Patriote
JF-Expert Member
- Jul 13, 2011
- 1,718
- 1,047
MWENYEKITI mpya wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), Jaji mstaafu Damian Lubuva, amesema katika utekelezaji wa majukumu yake watu wasitegemee mapya kutokana na mfumo uliopo kumtaka aendeleze yaliyokuwa yakifanywa na mtangulizi wake, Jaji Lewis Makame.
Jaji Lubuva alisema hayo muda mfupi baada ya kuapishwa Ikulu Dar es Salaam na Rais Jakaya Kikwete.
Alisema Rais Kikwete alipompa taarifa ya uteuzi wake, alisita kuchukua nafasi hiyo kwa sababu ina changamoto nyingi hasa kipindi hiki cha mchakato wa mabadiliko ya katiba.
"Nimekuwapo kwenye utumishi wa umma kama jaji kwa muda mrefu, lakini niliposikia uteuzi huu nilisita kwa kuwa ni kipindi kigumu hiki cha sasa. Hata hivyo, nilikubali nafasi hiyo baada ya kutafakari," alisema Jaji Lubuva.
Alisema kutokana na mfumo uliopo hana jipya, ila ataendeleza pale Jaji Makame alipoachia mpaka mfumo huo utakapobadilika."Tutaendeleza shughuli za tume kama ilivyo na kuboresha daftari la wapigakura kuanzia sasa ili kuondoa malalamiko," alisema.
Jaji Lubuva alisema atahakikisha hapendelei chama chochote katika uchaguzi wowote utakaofanyika, hivyo vijiandae kufanya uchaguzi huru na haki.
Mkurugenzi wa Uchaguzi, Julius Malaba, ambaye naye aliapishwa jana alisema anajua Nec kuna changamoto nyingi, lakini atapambana nazo ili kufanya kazi kwa ufanisi."Ninajua kuna changamoto nyingi na hatutapendelea kama tulivyoapa pale," alisema Malaba.Mwingine aliyeapisha jana ni Makamu Mwenyekiti wa Nec, Hamid Mahmoud Hamid.
Source: Mwananchi
Maoni yangu
Tunapohitaji Rais ateue watu wenye mawazo mapya, lengo letu linakuwa ni kuachana na utamaduni wa kuteua watu wasio innovative na wanaofanyakazi kwa mazoea kama hawa wastaafu wetu ambao kila kukicha Rais anaendelea kuwateua. Hivi kama hawa wastaafu wangekuwa ni potential si tungewasikia wakati wa utumishi wao kabla hawajastaafu???Kwann tunapewa watu waliochoka fikra na mawazo na wanaokuja kula fedha za walipa kodi bila ya kuwa na significant contribution kwa taifa letu?? Kuna ugumu gani kwa m/kiti wa tume ua uchaguzi kuongoza mabadiliko ya huo anaouita mfumo uliopo???Huo mfumo kauweka nani had usibadilike??Kama hawezi kazi ni kipi kilimfanya aikubali???Hizi njaa jamani zitawacost!!!
Lubuva anasema waziwazi tena bila aibu kuwa tusitegemee jipya, hivi kwa kauli hiyo anataka kuwaambia nini watanzania?? Tena anasema ataendeleza yale yaloyaliyoachwa na mtangulizi wake, Lewis Makame, Hivi Lewis Makame alifanya yapi mazuri zaidi ya kutuletea utata katika chaguzi zetu???Ni utendaji mbovu wa Tume ya uchaguzi chini ya Makame umekuwa ukilalamikiwa kila uchaguzi, Ni mfumo mbovu wa uchaguzi chini ya Makame unaoshindwa hata kutangaza idadi kamili za wapiga kura kila uchaguzi ktk kata na majimbo. Huu mwaka naona umeanza vibaya!!!!
KAMA LUBUVA UNAFIKIRIA KUENDESHA HIYO OFISI KWA MAZOEA NA KWA KUENDELEZA YALE ALIYOYAACHA MAKAME, TEGEMEA YALIYOMKUTA KIVUITU WA TUME YA UCHAGUZI WA KENYA. USIFIKIRIE KWAMBA TUTAENDELEA KUWA WAJINGA SIKU ZOTE.
Jaji Lubuva alisema hayo muda mfupi baada ya kuapishwa Ikulu Dar es Salaam na Rais Jakaya Kikwete.
Alisema Rais Kikwete alipompa taarifa ya uteuzi wake, alisita kuchukua nafasi hiyo kwa sababu ina changamoto nyingi hasa kipindi hiki cha mchakato wa mabadiliko ya katiba.
"Nimekuwapo kwenye utumishi wa umma kama jaji kwa muda mrefu, lakini niliposikia uteuzi huu nilisita kwa kuwa ni kipindi kigumu hiki cha sasa. Hata hivyo, nilikubali nafasi hiyo baada ya kutafakari," alisema Jaji Lubuva.
Alisema kutokana na mfumo uliopo hana jipya, ila ataendeleza pale Jaji Makame alipoachia mpaka mfumo huo utakapobadilika."Tutaendeleza shughuli za tume kama ilivyo na kuboresha daftari la wapigakura kuanzia sasa ili kuondoa malalamiko," alisema.
Jaji Lubuva alisema atahakikisha hapendelei chama chochote katika uchaguzi wowote utakaofanyika, hivyo vijiandae kufanya uchaguzi huru na haki.
Mkurugenzi wa Uchaguzi, Julius Malaba, ambaye naye aliapishwa jana alisema anajua Nec kuna changamoto nyingi, lakini atapambana nazo ili kufanya kazi kwa ufanisi."Ninajua kuna changamoto nyingi na hatutapendelea kama tulivyoapa pale," alisema Malaba.Mwingine aliyeapisha jana ni Makamu Mwenyekiti wa Nec, Hamid Mahmoud Hamid.
Source: Mwananchi
Maoni yangu
Tunapohitaji Rais ateue watu wenye mawazo mapya, lengo letu linakuwa ni kuachana na utamaduni wa kuteua watu wasio innovative na wanaofanyakazi kwa mazoea kama hawa wastaafu wetu ambao kila kukicha Rais anaendelea kuwateua. Hivi kama hawa wastaafu wangekuwa ni potential si tungewasikia wakati wa utumishi wao kabla hawajastaafu???Kwann tunapewa watu waliochoka fikra na mawazo na wanaokuja kula fedha za walipa kodi bila ya kuwa na significant contribution kwa taifa letu?? Kuna ugumu gani kwa m/kiti wa tume ua uchaguzi kuongoza mabadiliko ya huo anaouita mfumo uliopo???Huo mfumo kauweka nani had usibadilike??Kama hawezi kazi ni kipi kilimfanya aikubali???Hizi njaa jamani zitawacost!!!
Lubuva anasema waziwazi tena bila aibu kuwa tusitegemee jipya, hivi kwa kauli hiyo anataka kuwaambia nini watanzania?? Tena anasema ataendeleza yale yaloyaliyoachwa na mtangulizi wake, Lewis Makame, Hivi Lewis Makame alifanya yapi mazuri zaidi ya kutuletea utata katika chaguzi zetu???Ni utendaji mbovu wa Tume ya uchaguzi chini ya Makame umekuwa ukilalamikiwa kila uchaguzi, Ni mfumo mbovu wa uchaguzi chini ya Makame unaoshindwa hata kutangaza idadi kamili za wapiga kura kila uchaguzi ktk kata na majimbo. Huu mwaka naona umeanza vibaya!!!!
KAMA LUBUVA UNAFIKIRIA KUENDESHA HIYO OFISI KWA MAZOEA NA KWA KUENDELEZA YALE ALIYOYAACHA MAKAME, TEGEMEA YALIYOMKUTA KIVUITU WA TUME YA UCHAGUZI WA KENYA. USIFIKIRIE KWAMBA TUTAENDELEA KUWA WAJINGA SIKU ZOTE.