapo hiyo mishahara ya wafanyakazi wa ndani itapanda kwa 100%,hivi wenzangu wa serikalini wenye kima cha chini na wanawafanyakazi wa ndani si tutakuwa tunagawana nusu kwa nusu na wafanyakazi wetu wa ndani??
na hapo kumbuka natakiwa kutoa pesa ya nauli na chakula ambacho na huyo mfanyakazi atatumia.....aisee hii haijakaa vizuri hata kidogo.​
 
Back
Top Bottom