Mr Alpha
JF-Expert Member
- Jul 31, 2018
- 211
- 584
Kama kuna kosa kubwa wamewahi kulifanya Iran toka kuundwa taifa hilo ni hili la kuishambulia Israel. Hawa Israeli huwa hawanaga shoo ndogo ukiwachokoza uwe umejipanga vya kutosha lazima wakujibu kisawasawa, niwahakikishie tu shambulio la jana HALITAPITA BURE litajibiwa kimkakati mno.
Hatari kubwa ilionao utawala wa Iran ni vuguvugu la mapinduzi ya ndani dhidi ya sheria kali zinazowanyima uhuru na haki raia wengi hususan wanawake ambapo miaka ya karibuni kulizuka wimbi la maandamano kupinga sheria hizo na kifo cha binti Mahsa Amin aliyeuawa na polisi kwa kosa la kutokufunika kichwa. Vuguvugu hilo la ndani ni mtaji kwa Israel, wanaweza kupenya na kufanikiwa kirahisi ajenda zao.
Kitachotokea kwa Iran kama sio mashambulio ya moja kwa moja basi ni hujuma za kimkakati na mipango ya kuangushwa utawala wa Ali Khamenei itaanza.
Kwa wale msiojua, Israeli ndio mabingwa wa ujasusi duniani kuliko hata CIA. Unaambiwa mashariki ya kati wana maajenti wengine mpaka ni wanazuoni wakubwa wa kidini kwenye mataifa ya kiarabu, inasemekana hata kiongozi wa Islamic state Al Baghdad alikua jasusi wao na alibadilika baada ya kupishana maelewano baada ya misheni.
View attachment 2963885
Hatari kubwa ilionao utawala wa Iran ni vuguvugu la mapinduzi ya ndani dhidi ya sheria kali zinazowanyima uhuru na haki raia wengi hususan wanawake ambapo miaka ya karibuni kulizuka wimbi la maandamano kupinga sheria hizo na kifo cha binti Mahsa Amin aliyeuawa na polisi kwa kosa la kutokufunika kichwa. Vuguvugu hilo la ndani ni mtaji kwa Israel, wanaweza kupenya na kufanikiwa kirahisi ajenda zao.
Kitachotokea kwa Iran kama sio mashambulio ya moja kwa moja basi ni hujuma za kimkakati na mipango ya kuangushwa utawala wa Ali Khamenei itaanza.
Kwa wale msiojua, Israeli ndio mabingwa wa ujasusi duniani kuliko hata CIA. Unaambiwa mashariki ya kati wana maajenti wengine mpaka ni wanazuoni wakubwa wa kidini kwenye mataifa ya kiarabu, inasemekana hata kiongozi wa Islamic state Al Baghdad alikua jasusi wao na alibadilika baada ya kupishana maelewano baada ya misheni.
View attachment 2963885