Jaji kesi ya Lema Arusha kashikishwa kitu na mafisadi?

SOMENI HAPA


WAKATI Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kikiwa na furaha ya ushindi wa ubunge kilioupata katika jimbo la Arumeru Mashariki, furaha hiyo huenda ikaingia dosari endapo Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Arusha, itamwona na hatia mbunge wake, Godbless Lema.

Lema ambaye ni mmoja kati ya wabunge maarufu wa CHADEMA, anakabiliwa na kesi ya kupinga matokeo yake ya ubunge, iliyofunguliwa na baadhi ya makada wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Katika majumuisho ya utetezi wake, Lema ameomba shauri hilo litupiliwe mbali kwani madai dhidi yake ni uongo ndiyo maana Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowasa na Dk. Batilda Burian, waliodaiwa kukashfiwa hawakufika mahakamini kutoa ushahidi kukanusha au kuthibitisha maneno yaliyotamkwa dhidi yao.

Kupitia kwa wakili wake, Method Kimomogoro, Lema alidai iwapo kweli angetamka maneno ya kashfa, matusi na udhalilishaji dhidi ya Dk. Burian angefika mahakamani kama mlalamikaji au shahidi lakini hakufanya hivyo licha ya kupewa taarifa na walalamikaji katika shauri hilo baada ya kubaini ukweli kuwa hakuwahi kutamka maneno hayo.
"Wadai na mashahidi wao wameieleza mahakama kuwa miongoni mwa maneno yanayodaiwa kutamkwa na Lema ni uhusiano wa kingono kati ya Mheshimiwa Lowasa na Dk. Burian, lakini siyo Lowasa wala Dk. Burian aliyefika hapa mahakamani kuthibitisha au kukanusha uhusiano wao nje ya ndoa kati yao," alidai Wakili Kimomogoro.

Alidai hata mume wa Dk. Burian ambaye sasa ni Balozi wa Tanzania nchini Kenya akiwakilisha nchi za Pembe ya Afrika naye hakufika mahakamani kukanusha au kuthibitisha iwapo mtoto ambaye Lema anadaiwa kusema alizaliwa nje ya ndoa ni wa kwake au kueleza iwapo mimba aliyodaiwa kuwa nayo waziri huyo wa zamani ilikuwa yake.

Katika hati yake ya hoja za majumuisho, Wakili Kimomogoro alidai kitendo cha wote waliotajwa au kuguswa na ushahidi wa wadai na mashahidi wao kutofika mahakamani kutoa ushahidi kuthibitisha au kukanusha kinadhihirisha maneno yanayodaiwa kusemwa na mteja wake hayakuwahi kutamkwa na kuiomba mahakama kutupilia mbali shauri hilo.
Pamoja na kutupa shauri hilo, Kimomogoro pia aliiomba mahakama kuwaamuru wadai kulipa gharama zote ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia ya kufungua kesi za uongo.

Wadai katika shauri hilo namba 13/2010 ni Mussa Mkanga, Agnes Mollel na Happy Kivuyo ambao wanawakilishwa na mawakili, Alute Mughwai na Modest Akida wakati Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni mdaiwa wa pili akiwakilishwa na mawakili, Timon Vitalis, na Juma Masanja.

Kimomogoro alidai kuwa hata ushahidi wa mashahidi wote 14 wa walalamikaji umejikita katika maelezo ya mdomo bila kuongezewa uzito kwa vielelezo ikiwemo maandishi, magazeti au CD zenye kumwonyesha Lema akitoa kauli anazodaiwa kutoa kwenye mikutano yake ya kampeni ambayo wadai walieleza wanazo katika hati yao ya madai iliyoko mahakamani.

Alidai licha ya kushindwa kuwasilisha vielelezo kuthibitisha madai yao, wadai pamoja na mashahidi wao 14 waliofika mahakamani wametofautiana katika ushahidi wao kwenye mambo ya msingi yanayohusu tukio au jambo moja.
Alitoa mfano wa kutofautiana kwa shahidi wa tatu, Happy Kivuyo aliyedai kuvuliwa cheo cha katibu mwenezi wa CCM, kata ya Sokon I mwaka 2010 wakati shahidi wa nne, Salum Mpamba, aliyekuwa katibu wa CCM wilaya ya Arusha kipindi cha uchaguzi mkuu aliieleza mahakama kuwa alipohamishiwa wilaya ya Kyela Machi mwaka jana alimwacha Kivuyo akishikilia wadhifa huo.
Alidai ushahidi wa kimazingira unaonyesha kuwa Lema asingeweza kupuuza uwezo wa wanawake kiuongozi kwa sababu chama chake cha CHADEMA kilisimamisha wanawake wengi kugombea ubunge na udiwani sehemu mbalimbali nchini huku timu yake ya kampeni ikiwa na wanawake ambao alikuwa akiwanadi na kuwaombea kura.

"Wadai na mashahidi wao wameithibitishia mahakama katika ushahidi wao kuwa Lema alikuwa akiongozana na wagombea udiwani wanawake kupitia chama chake kwenye mikutano yake ya kampeni, hivyo isingekuwa rahisi yeye kusema Dk. Burian asichaguliwe kwa sababu ni mwanamke halafu papo hapo awaombee kura za udiwani wanawake wa chama chake," alidai Kimomogoro.

Kuhusu ubaguzi wa kidini na kikabila, wakili huyo alidai isingekuwa rahisi maneno ya kibaguzi kiimani na kikabila kutolewa na mgombea kwenye mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na watu wa dini na makabila mbalimbali.
Kwa upande wake wakili wa walalamikaji, Mughwai alipinga hoja ya kuwaleta Kimomogoro ya kushindwa kuwaleta mahakamani hapo Dk. Burian na Lowassa kwa madai kuwa Lema ndiye alipaswa kuwaleta mahakamani hapo kwani ndiye aliyeibua suala hilo.

Naye wakili wa serikali, Timon Vitalis, iliiomba mahakama kutupilia mbali madai hayo akidai kisheria mgombea kuelezea tofauti yake ya ukaazi na mgombea mwenzake hakuwezi kutafsiriwa kama kashfa, matusi wala udhalilishaji kwa sababu hiyo ni moja kati ya sifa anayotakiwa kuwa nayo kiongozi anayeomba kuongoza watu.

Vitalis alidai kuzuia wagombea kujinadai kwa tofauti zao kimakaazi ni sawa na kuwanyima kutaja sifa zao za kuchaguliwa na kusisitiza kuwa hata sheria ya uchaguzi haitaji kauli kuhusu ukaazi kama moja ya makosa kwenye kampeni za uchaguzi.

Akihitimisha hoja zake, wakili Kimomogoro anadai mlalamikaji wa kwanza, Mussa Mkanga, ndiye aliyeamua kutunga madai ya uongo dhidi ya Lema na kuwashirikisha wenzake kwa nia ya kulipa kisasi cha mbunge huyo kusababisha ajiuzulu nafasi yake ya udiwani kata ya Sombetini mwaka 2006.

Jaji Rwakibarila ambaye alijizolea sifa kutokana na aina yake ya uendeshaji wa shauri hilo anatarajiwa kusoma hukumu yake kesho kuanzia majira ya saa 3 asubuhi ambapo wasikilizaji wametakiwa kuingia kwenye chumba cha mahakama saa 2:30 asubuhi.
 
WAKATI Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kikiwa na furaha ya ushindi wa ubunge kilioupata katika jimbo la Arumeru Mashariki, furaha hiyo huenda ikaingia dosari endapo Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Arusha, itamwona na hatia mbunge wake, Godbless Lema.

Lema ambaye ni mmoja kati ya wabunge maarufu wa CHADEMA, anakabiliwa na kesi ya kupinga matokeo yake ya ubunge, iliyofunguliwa na baadhi ya makada wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Katika majumuisho ya utetezi wake, Lema ameomba shauri hilo litupiliwe mbali kwani madai dhidi yake ni uongo ndiyo maana Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowasa na Dk. Batilda Burian, waliodaiwa kukashfiwa hawakufika mahakamini kutoa ushahidi kukanusha au kuthibitisha maneno yaliyotamkwa dhidi yao.

Kupitia kwa wakili wake, Method Kimomogoro, Lema alidai iwapo kweli angetamka maneno ya kashfa, matusi na udhalilishaji dhidi ya Dk. Burian angefika mahakamani kama mlalamikaji au shahidi lakini hakufanya hivyo licha ya kupewa taarifa na walalamikaji katika shauri hilo baada ya kubaini ukweli kuwa hakuwahi kutamka maneno hayo.
"Wadai na mashahidi wao wameieleza mahakama kuwa miongoni mwa maneno yanayodaiwa kutamkwa na Lema ni uhusiano wa kingono kati ya Mheshimiwa Lowasa na Dk. Burian, lakini siyo Lowasa wala Dk. Burian aliyefika hapa mahakamani kuthibitisha au kukanusha uhusiano wao nje ya ndoa kati yao," alidai Wakili Kimomogoro.

Alidai hata mume wa Dk. Burian ambaye sasa ni Balozi wa Tanzania nchini Kenya akiwakilisha nchi za Pembe ya Afrika naye hakufika mahakamani kukanusha au kuthibitisha iwapo mtoto ambaye Lema anadaiwa kusema alizaliwa nje ya ndoa ni wa kwake au kueleza iwapo mimba aliyodaiwa kuwa nayo waziri huyo wa zamani ilikuwa yake.

Katika hati yake ya hoja za majumuisho, Wakili Kimomogoro alidai kitendo cha wote waliotajwa au kuguswa na ushahidi wa wadai na mashahidi wao kutofika mahakamani kutoa ushahidi kuthibitisha au kukanusha kinadhihirisha maneno yanayodaiwa kusemwa na mteja wake hayakuwahi kutamkwa na kuiomba mahakama kutupilia mbali shauri hilo.
Pamoja na kutupa shauri hilo, Kimomogoro pia aliiomba mahakama kuwaamuru wadai kulipa gharama zote ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia ya kufungua kesi za uongo.

Wadai katika shauri hilo namba 13/2010 ni Mussa Mkanga, Agnes Mollel na Happy Kivuyo ambao wanawakilishwa na mawakili, Alute Mughwai na Modest Akida wakati Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni mdaiwa wa pili akiwakilishwa na mawakili, Timon Vitalis, na Juma Masanja.

Kimomogoro alidai kuwa hata ushahidi wa mashahidi wote 14 wa walalamikaji umejikita katika maelezo ya mdomo bila kuongezewa uzito kwa vielelezo ikiwemo maandishi, magazeti au CD zenye kumwonyesha Lema akitoa kauli anazodaiwa kutoa kwenye mikutano yake ya kampeni ambayo wadai walieleza wanazo katika hati yao ya madai iliyoko mahakamani.

Alidai licha ya kushindwa kuwasilisha vielelezo kuthibitisha madai yao, wadai pamoja na mashahidi wao 14 waliofika mahakamani wametofautiana katika ushahidi wao kwenye mambo ya msingi yanayohusu tukio au jambo moja.
Alitoa mfano wa kutofautiana kwa shahidi wa tatu, Happy Kivuyo aliyedai kuvuliwa cheo cha katibu mwenezi wa CCM, kata ya Sokon I mwaka 2010 wakati shahidi wa nne, Salum Mpamba, aliyekuwa katibu wa CCM wilaya ya Arusha kipindi cha uchaguzi mkuu aliieleza mahakama kuwa alipohamishiwa wilaya ya Kyela Machi mwaka jana alimwacha Kivuyo akishikilia wadhifa huo.
Alidai ushahidi wa kimazingira unaonyesha kuwa Lema asingeweza kupuuza uwezo wa wanawake kiuongozi kwa sababu chama chake cha CHADEMA kilisimamisha wanawake wengi kugombea ubunge na udiwani sehemu mbalimbali nchini huku timu yake ya kampeni ikiwa na wanawake ambao alikuwa akiwanadi na kuwaombea kura.

"Wadai na mashahidi wao wameithibitishia mahakama katika ushahidi wao kuwa Lema alikuwa akiongozana na wagombea udiwani wanawake kupitia chama chake kwenye mikutano yake ya kampeni, hivyo isingekuwa rahisi yeye kusema Dk. Burian asichaguliwe kwa sababu ni mwanamke halafu papo hapo awaombee kura za udiwani wanawake wa chama chake," alidai Kimomogoro.

Kuhusu ubaguzi wa kidini na kikabila, wakili huyo alidai isingekuwa rahisi maneno ya kibaguzi kiimani na kikabila kutolewa na mgombea kwenye mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na watu wa dini na makabila mbalimbali.
Kwa upande wake wakili wa walalamikaji, Mughwai alipinga hoja ya kuwaleta Kimomogoro ya kushindwa kuwaleta mahakamani hapo Dk. Burian na Lowassa kwa madai kuwa Lema ndiye alipaswa kuwaleta mahakamani hapo kwani ndiye aliyeibua suala hilo.

Naye wakili wa serikali, Timon Vitalis, iliiomba mahakama kutupilia mbali madai hayo akidai kisheria mgombea kuelezea tofauti yake ya ukaazi na mgombea mwenzake hakuwezi kutafsiriwa kama kashfa, matusi wala udhalilishaji kwa sababu hiyo ni moja kati ya sifa anayotakiwa kuwa nayo kiongozi anayeomba kuongoza watu.

Vitalis alidai kuzuia wagombea kujinadai kwa tofauti zao kimakaazi ni sawa na kuwanyima kutaja sifa zao za kuchaguliwa na kusisitiza kuwa hata sheria ya uchaguzi haitaji kauli kuhusu ukaazi kama moja ya makosa kwenye kampeni za uchaguzi.

Akihitimisha hoja zake, wakili Kimomogoro anadai mlalamikaji wa kwanza, Mussa Mkanga, ndiye aliyeamua kutunga madai ya uongo dhidi ya Lema na kuwashirikisha wenzake kwa nia ya kulipa kisasi cha mbunge huyo kusababisha ajiuzulu nafasi yake ya udiwani kata ya Sombetini mwaka 2006.

Jaji Rwakibarila ambaye alijizolea sifa kutokana na aina yake ya uendeshaji wa shauri hilo anatarajiwa kusoma hukumu yake kesho kuanzia majira ya saa 3 asubuhi ambapo wasikilizaji wametakiwa kuingia kwenye chumba cha mahakama saa 2:30 asubuhi.

Source: Tanzania Daima


Nadhani hapo kwenye red Mahakama husika ni Mahakama kuu.
 
Kama kweli kuna mkono wa mafisadi hiyo kesi.....kazi ni kubwa na nawahakikishia kuwa tutashinda....TULIANZA NA MUNGU NA TUTAMALIZA NA MUNGU 2015, wanofikiri kuwa ni nguvu ya soda, IMEKULA KWAO.....
 
Anguko la mkwewe Arumeru mashariki linaonyesha ni jinsi gani ENL alivyoishiwa... Lema sio saizi yake
 
Ni nani kakwambia uchaguzi ukirudiwa CCM itashinda? Hata bila Lema CHADEMA itapeta tuu


Hakuna kitu, Kesho Lema pigwa chiniiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii, SUBIRINI MTAONA
 
hakuna atakaepigwa chini,kwanza ni garama kurudia uchaguzi,pile usindi wa Lema ni wa halali
hakuna ushahidi wa kuonyesha alihusika ktk wizi wa kura,CCM walishindwa kihalali
kama ni matusi hata CCM ni mabingwa na walitukana sana wkt wa kampeni
ntamwona huyo jaji kama kilaza wa kutupwa kama atasema kesi imethibitishwa pasi na mashaka
Lingine huyo jaji atakuwa mjinga kama hatajali maisha yake kwa kukubali vijisent vitakavomdhalilisha na kumweka ktk hali ya wasiwasi ktk maisha yake
KUWENI NA IMANI KWA MAHAKAMA NA ENDAPO LEMA ATANGOLEWA BADO KUNA RUFAA YA KUTENGUA KESI IKIFIKA MAHAKAMA YA RUFAA KWA KWELI LAZIMA HAKI ITENDEKE,MAJAJI WENGI WA MAHAKAMA KUU WALIPEWA KWA KWA KUJUANA NA WENGINE HAWAKUWA KTK TASNIA YA MAHAKAMA WALIBEBWA WALIPOKUWAKO WAKAPACHIKWA
Ila kwa hili la arusha mtashuhudia wenyewe haki itatendekea Lema atabaki kuwa kamanda na mbunge
 
Hii kesi inabeba ujumbe mzito kuelekea 2015. Kama Judge akitengua ushindi wa Lema kwa Ushahidi ule dhaifu uliotolewa mahakamani basi ni dhahiri kuwa Mahakama itakuwa imekosa Legitimacy ya kutoa haki na hapo ndipo tutakaposhuhudia 2015 wananchi wakitoa hukumu wenyewe pale tu watakapoona wamedhulumiwa katika Chaguzi. Precedence yake ni mbaya zaidi ya Judge kuhongwa Millioni 500. Itatu-cost wote yaani CCM, CDM na tusiokuwa na chama.

Judge hawezi kutengua matokeo ya uchaguzi kama mchakato wa upigaji kura na kuhesabu kura na kutangaza matokeo hakukuwa na kasoro za kuonesha kuwa matokeo yaliyotangazwa yanampatia ushindi mtu aliyekuwa ameshindwa. Kuhusu ni jinsi gani wagombea wameshawishi wapiga kura hilo ni suala jingine kabisa, kama mgombea katoa kashfa mkashfiwa ana haki ya kufungua civil case, na kama ni rushwa basi TAKUKURU wanatakiwa ku-prosecute kesi hiyo.

Hii kesi ni slam dunk kwa judge yeyote yule, baada ya kusikiliza pande zote mbili yaani upande wa wapuuzi na upande wa walalamikiwa, judge atakuwa ameridhisha pande zote na kutupilia mbali kesi hii. Hii kesi haina masilahi kwa CCM tena, maana uchaguzi wowote mdogo ni njia bora zaidi ya kukiimarisha CDM kwani inaongeza enthusiasm - Great excitement kwa wapenda mabadiliko. I hope hii habari ya Judge kuhongwa si kweli, maana inalifanya taifa kuwa katika law of the jungle. Nina imani na mahakimu wetu hasa katika kesi zenye national interest kama hizi.
 
Hakuna kitu, Kesho Lema pigwa chiniiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii, SUBIRINI MTAONA

Arumeru mlisema hivi hivi alafu mkadondokea kiuno.
Hivi unadhani mahakama ni choo cha stand???
 
Hakuna kitu, Kesho Lema pigwa chiniiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii, SUBIRINI MTAONA

hata arumeru mlituambia sioi lazima atashida, tumewazoea.
 
Back
Top Bottom