Iran inajiandaa kupiga ndani ya Israel kwa masaa 48 yajayo

Kwann aukimbie kwani yeye ndo katoa taarifa hiyo au imetolewa na shirika lenu pendwa CIA?
Isipo tokea ndo tujaua kuwa CIA ni shirika la kimbea na sio la kijadusi.
USHABADILI GIA ANGANI......KUA SIO SERIKALI YA IRAN ILIYOSEMA NI CIA....🤣🤣🤣🤣
Kweli udini mzigo
 
Ripoti za kiuchunguzi za CIA zinaeleza kuwa Iran inaendelea kujiandaa na mashambulizi ya drones ndani ya Israel hasa kwenye maeneo yake ya viwanja vya ndege na kambi za jeshi...

Wakati haya yakijiri Huko Iran na Israel nao kupitia waziri wa ulinzi bwana GALLANT amesema kuwa "vikosi vyetu vipo tayari na vimejipanga kitambo sana na vita Kwa kujilinda na kupiga"

Naona vita hii inayoendelea inapelekea vita ya 3 ya dunia...tuombe MUNGU Iran asijibu mapigo
MASAA 48 BADO MKUU??
🤣🤣😂😂 Ushakimbia uzi wako
 
Hapo Putin kama hajatoa baraka zake Iran haiwezi kufanya cho chote! Na sidhani kama Putin kwa urafiki alionao na Netanyahu ataruhusu.
Sitarajii kabisa kama Iran watajaribu.
 
Iran hawez mjibu israel kwa kumvamia kutokea tehran. Hapo anatafuta lunch site nzuri nje ya ardhi yake ili dawa iingie vizur na vibaraka wa israel wasifanye chochote.

Israel atapigwa kwa akili sana, wala hakutakua na vita ya 3 ya dunia.
 
Vita ni hesabu, ukikosea hesabu unalambwa kichwa. Kujibu mapigano sio mihemko ya mapenzi.

Na pengine irani hatojibu leo wala kesho kwa mtindo tunaoutaka sisi. Ila kibaraka yeyote wa marekani pale middle east atakabwa koo taratibuu mwisho atajifia mwenyewe.

Irani anamakubaliano ya siri na urusi kuhusu ulinzi na usalama, means chochote anachofanyiwa lazima ashauriane na mrusi coz kikinuka irani basi urusi naye mzigoni, hivyo sio rahisi hivyo
 
Back
Top Bottom