Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Wana-JF:
Kesho (Ijumaa), kituo cha televisheni cha ITV katika kipindi chake cha Kipima Joto saa 3 usiku, mada kuu itakuwa ni Sheria ya Matumizi ya Fedha katika kampeni iliyotiwa saini na JK April mwaka huu.
Ni sheria ambayo tayari imeanza kuwekwa majaribuni na iwapo makali yake au la yanaweza kujulikana wiki ijayo kutokana na maamuzi ya Msajili wa Vyama katika pingamizi la Chadema dhidi ya JK.
Mimi sipingi kwa ITV kufanya mjadala huo ambao wananchi pia wamearifiwa kuchangia kwa simu, ila nina wasiwasi wa timing ya kipindi hicho wakati huu ambapo maamuzi ya Tendwa yanasubiriwa.
Sote tumeshajua ule upande ITV unaegemea katika kampeni hizi (CCM) na hofu yangu ni kwamba pengine kipindi hicho kimeandaliwa maalum katika ku-influence maamuzi ya Msajili wa Vyama katika pingamizi hilo la kihistoiria.
Nina maana hapa ingawa mada ni Sheria hiyo yote kwa ujumla, lakini ni dhahihiri watakaojadili hawataacha kutia mkazo katika hilo pingamizi. Hivyo watoa mada wanaweza kuwa wameandaliwa ili ku-influence uamuzi. Hawa ni pamoja na wale "watakaopiga simu."
Ingefaa kipindi hiki kingeahirishwa hadi baada ya ruling ya Tendwa.
Kesho (Ijumaa), kituo cha televisheni cha ITV katika kipindi chake cha Kipima Joto saa 3 usiku, mada kuu itakuwa ni Sheria ya Matumizi ya Fedha katika kampeni iliyotiwa saini na JK April mwaka huu.
Ni sheria ambayo tayari imeanza kuwekwa majaribuni na iwapo makali yake au la yanaweza kujulikana wiki ijayo kutokana na maamuzi ya Msajili wa Vyama katika pingamizi la Chadema dhidi ya JK.
Mimi sipingi kwa ITV kufanya mjadala huo ambao wananchi pia wamearifiwa kuchangia kwa simu, ila nina wasiwasi wa timing ya kipindi hicho wakati huu ambapo maamuzi ya Tendwa yanasubiriwa.
Sote tumeshajua ule upande ITV unaegemea katika kampeni hizi (CCM) na hofu yangu ni kwamba pengine kipindi hicho kimeandaliwa maalum katika ku-influence maamuzi ya Msajili wa Vyama katika pingamizi hilo la kihistoiria.
Nina maana hapa ingawa mada ni Sheria hiyo yote kwa ujumla, lakini ni dhahihiri watakaojadili hawataacha kutia mkazo katika hilo pingamizi. Hivyo watoa mada wanaweza kuwa wameandaliwa ili ku-influence uamuzi. Hawa ni pamoja na wale "watakaopiga simu."
Ingefaa kipindi hiki kingeahirishwa hadi baada ya ruling ya Tendwa.