Jaji Samata akiri katiba iliyopo ina mapungufu makubwa

Nimemwona nikajiuliza kama magamba nao wamesikiliza. Maana tukisema sisi tunaambiwa ni cdm! Kwani cdm si watu.
Wote tunakumbuka udikteta wa ma dc na ma rc. Tuliona walimu wakichapwa viboko. Tunaona rc Arusha akilazimisha bendera za cdm zishushwe kwenye matawi ya chama huko Arumeru! Tumemsikia Mbunge akilalamika dc kuingia kwenye boma na kuchukua mbuzi na ng'ombe kama wake. Huu udikteta unalindwa na katiba. Halafu tunaletewa mswada unaomwongezea rais udikteta! Tukikataa kuujadili, bunge linageuka "lango la jiji"

Acha watutukane wanavyotaka, watudharau, watudhalilishe, lakini hoja ya msingi inabaki palepale, Hatuutaki huo mswada!

we waache waendelee kuchanja chale kwenye kidonda kibichi....wanadhani sisi ni wajinga sana na watu wa kuburuzwa tu...tutawaonyesha waa wasidhani wanalofanya ni sahihi
 
Kwakweli hata Mimi Judge Samatta kanifurahisha sana kwa points alizozitoa,ila kuna jamaa ni MKULIMA,amesema anashangaa WABUNGE wa CCM badala ya kujikita ktk hoja wao Tundu Lissu mara Kibanda kana kwamba hao watu ndio muswada uliokua unajadiliwa.Poor CCM,

paka aliyezoea kula jalalani hawezi kula kwenye sahani... wabunge wengi ni wajinga sana na hawajui wanalosema na kutetea na ndio maana hawana hoja kuhusu mswaada huo kazi ni kumshambulia lissu na chadema....mkuu wa kaya aangalie ana na wala asidhani sisi ni wajinga
 
Huyu jaji ana hasira na CCM kwasababu walimtosa mwanawe kwenye viti maalum. Hana chochote huyu ni wa kumpuuzia tu.
 
Hata Magamba wanayasikia, wanayajua na kuyaona haya mambo vizuri sana tu, ila wanajifanya viziwi na vipofu kwa makusudi tu. Ila nao siku zao zinahesabika. Yani unakuta mbunge anachanhia mada kwa kuunga mkono hata haina maslahi kwa taifa ili mradi imeletwa na chama chake, ama ni wa chama kinachotawala basi hoja imeletwa na serikali. upumbavu mtupu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
leo jaji mstaafu barnabas samatta amefunguka na kudai kuwa katiba ya sasa inamapungufu makubwa na inawapa baadhi ya watu madaraka makubwa ambayo yanawafanya kuwa madikteta. Mambo aliyogusia ni pamoja na
1. Raisi kuwa na madaraka makubwa katika katiba
2. Tume ya uchaguzi kuwa idara ndani ya serikali kitu ambacho kinaifanya kutokuwa huru
3. Spika wa bunge kutoka kwenye chama cha siasa kitu ambacho kinamfanya kuonyesha upendeleo wa dhairi.
Mwisho hakasema mchakato wa kwenda kwenye katiba mpya lazima uwe wa uhuru na amani na kila mwananchi ashirikishwe.
Mytake.
Haya maoni ambayo yanatolewa na watu maarufu kama magamba hawatayasikia basi lakuvunda halina ubani.
Source.itv news

Hiyo ndiyo njia sahihi ya kutoa maoni na wala si kutoka nje watu wanashindwa kutofautisha nani chizi
 
Nimemwona nikajiuliza kama magamba nao wamesikiliza. Maana tukisema sisi tunaambiwa ni cdm! Kwani cdm si watu.
Wote tunakumbuka udikteta wa ma dc na ma rc. Tuliona walimu wakichapwa viboko. Tunaona rc Arusha akilazimisha bendera za cdm zishushwe kwenye matawi ya chama huko Arumeru! Tumemsikia Mbunge akilalamika dc kuingia kwenye boma na kuchukua mbuzi na ng'ombe kama wake. Huu udikteta unalindwa na katiba. Halafu tunaletewa mswada unaomwongezea rais udikteta! Tukikataa kuujadili, bunge linageuka "lango la jiji"

Acha watutukane wanavyotaka, watudharau, watudhalilishe, lakini hoja ya msingi inabaki palepale, Hatuutaki huo mswada!

Nimeona sehemu fulani umesema mbunge wako ni G. Lema, lakini nikaona Lema amekuathiri sana hasa kwenye paragrafu ya mwisho.
 
Huyu jaji mnafiki, mbona wakati akiwa kazini hakulisema hili wakati alikuwa na madaraka

mpapai, nafikili kila jambo na wakati wake, Samata alikuwa jaji mkuu kipindi ambacho mahitaji ya katiba mpya hayakuwa makubwa kama ilivyo sasa, pia hakukuwa na matumizi mabaya ya madaraka kama lilivyo sasa. Jaji msitaafu SAMATA mfano mzuri wa aina ya viogozi, walezi na waelekezaji tunaowahitaji kwa usitawi wa taifa letu.
 
Huyu jaji ana hasira na CCM kwasababu walimtosa mwanawe kwenye viti maalum. Hana chochote huyu ni wa kumpuuzia tu.
Kwa hiyo hayo aliyoyasema yana uhusiano na mwanae kupigwa chini ubunge wa viti maalumu? Mwita 25 kama utashindwa kuelewa alichoongea Samata basi tena subiri miujiza toka CCM.
 
Huyu jaji ana hasira na CCM kwasababu walimtosa mwanawe kwenye viti maalum. Hana chochote huyu ni wa kumpuuzia tu.

sidhani kama hii argument yako ina ukweli wowote. Uongozi wa Jaji Samatta ulikuwa mzuri kulinganisha na hao wengine. Jaji samatta ndie Jaji mkuu ambaye baada yakuingia madarakani; kesi nyingi ambazo watu walifungua kushtaki serikali zilisikilizwa na serikali ikaanguka vibaya. In other words, aliacha sheria ishike mkondo wake na likataa kuingiliwa kwenye kazi yake. Rejea kesi za uchaguzi wakati huo, kesi ya yule wakili aliyeishtaki serikali nakulipwa fidia, rejea mahakimu walioondolewa baada ya kukamatwa kula rushwa, . Marehemu Jaji Nyalali alizibana sana kesi zilizogusa serikali; alipostaafu kila kitu kikawekwa wazi na Jaji Samatta. Long live Samatta. Hakuwahi kuwa popular sana kwasababu serikali haikumpenda kivile. Laiti wananchi wangetambua hilo!
 
Huyu jaji ana hasira na CCM kwasababu walimtosa mwanawe kwenye viti maalum. Hana chochote huyu ni wa kumpuuzia tu.

Mtu akisema ukweli wake anaambiwa ana gubu. Ndiyo maana Sungura alisema "Sizitaki mbichi hizi." kwani asiyetaka kuambiwa ukweli visingizio kwake ni vingi.
 
Mtu akisema ukweli wake anaambiwa ana gubu. Ndiyo maana Sungura alisema "Sizitaki mbichi hizi." kwani asiyetaka kuambiwa ukweli visingizio kwake ni vingi.

Miafrika ndivyo tulivyo, huwa tunasubiri hadi tutoke madarakani ndiyo tunajifanya kuipinga serikali. Ni juzi tu nimetoka kumsikia 'former' IGP Omar Mahita akiuponda uongozi wa JK kupitia Radio Abood FM. Watu wakaanza kumsifia sana Mahita na kusahau madudu yake yote.
 
Huyu jaji ana hasira na CCM kwasababu walimtosa mwanawe kwenye viti maalum. Hana chochote huyu ni wa kumpuuzia tu.

Mwita25 Jaji Barnabas Samata amestaafu kwa heshima siyo kama Jaji Agustino Ramadhan aliyestaafu kichwa chini baada ya kulikoroga na hukumu ya mgombea binafsi. Nakumbuka kama siyo mwaka jana basi ni mwaka juzi,Jaji Samata alitoa mhadhara wa wazi huko SAUT-Ruhaha Iringa ambao ulikua ni mzuri sana na aliishangaa Mahakama kukataa mgombea binafsi. Yawezekana maneno yake hayakuwafurahisha watawala pengine ndiyo maana walikata jina la bint yake(ingawa sijui kama bint yake aligombea ubunge kweli)
 
Huyu jaji mnafiki, mbona wakati akiwa kazini hakulisema hili wakati alikuwa na madaraka

Go read about Mr Justice Samatta, he will be remembered in this country for what he did in dispensation of justice. He is an icon in legal fraternity, no one like him. Hajawahi kuwa mnafiki huyu bwana hata siku moja, hata dakika moja
 
Miafrika ndivyo tulivyo, huwa tunasubiri hadi tutoke madarakani ndiyo tunajifanya kuipinga serikali. Ni juzi tu nimetoka kumsikia 'former' IGP Omar Mahita akiuponda uongozi wa JK kupitia Radio Abood FM. Watu wakaanza kumsifia sana Mahita na kusahau madudu yake yote.
Mahita hakuwa mzalendo na dhambi ya usaliti ndiyo inayomsumbua. Jaji Samata hakuwa msaliti na hakutumika kama kopo la chooni kulitumia na kuliacha huko huko.
 
Mtu akisema ukweli wake anaambiwa ana gubu. Ndiyo maana Sungura alisema "Sizitaki mbichi hizi." kwani asiyetaka kuambiwa ukweli visingizio kwake ni vingi.
Umenena kweli, ngoja tusikie wanayoambiwa wazee wa Dar kama yatakuwa tofauti na michango ya wabunge .
 
Back
Top Bottom