Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,900
ISHMAEL ALIZAA MASEYIDI(WATOTO) 12 AMBAO NDIO WAARABU WA LEO. ENEO LAO LA UMILIKI NI KUANZIA SAUDI ARABIA KUELEKEA Ashuru NA MASHARIKI YA MISRI.
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.
Kuna Watu wengi wanachanganya Madesa, kuchanganya waarabu na jamii zisizo na uhusiano na waarabu. Jamii za waarabu ni jamii zenye uhusiano wa kinasaba na uzao wa Ibrahimu ambazo zinatoka kwa mtoto wa kwanza wa Ibrahim aitwaye Ishmael kwa Mwanamke aitwaye Hajiri. Ikiwa jamii yoyote imetoka kwa Ishmael basi jamii hiyo inauhalali kuitwa Waarabu.
Hii ni kusema Muarabu ni mchanganyiko wa kidamu baina ya Muebrania" Hebrew"(Ibrahim) na Mmisri (Hajiri). Hapo ndipo anatoka Ishmael baba wa Waarabu aliyezaa Majumba, MASEYIDI, watoto kumi na mbili ambao ni jamii na jamaa zinajulikana leo kama Waarabu.
Ibrahim pia alizaa na Mwanamke mmoja aitwaye Ketura na kutoa mataifa mengine lakini hao sio waarabu. Hii ni nje ya mada.
Pia Ibrahimu alizaa na mkewe Sarah mtoto aitwaye Isaka ambaye huyu alitoa Mataifa Mawili, Waisrael kupitia Yakobo, na Waedomu kupitia Esau. Hii pia Ipo nje ya mada. Hao Waedomu na Waisraeli pia sio Waarabu kwani hawatokani na Ishmael ila wote ni ndugu kwa Baba yao Ibrahim.
Huwezi wataja Waarabu bila kumtaja Ibrahim na Sarah Mkewe kwa sababu bila Sarah kuchelewa kuzaa basi kusingekuwa na Waishmael. Huko pia ni nje ya mada.
Wanazuoni wakubwa wengi hupatana kuwa Waarabu Baba yao ni Ishmael na Babu yao ni Ibrahim.
Tofauti ya Waisraeli na Waarabu ni kuwa Waarabu wanaasili ya Afrika kupitia Wamisri(Hajiri).
Hajiri aliahidiwa na Malaika akiwa na mimba kuwa atamzaa Mtoto wa kiume na akaamrishwa amuite Ishmael, yaani Bwana amesikia mateso yake" utabiri ukaambatana na Baraka kuwa Mtoto huyo atatoa taifa kubwa lakini litakalopitia magomvi na misukosuko (sijajua kikomo chake)
Mwanzo 16:11-12
[11]Malaika wa BWANA akamwambia, Tazama! Wewe una mimba, utazaa mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Ishmaeli, maana BWANA amesikia kilio cha mateso yako.
[12]Naye atakuwa kama punda-mwitu kati ya watu, mkono wake utakuwa juu ya watu wote na mkono wa watu wote utakuwa juu yake, naye atakaa mbele yao ndugu zake wote.
Baada ya Hajiri na Ishmael kufukuzwa wakaelekea. Wakaelekea kuishi katika jangwa la Paran ambapo kwa leo ni kusini kwa nchi ya Saudi Arabia. Ukisema Saudi Arabia hutokuwa unakosea. Huko Kijana akakua. Maana yake akarudi kwao Misri kumchukulia kijana wake Mke. Kijana akaoa mke wa kimisri kama alivyo mama yake.
Mwanzo 21:20-21
[20]Mungu akawa pamoja na huyo kijana, naye akakua, akakaa katika jangwa, akawa mpiga upinde.
[21]Akakaa katika jangwa la Parani; mama yake akamtwalia mke katika nchi ya Misri.
Ukaaji wa jangwani na uwindaji na maisha ya kuhamahama (Nomad life) na kufanya uchuuzi na biashara ( Merchant) ndiko asili ya jina Arab. Hivyo kusema Arab kiasili utarejelea neno Jangwa au maisha ya kuhamahama.
Ishmael akajaliwa kupata watoto, majumbe kumi na wawili. Ambao waliitwa Waishmael " Ishmaelites" ambao nao walizaa jamii na jamaa zao.
Waishmael waliishi maeneo mengi ya mashariki ya kati, Kaskazini mwa pembe ya Afrika, kuanzia maeneo ya Somalia kaskazini, Arabia Peninsula mpaka maeneo ya Nchi za Hindi.
Mwanzo 25:16-18
[16]Hao ndio wana wa Ishmaeli, na hayo ni majina yao, katika miji yao, na katika vituo vyao, maseyidi kumi na wawili kwa kufuata jamaa zao.
These are the sons of Ishmael, and these are their names, by their towns, and by their castles; twelve princes according to their nations.
[17]Na hii ndiyo miaka ya maisha ya Ishmaeli, miaka mia na thelathini na saba. Akakata roho, akafa, akakusanyika kwa watu wake.
And these are the years of the life of Ishmael, an hundred and thirty and seven years: and he gave up the ghost and died; and was gathered unto his people.
[18]Wakakaa toka Havila mpaka Shuri, unaoelekea Misri, kwa njia ya kwenda Ashuru. Akakaa katikati ya ndugu zake wote.
And they dwelt from Havilah unto Shur, that is before Egypt, as thou goest toward Assyria: and he died in the presence of all his brethren.
Ishmael alizikwa alipozikwa Baba yake Ishmael. Pia Ishmael alimzika Baba yake Ibrahim.
Waarabu na Waisrael na Waedomu na jamii zote zinazotokana na Ibrahim zinafanana kiutamaduni kwa kiwango kikubwa. Ingawaje kuna utofauti kama wao wenyewe walivyo na utofauti wa kimaumbile kutokana na Mama zao kuwa na asili tofauti.
Gen 25:18 “These descendants of Ishmael were scattered across the country from Havilah to Shur (which is a little way to the northeast of the Egyptian border in the direction of Assyria)…compare
to 1Samuel 15:7 where Saul 'butchered the Amalekites from Havilah all the way to Shur, east of Egypt’ ..compare
Exodus 17:8 when “the Amalekites came and attacked the Israelites at Rephidim"
Based on these scriptures the ancient 'land of Havilah’ would be located in what is now Saudi Arabia.
Waishmael kutokana na shughuli zao za uchuuzi na biashara ( Merchantalism) ndio waliomnunua Yusufu kutoka kwa wanawayakobo na kwenda kumuuza Misri. Zingatia Waishmael na Waisraeli wakati huo walikuwa wanajuana kabisa kuwahi Babu yao ni mmoja ambaye ni Ibrahim.
Kuhusu ugomvi unaoendelea hapo Palestina, Ibrahim ambaye ndio chanzo kikuu cha mzozo huo yeye alimrithisha Isaka pekeake eneo hilo.
Huku akisahau au kupuuza iwe kwa bahati mbaya au makusudi kuwapa urithi watoto wake wengine akiwepo Ishmael na watoto wa Ketura.
Hii inatupa funzo sisi wababa yakuwa tunapotaka kutoa urithi tusitoe kwa upendeleo kwani inaweza kuleta matatizo.
Ingawaje siku hizi wapo wanaosema Uarabu ni utamaduni na haihusiani na Masuala ya damu, yaani mtu anaweza kufanyiwa assimilation akawa muarabu kwa kuwa na tamaduni za kiarabu. Hiyo inaweza kuwa sawa. Ni kama vile Wayahudi nao wanasheria hiyo ya kumsilimisha mtu asiyemyahudi kuwa MYAHUDI kwa utaratibu maalum. Hata Wafaransa nao walifanya hivyo.
Lakini tukizungumzia Masuala ya vinasaba basi Huwezi kuwa muarabu kama huna vinasaba au damu ya Ishmael. Mama au mama yako akiwa muarabu basi wewe utaitwa muarabu. Halikadhalika na kwa wayahudi na wafaransa na mataifa mengine.
Lakini hiyo ya kusilimishwa, assimilation ni mambo ya kisiasa tuu.
FaizaFoxy, Wairan, Wamedi(Iraq) Waashuru ( Syria) hao sio waarabu. Na sikatai kuwa zipo jamii na jamaa au makabila ya waarabu yanayoishi katika mataifa hayo. Ni kama hapa Tanzania kuna waarabu lakini huwezi sema Watanzania ni waarabu. Pia wapo machotara waliozaliwa.
Taikon acha nipumzike sasa.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.
Kuna Watu wengi wanachanganya Madesa, kuchanganya waarabu na jamii zisizo na uhusiano na waarabu. Jamii za waarabu ni jamii zenye uhusiano wa kinasaba na uzao wa Ibrahimu ambazo zinatoka kwa mtoto wa kwanza wa Ibrahim aitwaye Ishmael kwa Mwanamke aitwaye Hajiri. Ikiwa jamii yoyote imetoka kwa Ishmael basi jamii hiyo inauhalali kuitwa Waarabu.
Hii ni kusema Muarabu ni mchanganyiko wa kidamu baina ya Muebrania" Hebrew"(Ibrahim) na Mmisri (Hajiri). Hapo ndipo anatoka Ishmael baba wa Waarabu aliyezaa Majumba, MASEYIDI, watoto kumi na mbili ambao ni jamii na jamaa zinajulikana leo kama Waarabu.
Ibrahim pia alizaa na Mwanamke mmoja aitwaye Ketura na kutoa mataifa mengine lakini hao sio waarabu. Hii ni nje ya mada.
Pia Ibrahimu alizaa na mkewe Sarah mtoto aitwaye Isaka ambaye huyu alitoa Mataifa Mawili, Waisrael kupitia Yakobo, na Waedomu kupitia Esau. Hii pia Ipo nje ya mada. Hao Waedomu na Waisraeli pia sio Waarabu kwani hawatokani na Ishmael ila wote ni ndugu kwa Baba yao Ibrahim.
Huwezi wataja Waarabu bila kumtaja Ibrahim na Sarah Mkewe kwa sababu bila Sarah kuchelewa kuzaa basi kusingekuwa na Waishmael. Huko pia ni nje ya mada.
Wanazuoni wakubwa wengi hupatana kuwa Waarabu Baba yao ni Ishmael na Babu yao ni Ibrahim.
Tofauti ya Waisraeli na Waarabu ni kuwa Waarabu wanaasili ya Afrika kupitia Wamisri(Hajiri).
Hajiri aliahidiwa na Malaika akiwa na mimba kuwa atamzaa Mtoto wa kiume na akaamrishwa amuite Ishmael, yaani Bwana amesikia mateso yake" utabiri ukaambatana na Baraka kuwa Mtoto huyo atatoa taifa kubwa lakini litakalopitia magomvi na misukosuko (sijajua kikomo chake)
Mwanzo 16:11-12
[11]Malaika wa BWANA akamwambia, Tazama! Wewe una mimba, utazaa mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Ishmaeli, maana BWANA amesikia kilio cha mateso yako.
[12]Naye atakuwa kama punda-mwitu kati ya watu, mkono wake utakuwa juu ya watu wote na mkono wa watu wote utakuwa juu yake, naye atakaa mbele yao ndugu zake wote.
Baada ya Hajiri na Ishmael kufukuzwa wakaelekea. Wakaelekea kuishi katika jangwa la Paran ambapo kwa leo ni kusini kwa nchi ya Saudi Arabia. Ukisema Saudi Arabia hutokuwa unakosea. Huko Kijana akakua. Maana yake akarudi kwao Misri kumchukulia kijana wake Mke. Kijana akaoa mke wa kimisri kama alivyo mama yake.
Mwanzo 21:20-21
[20]Mungu akawa pamoja na huyo kijana, naye akakua, akakaa katika jangwa, akawa mpiga upinde.
[21]Akakaa katika jangwa la Parani; mama yake akamtwalia mke katika nchi ya Misri.
Ukaaji wa jangwani na uwindaji na maisha ya kuhamahama (Nomad life) na kufanya uchuuzi na biashara ( Merchant) ndiko asili ya jina Arab. Hivyo kusema Arab kiasili utarejelea neno Jangwa au maisha ya kuhamahama.
Ishmael akajaliwa kupata watoto, majumbe kumi na wawili. Ambao waliitwa Waishmael " Ishmaelites" ambao nao walizaa jamii na jamaa zao.
Waishmael waliishi maeneo mengi ya mashariki ya kati, Kaskazini mwa pembe ya Afrika, kuanzia maeneo ya Somalia kaskazini, Arabia Peninsula mpaka maeneo ya Nchi za Hindi.
Mwanzo 25:16-18
[16]Hao ndio wana wa Ishmaeli, na hayo ni majina yao, katika miji yao, na katika vituo vyao, maseyidi kumi na wawili kwa kufuata jamaa zao.
These are the sons of Ishmael, and these are their names, by their towns, and by their castles; twelve princes according to their nations.
[17]Na hii ndiyo miaka ya maisha ya Ishmaeli, miaka mia na thelathini na saba. Akakata roho, akafa, akakusanyika kwa watu wake.
And these are the years of the life of Ishmael, an hundred and thirty and seven years: and he gave up the ghost and died; and was gathered unto his people.
[18]Wakakaa toka Havila mpaka Shuri, unaoelekea Misri, kwa njia ya kwenda Ashuru. Akakaa katikati ya ndugu zake wote.
And they dwelt from Havilah unto Shur, that is before Egypt, as thou goest toward Assyria: and he died in the presence of all his brethren.
Ishmael alizikwa alipozikwa Baba yake Ishmael. Pia Ishmael alimzika Baba yake Ibrahim.
Waarabu na Waisrael na Waedomu na jamii zote zinazotokana na Ibrahim zinafanana kiutamaduni kwa kiwango kikubwa. Ingawaje kuna utofauti kama wao wenyewe walivyo na utofauti wa kimaumbile kutokana na Mama zao kuwa na asili tofauti.
Gen 25:18 “These descendants of Ishmael were scattered across the country from Havilah to Shur (which is a little way to the northeast of the Egyptian border in the direction of Assyria)…compare
to 1Samuel 15:7 where Saul 'butchered the Amalekites from Havilah all the way to Shur, east of Egypt’ ..compare
Exodus 17:8 when “the Amalekites came and attacked the Israelites at Rephidim"
Based on these scriptures the ancient 'land of Havilah’ would be located in what is now Saudi Arabia.
Waishmael kutokana na shughuli zao za uchuuzi na biashara ( Merchantalism) ndio waliomnunua Yusufu kutoka kwa wanawayakobo na kwenda kumuuza Misri. Zingatia Waishmael na Waisraeli wakati huo walikuwa wanajuana kabisa kuwahi Babu yao ni mmoja ambaye ni Ibrahim.
Kuhusu ugomvi unaoendelea hapo Palestina, Ibrahim ambaye ndio chanzo kikuu cha mzozo huo yeye alimrithisha Isaka pekeake eneo hilo.
Huku akisahau au kupuuza iwe kwa bahati mbaya au makusudi kuwapa urithi watoto wake wengine akiwepo Ishmael na watoto wa Ketura.
Hii inatupa funzo sisi wababa yakuwa tunapotaka kutoa urithi tusitoe kwa upendeleo kwani inaweza kuleta matatizo.
Ingawaje siku hizi wapo wanaosema Uarabu ni utamaduni na haihusiani na Masuala ya damu, yaani mtu anaweza kufanyiwa assimilation akawa muarabu kwa kuwa na tamaduni za kiarabu. Hiyo inaweza kuwa sawa. Ni kama vile Wayahudi nao wanasheria hiyo ya kumsilimisha mtu asiyemyahudi kuwa MYAHUDI kwa utaratibu maalum. Hata Wafaransa nao walifanya hivyo.
Lakini tukizungumzia Masuala ya vinasaba basi Huwezi kuwa muarabu kama huna vinasaba au damu ya Ishmael. Mama au mama yako akiwa muarabu basi wewe utaitwa muarabu. Halikadhalika na kwa wayahudi na wafaransa na mataifa mengine.
Lakini hiyo ya kusilimishwa, assimilation ni mambo ya kisiasa tuu.
FaizaFoxy, Wairan, Wamedi(Iraq) Waashuru ( Syria) hao sio waarabu. Na sikatai kuwa zipo jamii na jamaa au makabila ya waarabu yanayoishi katika mataifa hayo. Ni kama hapa Tanzania kuna waarabu lakini huwezi sema Watanzania ni waarabu. Pia wapo machotara waliozaliwa.
Taikon acha nipumzike sasa.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam