Iramba: Serikali kupitia TARURA yatoa TZS 7bl kufungua barabara

Tajiri la Bitcoin

JF-Expert Member
Apr 9, 2017
1,087
643
IMG-20211216-WA0060.jpg


SERIKALI ya Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imetenga TZS 7.3BL kwa ajili ya kufungua barabara za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida ikiwa ni utekelezaji wa kauli mbiu yake ijulikanayo kama ‘Tunakufungulia barabara kufika kusikofikika’.

Aidha kwa niaba ya Rais Samia akiwa katika ziara ya kikazi wilayani humo,Waziri wa Nchi Ofisi ya Raia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mheshimiwa Ummy Mwalimu amesema azma ya Serikali ni kufungua barabara za vijijini ili wananchi waweza kufanya kazi zao bila kikwazo cha usafiri.

Akikagua barabara ya Shelui - Tintigulu inayojengwa kwa urefu wa kilomita saba, Waziri ameelekeza barabara hiyo ijengwe kwa ubora unaotakiwa ili iweze kudumu na kuwasaidia wananchi wa Shelui katika shughuli zao za kila siku.

"Lengo la Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kuwafungulia wananchi wa vijijini barabara ili isiwe kikwazo tena katika shughuli zao na hapa nimeona baada ya barabara hii kukamilika inakwenda kufungua na kurahisisha mawasiliano ya kata tatu na vijiji sita,"amesema.

Pia Waziri Ummy alimuelekeza Meneja wa TARURA Wilaya ya Shelui, Mhandisi Evance Kibona kuhakikisha kuwa wanafanya usanifu wa Daraja la Nshoka linalounganisha kata za Shelui - Tintigulu ili barabara hiyo inayojengwa iweze kuleta manufaa zaidi kwa wananchi wa maeneo hayo.

"Nimekagua ujenzi wa barabara, umeanza lakini nimeona kuna mto Nshoka ambao unatakiwa kujengewa daraja ili barabara hii inayojengwa iweze kuleta manufaa, vinginevyo bado watakuwa wanapata usumbufu wakati wa mvua nataka tumalize kabisa changamoto hii.

"Mto huu ni mkubwa na hakuna daraja sasa wakati wa mvua wananchi hawawezi kupita hapa hivyo ni vyema hapa pakajengwa daraja ili barabara hii iwe na tija stahiki, hivyo wahandisi anzeni kufanya usanifu na muingize kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2022|23 tuweke ujenzi wa daraja hili kwenye bajeti yetu.

Akizungumza wakati wa ukaguzo wa barabara hiyo ya Shelui-Tintigulu Meneja wa TARURA Wilaya ya Iramba, Mhandisi Evance Kibona amesema, ujenzi wa barabara hiyo umeanza Desemba 11 na utakamilika Juni,2022.

Wilaya ya Iramba ilikuwa na majimbo mawili ya Iramba mashariki|Mkalama na Iramba magharibi kabla ya Mkalama kuwa Wilaya, Jimbo la Iramba Magh linaloongozwa na Waziri wa fedha na Mipango Dkt Mwigulu Nchemba,Iramba Kaziiendelee
 
View attachment 2052042

SERIKALI ya Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imetenga shilingi bilioni 7.3 kwa ajili ya kufungua barabara za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida ikiwa ni utekelezaji wa kauli mbiu yake ijulikanayo kama ‘Tunakufungulia barabara kufika kusikofikika’.

Aidha kwa niaba ya Rais Samia akiwa katika ziara ya kikazi wilayani humo,Waziri wa Nchi Ofisi ya Raia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mheshimiwa Ummy Mwalimu amesema azma ya Serikali ni kufungua barabara za vijijini ili wananchi waweza kufanya kazi zao bila kikwazo cha usafiri.

Akikagua barabara ya Shelui - Tintigulu inayojengwa kwa urefu wa kilomita saba, Waziri ameelekeza barabara hiyo ijengwe kwa ubora unaotakiwa ili iweze kudumu na kuwasaidia wananchi wa Shelui katika shughuli zao za kila siku.

"Lengo la Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kuwafungulia wananchi wa vijijini barabara ili isiwe kikwazo tena katika shughuli zao na hapa nimeona baada ya barabara hii kukamilika inakwenda kufungua na kurahisisha mawasiliano ya kata tatu na vijiji sita,"amesema.

Pia Waziri Ummy alimuelekeza Meneja wa TARURA Wilaya ya Shelui, Mhandisi Evance Kibona kuhakikisha kuwa wanafanya usanifu wa Daraja la Nshoka linalounganisha kata za Shelui - Tintigulu ili barabara hiyo inayojengwa iweze kuleta manufaa zaidi kwa wananchi wa maeneo hayo.

"Nimekagua ujenzi wa barabara, umeanza lakini nimeona kuna mto Nshoka ambao unatakiwa kujengewa daraja ili barabara hii inayojengwa iweze kuleta manufaa, vinginevyo bado watakuwa wanapata usumbufu wakati wa mvua nataka tumalize kabisa changamoto hii.

"Mto huu ni mkubwa na hakuna daraja sasa wakati wa mvua wananchi hawawezi kupita hapa hivyo ni vyema hapa pakajengwa daraja ili barabara hii iwe na tija stahiki, hivyo wahandisi anzeni kufanya usanifu na muingize kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2022/23 tuweke ujenzi wa daraja hili kwenye bajeti yetu.

Akizungumza wakati wa ukaguzo wa barabara hiyo ya Shelui-Tintigulu Meneja wa TARURA Wilaya ya Iramba, Mhandisi Evance Kibona amesema, ujenzi wa barabara hiyo umeanza Desemba 11 na utakamilika Juni,2022.
Aise kila kona ya nchi kuna mradi mpya wa Rais Samia unaendelea,

Huyu mama atawala mpaka achoke aise
 
Back
Top Bottom