NostradamusEstrademe
JF-Expert Member
- Jul 1, 2017
- 3,032
- 4,028
Siku chache tu baada ya shambulio la Hamas tarehe 7 Oktoba, Rais wa Marekani Joe Biden alifika Tel Aviv na kueleza mshikamano wa Marekani na Israel.
Aliwaita Hamas ni 'mashetani' na kusema Marekani iko pamoja na Israel katika kila hali na itapata kila msaada.
Mwanzoni mwa mwezi Novemba, Bunge la Marekani liliidhinisha pendekezo la msaada wa kijeshi wa dola bilioni 14.5 kwa Israel.
Marekani pia inaonekana kuunga mkono msimamo wa Israel kuhusu kutositisha mapigano Gaza.
Urafiki wao una umri gani?
Rais wa Marekani Henry Truman alikuwa mwanasiasa wa kwanza duniani kuitambua Israel. Tarehe 2 Novemba 1917, Azimio la Balfour la Uingereza liliunga mkono kuanzishwa nchi ya Wayahudi huko Palestina.
Miaka miwili baadaye, Machi 3, 1919, aliyekuwa Rais wa Marekani wakati huo Woodrow Wilson aliunga mkono wazo la kuwa na nchi ya Wayahudi.
Baadaye mwaka 1922 na tena mwaka 1944, Bunge la Marekani lilipitisha maazimio ya kuunga mkono Azimio la Balfour. 1948 Marekani ikawa nchi ya kwanza kuitambua.
Ndani ya dakika 11 tangu Israel kujitangaza kuwa nchi, Marekani iliitambua Israel kama nchi. Rais wa wakati huo Harry Truman alikuwa kiongozi wa kwanza duniani kuitambua Israel.
Kwa nini Marekani iliitambua Israel haraka?
Kilikuwa ni kipindi cha baada ya Vita vya Pili vya Dunia - wakati Vita Baridi kati ya Marekani na Muungano wa Sovieti vilipokuwa vinaanza.
Marekani ilivutiwa na nchi za Kiarabu kutokana na hifadhi zao za mafuta(uroho). Vilevile njia ya baharini ya Mfereji wa Suez - ilikuwa njia ya biashara ya kimataifa. Ulikuwa ni uwanja wa kupimana nguvu kati ya Marekani na Sovieti.
Marekani ilivutiwa na hifadhi ya mafuta katika ulimwengu wa Kiarabu. Kwa hiyo ilihitaji Israel ili kudhibiti nchi za Kiarabu. Hii ndiyo sababu kwa nini Marekani haikuchelewa kuitambua Israel na kuijengea uwezo wa kijeshi.
Nyakati za mivutano
Licha ya uhusiano imara wa Marekani na Israel – lakini huko nyuma kumekuwa na mivutano katika uhusiano wao. Wakati Israel ilipoanzisha vita na Ufaransa na Uingereza juu ya Mfereji wa Suez, utawala wa Eisenhower wa Marekani uliikasirikia sana.
Rais wa Marekani alitishia ikiwa Israel haitaondoka katika maeneo iliyoyateka wakati wa vita, misaada itasitishwa.
Umoja wa Kisovieti pia ulitishia ikiwa Israel haitarudi nyuma, ingeishambulia kwa makombora. Chini ya shinikizo hilo, Israel ilibidi kurudi nyuma kutoka maeneo hayo.
Vile vile, katika miaka ya 1960, kulikuwa na mvutano katika uhusiano wa Marekani na Israel. Wakati huo, utawala wa Kennedy wa Marekani ulikuwa na wasiwasi kuhusu mipango ya siri ya Israel ya nyuklia.
Lakini 1967 baada ya Israel kuzishinda Jordan, Syria na Misri katika vita vya siku sita na kuteka eneo kubwa la ulimwengu wa Kiarabu, mtazamo wa Marekani kwa nchi hii ya Kiyahudi ulibadilika kabisa.
Wakati huo Marekani ilikuwa imejiingiza katika Vita vya Vietnam na Israel ilizishinda nchi za Kiarabu bila msaada wowote mkubwa kutoka Marekani.Kuna wanaoamini kuwa kifo cha raisi wa Misri Gamael Abdel Nasseer kilicho sababishwa na shambulio la moyo mwaka 1970 wakati akiwa kwenye mkutano wa jumuiya ya nchi za kiarabu ulichangiwa pia na Israeli ilivyofanikiwa kuzitandika nchi tatu za kiarabu Misri ikiwepo kwa ushindi mkubwa katika vita hiyo ya siku sita mwaka 1967.Hata hivyo dhana hii haina mashiko maana alifariki miaka mitatu baada ya vita hiyo.
Jambo jingine muhimu ni kwamba - nchi mbili ambazo zilishindwa na Israel, Misri na Syria, zilikuwa marafiki wa Umoja wa Kisovieti.
Baada ya ushindi huu wa Israel, Marekani ilianza kuiona Israel kama mshirika wa kudumu dhidi ya Umoja wa Kisovieti katika ulimwengu wa Kiarabu.
Obama, Netanyahu na Biden
Uhusiano kati ya Marekani na Israel ulionekana kuyumba kwa muda mfupi kutokana na tofauti kati ya Rais wa zamani wa Marekani Barack Obama na Waziri Mkuu wa sasa wa Israel.
Kulikuwa na mzozo kati ya wawili hao kuhusu makubaliano ya nyuklia na Iran. Netanyahu alikwenda kwenye Bunge la Marekani linalotawaliwa na Chama cha Republican na kumkosoa vikali Barack Obama kuhusiana na sera ya Marekani kwa Iran.
Wakati wa utawala wake wa miaka minane, Obama alipinga maazimio yote dhidi ya Israel isipokuwa azimio moja katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Biden hivi karibuni alikosoa jaribio la Netanyahu la kubadili mfumo wa mahakama nchini Israel, lakini baada ya shambulio la Hamas Oktoba 7, ameonekana kusimama imara na Waziri Mkuu wa Israel.
Uhusiano wao sasa ukoje?
Kwa sasa, Marekani inafanya kazi kama mshirika wa ajabu wa Israel. Marekani inatoa msaada wa kifedha, kijeshi na kisiasa bila masharti kwa Israel.
Israel ina nguvu ya nyuklia ambayo haijatangazwa. Lakini kwa sababu ya kukingiwa kifua na Marekani haijawahi kukabiliwa na uchunguzi wowote.
Marekani inatoa msaada mkubwa wa kiuchumi kwa Israel. Tangu Vita vya Pili vya Dunia, imepokea msaada wa Marekani wenye thamani ya dola bilioni 158.
Kila mwaka inapokea misaada ya Marekani yenye thamani ya dola bilioni 3.8, ambayo ni takriban asilimia 16 ya bajeti yote ya ulinzi ya Israel. Leo Israel imekuwa msafirishaji wa kumi wa silaha na zana za kijeshi ulimwenguni.
Israel pia ni mshirika mkubwa wa kibiashara wa Marekani. Kuna biashara ya dola bilioni 50 kati ya nchi hizo mbili kila mwaka.
Tangu 1972, Marekani imekataa maazimio 50 yaliyoletwa dhidi ya Israeli katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Makundi ya ushawishi ya Israel
Israel ina umuhimu wa kimkakati katika siasa za ulimwengu wa Kiarabu. Wakati wa Vita Baridi, Marekani iliitumia Israeli kama ngome muhimu dhidi ya ushawishi wa Umoja wa Kisovieti katika ulimwengu wa Kiarabu.
Baada ya Vita Baridi, Marekani ilizidi kujiweka Asia Magharibi na nchi ya Israel, Saudi Arabia na Misri zikawa washirika wake muhimu.
Maoni ya watu wa Marekani, siasa za wakati wa uchaguzi na makundi ya ushawishi - ni mambo yanyochangia sera ya Marekani inayoiunga mkono Israel.
Katika Bunge la Marekani, wabunge wengi wa vyama vya Republican na Democratic wanaunga mkono Israel. Makundi ya ushawishi kutoka jamii ya Wayahudi na Wakristo wote hufanya kazi kubwa kuhakikisha uungwaji mkono wa Israel katika siasa za Marekani.
Kundi moja la ushawishi lenye nguvu ni Kamati ya Masuala ya Israel na Marekani au AIPAC. Marais, Maseneta na Mawaziri Wakuu wa Israel na Marekani huhudhuria mikutano yake ya kila mwaka kama wageni.
Mashirika yanayounga mkono Israel hutoa usaidizi wa kifedha kwa vyama vya Republican na Democratic. 2020 mashirika hayo yalikusanya dola bilioni 30, asilimia 63 zilitolewa kwa Democratic na nyingine kwa wabunge wa Republican.
Je, kuna makundi ya ushawishi kwa Wapalestina?
Katika miaka michache iliyopita, maseneta kama Bernie Sanders na Elizabeth Warren wa Chama cha Democratic wamejitokeza kama wafuasi wa Palestina.
Wote wawili walishiriki katika kinyang'anyiro cha kusaka tiketi ya kugombea urais 2020. Bernie na Warren wanasema misaada ya kiuchumi inayotolewa kwa Israel inapaswa kuwa na masharti ya kulinda haki za binadamu za Wapalestina.
Kizazi cha wanasiasa wachanga kama Alexandria Ocasio-Cortez, Ilhan Omar, Ayanna Presley na Rashida Taleb wameibuka kama sauti za Palestina katika Bunge la Marekani.
Katika miaka ya hivi karibuni, uungaji mkono wa Palestina umeongezeka miongoni mwa wa-Marekani. Kwa mujibu wa utafiti wa Gallup, asilimia 25 ya watu walioshiriki katika utafiti huo mwezi Februari mwaka huu walionesha kuunga mkono harakati za Palestina. Miaka mitano iliyopita ilikuwa asilimia 19.
Lakini sehemu kubwa ya umma wa Marekani bado wanaunga mkono Israel. Asilimia 58 ya Wamarekani waliohojiwa waliunga mkono Israel. Na asilimia 75 ya Wamarekani walitoa maoni mazuri juu ya Israel.
Kwa hiyo tumeona kuwa uhusiano wa Israeli na Marekani hauko katika mrengo wa kidini kuwa Israeli ni nchi ya Kikristo hivyo inaisaidia Israeli sababu ya Ukristo wake jambo ambalo sio kweli kabisa.Marekani kwa kawaida ni nchi ya kinafiki sana hivyo kuipenda kwake Israel ni kisiasa zaidi na maslahi.Kwa upande wa maslahi Israel ni nchi ndogo kuliko mkoa wa Tabora lakini imejaliwa kuwa na watu wenye akili nyingi kupindukia.
Wataalamu waliobobea wagunduzi wengi mfano Albert Eistein aliyegundua bomu la atomic alikuwa myahudi,Mark Zuckeberg mmiliki wa Facebook na mwenzake Eduardo Severin ni wayahudi,huko Ujerumani wayahudi ndio waliokuwa wanamiliki uchumi wa Ujerumani na ndio maana Hitler aliwachukia baada ya vita vya kwanza vya dunia wajerumani kushindwa ndio akawa anawasingizia kuwa wao ndio chanzo,kwa kuangalia idadi ya watu wake na eneo lake ugawe uwiano kwa watu walioshinda medali ya Nobel utagundua ni Waisraeli wako wengi,
Hapan nitoe mfano kuanzia mwaka 1901 hadi mwaka huu 2023 katika watu walipata medali za nobel ya katika sayansi na uchumi duniani ni 965 kati ya hao wayahudi ni 214. Kwa maana hiyo ni asilimia 22%.Na Wayahudi ni aisilimia 0.2% ya idadi ya watu duniani ambao ni billioni 8.Wayahudi wao wako millioni 16.1 hii ni kwa walio dunia nzima sio Israel.Sasa ukichukua eneo la Israeli ni kilomita za Mraba 21,671 na ukichukua eneo la dunia nzima ni kilomita za mraba millioni 149.Sasa ukipiga hesabu uchukue eneo la mraba ugawe kwa idadi ya watu walipata nishani za Nobel utagundua kuwa 21,671/214 utapata kuwa kwa Israeli kila kilomita za mraba 101 kuna Muisraeli mmoja amesimama mwenye nishani hiyo.Ukichukua dunia nzima chukua milioni149/965 utaona kuwa kila baada ya kilomita za mraba l54,000 ndio kumesimama mtu mmoja mwenye nishani hiyo.
Makampuni makubwa yaliyoko Marekani yanamilikiwa na waisraeli mababu zao waliohama miaka nenda rudi kiasi wengine hata hawajui kuwa kwao ni Israel,Ukienda mbali zaidi waliogundua vifaa vya anga za kwenda kwenye masayari ni wayahudi upande wa Urusi,Marekani,Ujerumani na nchi zingine.Wamarekani na warusi waliwaiba wataalamu hawa wa kiyahudi kwa mtutu wa bunduki hasa upande wa Urusi ndio vyombo vikaanza kwenda anga za mbali.Nchi ya Marekani na ukubwa wake ukweli ni kwamba wote ni wahamiaji wakazi asili wa kule ni Wahindi wekundu.Hivyo maendeleo ya uchumi nguvu za kijeshi,teknolojia vyote hivyi vimechangiwa na wageni Wayahudi wakiwemo kwa mchango mkubwa.Marekani kilikuwa kituo kikubwa au tuite hub kwenye karne ya 18 kuwapokea wahamiaji wa Kiyahudi waliokuwa wanatoroka ulaya kukwepa mateso na manyanyaso.Sasa nadhani mmeona msimamo wa Marekani juu ya hawa Wayahudi
Pia ni ukweli ulio wazi asilimia ya wakristo Israeli ni ndogo mno kuliko waislam walioko Israeli.
Watu wengi hapa nchi watanisamehe sana nitatumia lugha sio nzuri nitawaita wajinga na wapumbafu.Kwasababu wao wanaona Israel ni taifa ya Kikristo wakati sio kweli kabisa ila katiba ya Israeli imetoa haki ya kuabudu dini zote wako waislam Israeli ambao wako jeshi la IDF wako wakrito pia na wapo wa dini ya Yuda.Ukienda upande wa Palestina kuna wakristo pia na Waislam.
Sisi huku wajinga wanataka kufanya maandamano kutetea wapalestina kisa ni waislam wenzao kiukweli hawa wanaopigana ni watu ndugu kabisa sana mtoto wa baba mkubwa na mdogo.HAMAS ni kundi la kidini tu ambalo lina nguvu kubwa kuliko serikali ila sio msimamo wa Serikali.
Toleo lijalo tutaona Dini za Yuda,Ukristo na Uislama wa Israeli na wapalestina wanavyoabudu na chanzo chake.
Tutaona uhusiano wa YESU na wanawaisraeli wa sasa na tutaona ni jinsi gani waisraeli wanamchukulia YESU ni jinsi gani idadi ya Waislam Israeli ni kubwa kuliko wakristo wenyewe ambapo ndio YESU alikotokea
Itaendelea…………………………………………………….
Aliwaita Hamas ni 'mashetani' na kusema Marekani iko pamoja na Israel katika kila hali na itapata kila msaada.
Mwanzoni mwa mwezi Novemba, Bunge la Marekani liliidhinisha pendekezo la msaada wa kijeshi wa dola bilioni 14.5 kwa Israel.
Marekani pia inaonekana kuunga mkono msimamo wa Israel kuhusu kutositisha mapigano Gaza.
Urafiki wao una umri gani?
Rais wa Marekani Henry Truman alikuwa mwanasiasa wa kwanza duniani kuitambua Israel. Tarehe 2 Novemba 1917, Azimio la Balfour la Uingereza liliunga mkono kuanzishwa nchi ya Wayahudi huko Palestina.
Miaka miwili baadaye, Machi 3, 1919, aliyekuwa Rais wa Marekani wakati huo Woodrow Wilson aliunga mkono wazo la kuwa na nchi ya Wayahudi.
Baadaye mwaka 1922 na tena mwaka 1944, Bunge la Marekani lilipitisha maazimio ya kuunga mkono Azimio la Balfour. 1948 Marekani ikawa nchi ya kwanza kuitambua.
Ndani ya dakika 11 tangu Israel kujitangaza kuwa nchi, Marekani iliitambua Israel kama nchi. Rais wa wakati huo Harry Truman alikuwa kiongozi wa kwanza duniani kuitambua Israel.
Kwa nini Marekani iliitambua Israel haraka?
Kilikuwa ni kipindi cha baada ya Vita vya Pili vya Dunia - wakati Vita Baridi kati ya Marekani na Muungano wa Sovieti vilipokuwa vinaanza.
Marekani ilivutiwa na nchi za Kiarabu kutokana na hifadhi zao za mafuta(uroho). Vilevile njia ya baharini ya Mfereji wa Suez - ilikuwa njia ya biashara ya kimataifa. Ulikuwa ni uwanja wa kupimana nguvu kati ya Marekani na Sovieti.
Marekani ilivutiwa na hifadhi ya mafuta katika ulimwengu wa Kiarabu. Kwa hiyo ilihitaji Israel ili kudhibiti nchi za Kiarabu. Hii ndiyo sababu kwa nini Marekani haikuchelewa kuitambua Israel na kuijengea uwezo wa kijeshi.
Nyakati za mivutano
Licha ya uhusiano imara wa Marekani na Israel – lakini huko nyuma kumekuwa na mivutano katika uhusiano wao. Wakati Israel ilipoanzisha vita na Ufaransa na Uingereza juu ya Mfereji wa Suez, utawala wa Eisenhower wa Marekani uliikasirikia sana.
Rais wa Marekani alitishia ikiwa Israel haitaondoka katika maeneo iliyoyateka wakati wa vita, misaada itasitishwa.
Umoja wa Kisovieti pia ulitishia ikiwa Israel haitarudi nyuma, ingeishambulia kwa makombora. Chini ya shinikizo hilo, Israel ilibidi kurudi nyuma kutoka maeneo hayo.
Vile vile, katika miaka ya 1960, kulikuwa na mvutano katika uhusiano wa Marekani na Israel. Wakati huo, utawala wa Kennedy wa Marekani ulikuwa na wasiwasi kuhusu mipango ya siri ya Israel ya nyuklia.
Lakini 1967 baada ya Israel kuzishinda Jordan, Syria na Misri katika vita vya siku sita na kuteka eneo kubwa la ulimwengu wa Kiarabu, mtazamo wa Marekani kwa nchi hii ya Kiyahudi ulibadilika kabisa.
Wakati huo Marekani ilikuwa imejiingiza katika Vita vya Vietnam na Israel ilizishinda nchi za Kiarabu bila msaada wowote mkubwa kutoka Marekani.Kuna wanaoamini kuwa kifo cha raisi wa Misri Gamael Abdel Nasseer kilicho sababishwa na shambulio la moyo mwaka 1970 wakati akiwa kwenye mkutano wa jumuiya ya nchi za kiarabu ulichangiwa pia na Israeli ilivyofanikiwa kuzitandika nchi tatu za kiarabu Misri ikiwepo kwa ushindi mkubwa katika vita hiyo ya siku sita mwaka 1967.Hata hivyo dhana hii haina mashiko maana alifariki miaka mitatu baada ya vita hiyo.
Jambo jingine muhimu ni kwamba - nchi mbili ambazo zilishindwa na Israel, Misri na Syria, zilikuwa marafiki wa Umoja wa Kisovieti.
Baada ya ushindi huu wa Israel, Marekani ilianza kuiona Israel kama mshirika wa kudumu dhidi ya Umoja wa Kisovieti katika ulimwengu wa Kiarabu.
Obama, Netanyahu na Biden
Uhusiano kati ya Marekani na Israel ulionekana kuyumba kwa muda mfupi kutokana na tofauti kati ya Rais wa zamani wa Marekani Barack Obama na Waziri Mkuu wa sasa wa Israel.
Kulikuwa na mzozo kati ya wawili hao kuhusu makubaliano ya nyuklia na Iran. Netanyahu alikwenda kwenye Bunge la Marekani linalotawaliwa na Chama cha Republican na kumkosoa vikali Barack Obama kuhusiana na sera ya Marekani kwa Iran.
Wakati wa utawala wake wa miaka minane, Obama alipinga maazimio yote dhidi ya Israel isipokuwa azimio moja katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Biden hivi karibuni alikosoa jaribio la Netanyahu la kubadili mfumo wa mahakama nchini Israel, lakini baada ya shambulio la Hamas Oktoba 7, ameonekana kusimama imara na Waziri Mkuu wa Israel.
Uhusiano wao sasa ukoje?
Kwa sasa, Marekani inafanya kazi kama mshirika wa ajabu wa Israel. Marekani inatoa msaada wa kifedha, kijeshi na kisiasa bila masharti kwa Israel.
Israel ina nguvu ya nyuklia ambayo haijatangazwa. Lakini kwa sababu ya kukingiwa kifua na Marekani haijawahi kukabiliwa na uchunguzi wowote.
Marekani inatoa msaada mkubwa wa kiuchumi kwa Israel. Tangu Vita vya Pili vya Dunia, imepokea msaada wa Marekani wenye thamani ya dola bilioni 158.
Kila mwaka inapokea misaada ya Marekani yenye thamani ya dola bilioni 3.8, ambayo ni takriban asilimia 16 ya bajeti yote ya ulinzi ya Israel. Leo Israel imekuwa msafirishaji wa kumi wa silaha na zana za kijeshi ulimwenguni.
Israel pia ni mshirika mkubwa wa kibiashara wa Marekani. Kuna biashara ya dola bilioni 50 kati ya nchi hizo mbili kila mwaka.
Tangu 1972, Marekani imekataa maazimio 50 yaliyoletwa dhidi ya Israeli katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Makundi ya ushawishi ya Israel
Israel ina umuhimu wa kimkakati katika siasa za ulimwengu wa Kiarabu. Wakati wa Vita Baridi, Marekani iliitumia Israeli kama ngome muhimu dhidi ya ushawishi wa Umoja wa Kisovieti katika ulimwengu wa Kiarabu.
Baada ya Vita Baridi, Marekani ilizidi kujiweka Asia Magharibi na nchi ya Israel, Saudi Arabia na Misri zikawa washirika wake muhimu.
Maoni ya watu wa Marekani, siasa za wakati wa uchaguzi na makundi ya ushawishi - ni mambo yanyochangia sera ya Marekani inayoiunga mkono Israel.
Katika Bunge la Marekani, wabunge wengi wa vyama vya Republican na Democratic wanaunga mkono Israel. Makundi ya ushawishi kutoka jamii ya Wayahudi na Wakristo wote hufanya kazi kubwa kuhakikisha uungwaji mkono wa Israel katika siasa za Marekani.
Kundi moja la ushawishi lenye nguvu ni Kamati ya Masuala ya Israel na Marekani au AIPAC. Marais, Maseneta na Mawaziri Wakuu wa Israel na Marekani huhudhuria mikutano yake ya kila mwaka kama wageni.
Mashirika yanayounga mkono Israel hutoa usaidizi wa kifedha kwa vyama vya Republican na Democratic. 2020 mashirika hayo yalikusanya dola bilioni 30, asilimia 63 zilitolewa kwa Democratic na nyingine kwa wabunge wa Republican.
Je, kuna makundi ya ushawishi kwa Wapalestina?
Katika miaka michache iliyopita, maseneta kama Bernie Sanders na Elizabeth Warren wa Chama cha Democratic wamejitokeza kama wafuasi wa Palestina.
Wote wawili walishiriki katika kinyang'anyiro cha kusaka tiketi ya kugombea urais 2020. Bernie na Warren wanasema misaada ya kiuchumi inayotolewa kwa Israel inapaswa kuwa na masharti ya kulinda haki za binadamu za Wapalestina.
Kizazi cha wanasiasa wachanga kama Alexandria Ocasio-Cortez, Ilhan Omar, Ayanna Presley na Rashida Taleb wameibuka kama sauti za Palestina katika Bunge la Marekani.
Katika miaka ya hivi karibuni, uungaji mkono wa Palestina umeongezeka miongoni mwa wa-Marekani. Kwa mujibu wa utafiti wa Gallup, asilimia 25 ya watu walioshiriki katika utafiti huo mwezi Februari mwaka huu walionesha kuunga mkono harakati za Palestina. Miaka mitano iliyopita ilikuwa asilimia 19.
Lakini sehemu kubwa ya umma wa Marekani bado wanaunga mkono Israel. Asilimia 58 ya Wamarekani waliohojiwa waliunga mkono Israel. Na asilimia 75 ya Wamarekani walitoa maoni mazuri juu ya Israel.
Kwa hiyo tumeona kuwa uhusiano wa Israeli na Marekani hauko katika mrengo wa kidini kuwa Israeli ni nchi ya Kikristo hivyo inaisaidia Israeli sababu ya Ukristo wake jambo ambalo sio kweli kabisa.Marekani kwa kawaida ni nchi ya kinafiki sana hivyo kuipenda kwake Israel ni kisiasa zaidi na maslahi.Kwa upande wa maslahi Israel ni nchi ndogo kuliko mkoa wa Tabora lakini imejaliwa kuwa na watu wenye akili nyingi kupindukia.
Wataalamu waliobobea wagunduzi wengi mfano Albert Eistein aliyegundua bomu la atomic alikuwa myahudi,Mark Zuckeberg mmiliki wa Facebook na mwenzake Eduardo Severin ni wayahudi,huko Ujerumani wayahudi ndio waliokuwa wanamiliki uchumi wa Ujerumani na ndio maana Hitler aliwachukia baada ya vita vya kwanza vya dunia wajerumani kushindwa ndio akawa anawasingizia kuwa wao ndio chanzo,kwa kuangalia idadi ya watu wake na eneo lake ugawe uwiano kwa watu walioshinda medali ya Nobel utagundua ni Waisraeli wako wengi,
Hapan nitoe mfano kuanzia mwaka 1901 hadi mwaka huu 2023 katika watu walipata medali za nobel ya katika sayansi na uchumi duniani ni 965 kati ya hao wayahudi ni 214. Kwa maana hiyo ni asilimia 22%.Na Wayahudi ni aisilimia 0.2% ya idadi ya watu duniani ambao ni billioni 8.Wayahudi wao wako millioni 16.1 hii ni kwa walio dunia nzima sio Israel.Sasa ukichukua eneo la Israeli ni kilomita za Mraba 21,671 na ukichukua eneo la dunia nzima ni kilomita za mraba millioni 149.Sasa ukipiga hesabu uchukue eneo la mraba ugawe kwa idadi ya watu walipata nishani za Nobel utagundua kuwa 21,671/214 utapata kuwa kwa Israeli kila kilomita za mraba 101 kuna Muisraeli mmoja amesimama mwenye nishani hiyo.Ukichukua dunia nzima chukua milioni149/965 utaona kuwa kila baada ya kilomita za mraba l54,000 ndio kumesimama mtu mmoja mwenye nishani hiyo.
Makampuni makubwa yaliyoko Marekani yanamilikiwa na waisraeli mababu zao waliohama miaka nenda rudi kiasi wengine hata hawajui kuwa kwao ni Israel,Ukienda mbali zaidi waliogundua vifaa vya anga za kwenda kwenye masayari ni wayahudi upande wa Urusi,Marekani,Ujerumani na nchi zingine.Wamarekani na warusi waliwaiba wataalamu hawa wa kiyahudi kwa mtutu wa bunduki hasa upande wa Urusi ndio vyombo vikaanza kwenda anga za mbali.Nchi ya Marekani na ukubwa wake ukweli ni kwamba wote ni wahamiaji wakazi asili wa kule ni Wahindi wekundu.Hivyo maendeleo ya uchumi nguvu za kijeshi,teknolojia vyote hivyi vimechangiwa na wageni Wayahudi wakiwemo kwa mchango mkubwa.Marekani kilikuwa kituo kikubwa au tuite hub kwenye karne ya 18 kuwapokea wahamiaji wa Kiyahudi waliokuwa wanatoroka ulaya kukwepa mateso na manyanyaso.Sasa nadhani mmeona msimamo wa Marekani juu ya hawa Wayahudi
Pia ni ukweli ulio wazi asilimia ya wakristo Israeli ni ndogo mno kuliko waislam walioko Israeli.
Watu wengi hapa nchi watanisamehe sana nitatumia lugha sio nzuri nitawaita wajinga na wapumbafu.Kwasababu wao wanaona Israel ni taifa ya Kikristo wakati sio kweli kabisa ila katiba ya Israeli imetoa haki ya kuabudu dini zote wako waislam Israeli ambao wako jeshi la IDF wako wakrito pia na wapo wa dini ya Yuda.Ukienda upande wa Palestina kuna wakristo pia na Waislam.
Sisi huku wajinga wanataka kufanya maandamano kutetea wapalestina kisa ni waislam wenzao kiukweli hawa wanaopigana ni watu ndugu kabisa sana mtoto wa baba mkubwa na mdogo.HAMAS ni kundi la kidini tu ambalo lina nguvu kubwa kuliko serikali ila sio msimamo wa Serikali.
Toleo lijalo tutaona Dini za Yuda,Ukristo na Uislama wa Israeli na wapalestina wanavyoabudu na chanzo chake.
Tutaona uhusiano wa YESU na wanawaisraeli wa sasa na tutaona ni jinsi gani waisraeli wanamchukulia YESU ni jinsi gani idadi ya Waislam Israeli ni kubwa kuliko wakristo wenyewe ambapo ndio YESU alikotokea
Itaendelea…………………………………………………….