its just a story with lesson in it

First Born

JF-Expert Member
Jul 11, 2011
5,310
1,473
ONCE UPON A TIME
There was 3 best friends Mike, Josh and
Chris.These guys were good friends,they were very
open to each other.Many people envied them and
tried to destroy their friendship but they failed.
One day the three of them were on a tour having a
nice time viewing wildlife,waterfalls,rivers etc.Then
they saw a mountain about 7 kilometers from where
they were standing.
They left there vehicle and decided to go to the
mountain on foot because there was no road to use
a vehicle.After walking for about 45 minutes they
reached the mountain.
As they were trying to climb the mountain they saw
a big curve.They entered the curve and found
Diamonds and other precious stones there.They
were very happy and Mike said "right now we are
the richest friends on earth".
They started parking the Diamonds and other
precious stones in their bags,before they could
Finnish parking Chris and Josh were very tired and
hungry. Mike said "guys i can see you are very
tired and hungry let me go back where we left our
car and get the food we left in the car so that we
can have the energy to carry these Diamonds".
Chris said "that's a good idea,i will remain with
Josh here so that we continue parking these
stones"after Mike had gone,Josh said "Chris lets kill
him and share the diamonds just the two of
us"Chris said "that's what i was thinking too but
lets wait until he comes back then we will kill him"
Mike reached where the car was and got the food
then he started saying to himself "what if i put
poison to this food and kill Chris and Josh,all the
diamonds will be mine,i would be very rich"so he
took the acid from the car battery and put it in the
food and drinks of Josh and Chris,not knowing that
they are also planning to kill him.
Moments later,Mike was back at the mountain where
he left Chris and Josh,as soon as they saw him
they stabbed him in the chest and stomach with
knives just as they had planned and he died.
Now,after they had killed Mike they decided to eat
the food which he brought so that they have the
energy to carry the Bags of Diamonds,not knowing
that the drinks and food were poisoned they ate and
drunk and they died as well also,the diamonds
remained there but the 3 best friends were all dead.
To others it is just a story,to some it is a lesson.
 
HAPO ZAMANI ZA KALE

Kulikuwa na marafiki watatu wanaopendana ambao majina yao ni Mike, Josh na Chris.
Kwa kweli hawa jamaa walikuwa ni marafiki wa kufa na kuzikana, hawakufichana jambo lolote iwe la kheri au shari.

Watu wengi waliowaonea sana wivu ikafikia hadi kutaka kuwaharibia urafiki wao lakini kwa jinsi walivyo marafiki wa kweli hakuna kilichoweza kuwatenganisha au juhudi za kuuvunja urafiki wao ziligonga mwamba kwa wale wenye vijiba vya roho.

Kuna siku marafiki hao walikuwa matembezini kwa ajili ya kujifurahisha nafsi zao ikiwemo kutembelea sehemu tofauti tofauti ikiwemo Mbuga, Mito, Maziwa, n.k. Ghafla kwa mbali wakiwa takribani umbali wa kilomita saba waliuona mlima.
Ikawabidi waliache gari lao na kuanza kutembea kuelekea mlimani sababu gari isingeweza kufika kuelekea mlimani kutokana hakukuwa na njia ya kuweza kuwafikisha kwa usafiri wa gari. Baada ya mwendo wa miguu wa takribani dakika 45 waliufikia mlima.

Na pale walipokuwa wanaanza kupanda mlima wakaliona pango kubwa sana. Bila kuleta ajizi wakaingia pangoni ile wanaingia tu wakaanza kuona madini ya Almasi na mengineyo tele aina tofauti tofauti yenye thamani ya hali ya juu. Kwa kweli walifurahi sana ikafikia hadi Mike kusema "hakika sasa sisi ni marafiki tajiri sana hapa ulimwenguni(tumetoka)".

Bila ajizi wakaanza kuzikusanya mali walizozikuta mle pangoni na kuanza kuzihifadhi kwenye mifuko yao kwa kila mmoja, wakiwa bado wapo kwenye zoezi la kujikusanyia Mali ghafla Chris na Josh wakashikwa na njaa na uchovu wa hali ya juu. Ikabidi Mike awaambie "ndugu zangu nawaona mmechoka na kubanwa na njaa ngoja niende ilipo Gari nikachukue chakula tulichokibakiza nije nacho tugonge(tule) ili tupate nguvu mpya kuendelea na zoezi letu la kujikusanyia Mali".
Chris akamjibu Mike "wazo zuri sana mimi nitaendelea kubaki na Josh hapa tukiendeleza zoezi la kujikusanyia Mali mdogo mdogo au kwa lugha nyingine tunaliendeleza libeneke taratibu" Baada ya Mike kuondoka Josh akapata wazo "Chris unaonaje tukimmaliza(tumuue) Mike ili hizi Mali zote tugawane mimi na wewe" Chris akajibu hata mimi nilikuwa nafikiria kitu kama hicho lakini ngoja kwanza arudi kisha tummalize"

Mike alifanikiwa kufika walipoliacha gari na kukichukua chakula kisha akawa anajiambia(kimoyo moyo) "kwanini nisiwawekee sumu Chris na Josh ili wapunguze idadi, na kisha Mali yote iwe yangu, hakika nikifanikisha zoezi la kuwaua Chris na Josh kwa kweli nitakuwa tajiri sana"

Alichokifanya Mike akachukua maji ya betri akayanyunyizia kwenye chakula na vinywaji vya wenzake wawili aliowaacha pangoni, bila na yeye kujua na yeye wawili aliowaacha pangoni wanamfanyia mpango wa kumuua.

Baada ya muda fulani Mike akawa na yeye amesharejea Mlimani alipowaacha marafiki zake Chris na Josh, lahaula ile Mike anafika tu akakaribishwa na visu kwa kweli walimchoma choma kifuani na kwenye tumbo kama walivyopanga mpango wao kwa kweli walifanikisha Mike alifariki dunia.

Baada ya kumuua Mike, Josh na Chris wakaanza kupata chakula(kula) kilicholetwa na Mike(marehemu) ili wapate nguvu mpya kujibebea mijifuko iliyosheheni Mali, walifakamia bila ya kufahamu kuwa chakula wanachokifakamia na vinywaji vilikuwa tayari vimeshanyunyiziwa sumu na Mike(Marehemu), Mungu si Athumani na wao(Chris na Josh) wakafariki dunia baada ya kufakamia chakula na vinywaji vyenye sumu.

Basi tena Mali zilibaki pale huku Marafiki wote watatu wakiwa wameshapoteza maisha, na hii yote sababu ya tamaa.

Kwa wengine inaweza kuwa hadithi, lakini kwa wengineo hili ni funzo tosha
 
HAPO ZAMANI ZA KALE

Kulikuwa na marafiki watatu wanaopendana ambao majina yao ni Mike, Josh na Chris.
Kwa kweli hawa jamaa walikuwa ni marafiki wa kufa na kuzikana, hawakufichana jambo lolote iwe la kheri au shari.

Watu wengi waliowaonea sana wivu ikafikia hadi kutaka kuwaharibia urafiki wao lakini kwa jinsi walivyo marafiki wa kweli hakuna kilichoweza kuwatenganisha au juhudi za kuuvunja urafiki wao ziligonga mwamba kwa wale wenye vijiba vya roho.

Kuna siku marafiki hao walikuwa matembezini kwa ajili ya kujifurahisha nafsi zao ikiwemo kutembelea sehemu tofauti tofauti ikiwemo Mbuga, Mito, Maziwa, n.k. Ghafla kwa mbali wakiwa takribani umbali wa kilomita saba waliuona mlima.
Ikawabidi waliache gari lao na kuanza kutembea kuelekea mlimani sababu gari isingeweza kufika kuelekea mlimani kutokana hakukuwa na njia ya kuweza kuwafikisha kwa usafiri wa gari. Baada ya mwendo wa miguu wa takribani dakika 45 waliufikia mlima.

Na pale walipokuwa wanaanza kupanda mlima wakaliona pango kubwa sana. Bila kuleta ajizi wakaingia pangoni ile wanaingia tu wakaanza kuona madini ya Almasi na mengineyo tele aina tofauti tofauti yenye thamani ya hali ya juu. Kwa kweli walifurahi sana ikafikia hadi Mike kusema "hakika sasa sisi ni marafiki tajiri sana hapa ulimwenguni(tumetoka)".

Bila ajizi wakaanza kuzikusanya mali walizozikuta mle pangoni na kuanza kuzihifadhi kwenye mifuko yao kwa kila mmoja, wakiwa bado wapo kwenye zoezi la kujikusanyia Mali ghafla Chris na Josh wakashikwa na njaa na uchovu wa hali ya juu. Ikabidi Mike awaambie "ndugu zangu nawaona mmechoka na kubanwa na njaa ngoja niende ilipo Gari nikachukue chakula tulichokibakiza nije nacho tugonge(tule) ili tupate nguvu mpya kuendelea na zoezi letu la kujikusanyia Mali".
Chris akamjibu Mike "wazo zuri sana mimi nitaendelea kubaki na Josh hapa tukiendeleza zoezi la kujikusanyia Mali mdogo mdogo au kwa lugha nyingine tunaliendeleza libeneke taratibu" Baada ya Mike kuondoka Josh akapata wazo "Chris unaonaje tukimmaliza(tumuue) Mike ili hizi Mali zote tugawane mimi na wewe" Chris akajibu hata mimi nilikuwa nafikiria kitu kama hicho lakini ngoja kwanza arudi kisha tummalize"

Mike alifanikiwa kufika walipoliacha gari na kukichukua chakula kisha akawa anajiambia(kimoyo moyo) "kwanini nisiwawekee sumu Chris na Josh ili wapunguze idadi, na kisha Mali yote iwe yangu, hakika nikifanikisha zoezi la kuwaua Chris na Josh kwa kweli nitakuwa tajiri sana"

Alichokifanya Mike akachukua maji ya betri akayanyunyizia kwenye chakula na vinywaji vya wenzake wawili aliowaacha pangoni, bila na yeye kujua na yeye wawili aliowaacha pangoni wanamfanyia mpango wa kumuua.

Baada ya muda fulani Mike akawa na yeye amesharejea Mlimani alipowaacha marafiki zake Chris na Josh, lahaula ile Mike anafika tu akakaribishwa na visu kwa kweli walimchoma choma kifuani na kwenye tumbo kama walivyopanga mpango wao kwa kweli walifanikisha Mike alifariki dunia.

Baada ya kumuua Mike, Josh na Chris wakaanza kupata chakula(kula) kilicholetwa na Mike(marehemu) ili wapate nguvu mpya kujibebea mijifuko iliyosheheni Mali, walifakamia bila ya kufahamu kuwa chakula wanachokifakamia na vinywaji vilikuwa tayari vimeshanyunyiziwa sumu na Mike(Marehemu), Mungu si Athumani na wao(Chris na Josh) wakafariki dunia baada ya kufakamia chakula na vinywaji vyenye sumu.

Basi tena Mali zilibaki pale huku Marafiki wote watatu wakiwa wameshapoteza maisha, na hii yote sababu ya tamaa.

Kwa wengine inaweza kuwa hadithi, lakini kwa wengineo hili ni funzo tosha

Mmmmh!!! asante kwa tafsiri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom