Juzi nilipokuwa naangalia habari ya saa 2 usiku ITV tulionyeshwa watu wakilalamika wilayani Sengerema mkoani Mwanza baada ya Tanroads kuweka mzani wa kupimia magari(weightbridge) kwenye barabara ya CHANGARAWE! Magari yalioonekana kuzidisha kipimo yalikua yanalipishwa faini kwa KUHARIBU barabara.Kote ulimwenguni kuna utaratibu wa kuzuia magari kuzidisha uzito kwenye barabara za lami na nchini ZAmbia niliona utaratibu wa magari mazito kwenye migodi ya shaba kutengenezewa barabara za changarawe kuepusha magari hayo kupita kwenya njia za lami.