IPhone 6 Plus na Kashfa ya Bentgate

ManiTek TV

JF-Expert Member
Jun 3, 2011
410
159
[h=1]IPHONE 6 PLUS NA KASHFA YA BENTGATE[/h]
  • user.png
    By Mwandishi Wetu
  • date.png
    16:37
  • comments.png
    0 comments
  • tungs.png
    iPhone, Mwanzo, Simu, Uchambuzi Wetu


iPhone 6 Plus jinsi inavyopinda
Amini usiamini Apple bila ya kukusudia wametoa simu inayopinda! Simu hiyo pamoja na ndogo yake yaani iPhone 6 tayari inarajiwa kuongoza kwa mauzo baada ya kuuza simu milioni 10 kwa muda wa wikiendi moja tu, Watumiaji wa Phone 6 Plus wamekuwa wakililalamikia jambo hili kwenye mitandao ya kijamii. iPhone 6 Plus ambayo ina kioo chenye ukubwa wa inchi 5.5 huku ikiwa na wembamba wa 7.1 mm ni moja kati fableti (simu kubwa) nyembamba mno.



Kabla ya kuichambua kashfa hii kwanza tulinganishe wembamba wa iPhone 6 Plus na simu zinazofanana au kukaribiana na kwa ukubwa na simu hii. Samsung Galaxy note 4 ambayo ina skioo chenye ukubwa wa inchi 5.7 ni pana kuliko iPhone 6 Plus kwa 1.3 mm nzima ikiwa na upana wa inchi 8.4mm, nayo Samsung Galaxy Note 4 Edge nayo ina upana sawa na Galaxy Note 4. Nokia Lumia 1520 yenye skrini yenye ukubwa wa inchi 6 ni pana zaidi ya iPhone 6 kwa 1.6 mm ikiwa na upana wa 8.7mm. Nayo LG G Flex yenye kioo chenye ukubwa wa inchi sita nayo ina upana sawa na Nokia Lumia 1520. Ukitaka kutambua jinsi simu hii ilivyo nyembamba hata Samsung Galaxy S5 ambayo ni ndogo kuliko iPhone 6 Plus inaizidi iPhone hii upana kwa 1 mm nzima.



Sababu ya uchambuzi huu wa mlinganyo wa wembamba ni kuwa tunaamini kuwa wembamba wa iPhone 6 Plus ukilinganisha na ukubwa basi unachangia kuwepo kwa udhaifu hii kwenye simu hii ukizingatia ukubwa wake. iPhone 6 ambayo ina kioo chenye ukubwa wa inchi 4.7 haikuripotiwa kuwa na tatizo hili.


Kupinda kwa iPhone 6 Plus ambako kumepewa hashtag ya bentgate (#bentgate) kunatokea unapoikalia simu yako ukiiweka mfuko wa nyuma wa suruali, pia wako wanaodai kuwa simu zao zimepinda zikiwa mfuko wa mbele bila ya hata kuikali. Simu hii imetengenezwa ikiwa na gamba la madini ya aluminium.

Wakati habari za kupinda kwa simu hii zinasambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii, blogu za teknolojia na hata mashirika rasmi ya habari kama vile BBC, Apple bado hawakutoa kauli yoyote rasmi kutokana na tatizo hili.


Wadau wa mtandao wa Unbox Therapy walijaribu kuipinda simu hii kwa makusudi wamepatwa na ย“msibaย” kwani baada ya kutaka kuinyosha wanadai iPhone 6 Plus ilivunjika kioo na pia kukatika fremu kwa upande wa kushoto chini ya vifungo vya kuzidisha na kupunguza sauti. Hata hivyo wadau hao walijaribu kupinda Galaxy Note 3 ambayo ilipinda kwa kiasi kidogo sana ukilinganisha na iPhone 6 Plus, hata hivyo Samsung hii imetengenezwa ikiwa na gamba la plastiki. Ni vigumu kuthibitisha nguvu walizotumia kuipinda iPhone 6 Plus ukilinganisha na Samsung Galaxy Note 3, hata hivyo mdau huyo wa Ungox Therapy Norm Uhl alidai kutumia nguvu zaidi katika jaribio lake la kuipinda Samsung Galaxy Note 3, hata video inaonyesha akiwa katika hali hiyo. Ikiwa Norm Uhl ni mkweli angalau sasa tunajua kwamba simu za plastiki nazo zina faida yake.



Chanzo:gajetek habari
 
Its a shame, that that's happening. Though being an Android fan, I do appreciate Apple's hardware standards. Its funny since most of Android fans specially Samsung's would like to have metal phones. Now that this happened, this will be interesting to see how it unfolds and what apple will say about it. Good read and kudos my friend for the Swahili gadget website. Always wanted to see one like that.
 
Its a shame, that that's happening. Though being an Android fan, I do appreciate Apple's hardware standards. Its funny since most of Android fans specially Samsung's would like to have metal phones. Now that this happened, this will be interesting to see how it unfolds and what apple will say about it. Good read and kudos my friend for the Swahili gadget website. Always wanted to see one like that.

A Few days before release of i phone 6 , apple's engineer was demonstrating about sapphire glass which was expect to come with phone 6 . Sapphire glass is one of very strong material and cannot be broken easily . I wonder why they are so vulnerable like that
 
kupinda ikiwa kwenye mfuko wa mbele ni propaganda! hata hii kukatika imetokea katika weakest point ambapo ni kwenye button za volume ambapo kutokana na wembamba wa simu lazima ipinde. kwa matumizi ya kawaida tu si rahisi kuikunja hiyo simu, na wala kukunjika kwake hakuathiri soko la apple, ni sisi wachache tu ambao hatujapendezewa na design hii kwa ujumla.
 
A Few days before release of i phone 6 , apple's engineer was demonstrating about sapphire glass which was expect to come with phone 6 . Sapphire glass is one of very strong material and cannot be broken easily . I wonder why they are so vulnerable like that

nadhani 6s itakuwa na safire!
 
A Few days before release of i phone 6 , apple's engineer was demonstrating about sapphire glass which was expect to come with phone 6 . Sapphire glass is one of very strong material and cannot be broken easily . I wonder why they are so vulnerable like that

Sapphire is quite expensive. It would have driven the costs quit higher, and the Chinese companies that manufacturer iphones would be able to meet the deadlines. But I think apple will apply Sapphire in their Apple Watch!!
 
Nilichokuwa nashangaa ni kwa nini hawakufanya pilot testing ya hii simu kabla ya kuiachia sokoni.
Nadhani hii matatizo iliyojitokeza sasa would have been avoided mapema
 
Nilichokuwa nashangaa ni kwa nini hawakufanya pilot testing ya hii simu kabla ya kuiachia sokoni.
Nadhani hii matatizo iliyojitokeza sasa would have been avoided mapema

The disadvantages of 'Mass Production'. Naamini walifanya Testing, lakini siamini kama walifanya kwa Unit Million 4 na zaidi. Wana stress test Macbook zote, na kuhakikisha hazi bend to a point of breaking. Either way, I'm an Android fan, so now I have something to poke fun to Apple fans.
 
A Few days before release of i phone 6 , apple's engineer was demonstrating about sapphire glass which was expect to come with phone 6 . Sapphire glass is one of very strong material and cannot be broken easily . I wonder why they are so vulnerable like that

Sapphire glass was not used on any of the iPhone screen, it has only been used on the camera lens. Probably next year iPhones 6 S snd 6 Plus S.
 
Well, iPhone 6 sio simu ya kwanza kupinda, nashangaa kwanini watu wanaiongelea sana...

Kama unataka kununua au kama unayo, wala usivunjike moyo, kwanza nashindwa kuelewa how will you apply that much pressure mpaka simu yako ipinde?, unless kama umekusudia, kama alivyofanya yule jamaa wa youtube, kwasababu alikusudia kuipindisha... Check out these videos For more info.

[video=youtube_share;s3QcOSyD38M]http://youtu.be/s3QcOSyD38M[/video]
 
Its a shame, that that's happening. Though being an Android fan, I do appreciate Apple's hardware standards. Its funny since most of Android fans specially Samsung's would like to have metal phones. Now that this happened, this will be interesting to see how it unfolds and what apple will say about it. Good read and kudos my friend for the Swahili gadget website. Always wanted to see one like that.

Mkuu bana hiyo sentensi yako ya mwisho tu..umeandika kiingereza kukisifia kiswahili
 
The disadvantages of 'Mass Production'. Naamini walifanya Testing, lakini siamini kama walifanya kwa Unit Million 4 na zaidi. Wana stress test Macbook zote, na kuhakikisha hazi bend to a point of breaking. Either way, I'm an Android fan, so now I have something to poke fun to Apple fans.

Sure na Apple wameongelea kuwa ni wateja tisa tuu waliokutana na janga hilo ambao pia watafidiwa kwa kupewa nyingine
 
Hii simu ni nzuri. Hayo mambo ya kupinda ni kashfa tu iliyoshikiwa bango. Watu kibao wamejaribu kuipindisha wameshindwa.
Jana nimeangalia BBC na hata CNN kwamba labda wahitaji kuwa body builder kupindisha simu hii. Lakini kwa matumizi ya kawaida tu utafanya nini mpaka uipindishe? Au uwe kichaa kama wale wanaoziweka simu mpya kwenye microwave. Off course wazungu wanafanya hivyo kujenga majina tu!!!
Hata hivyo kwanini uweke simu mfuko wa nyuma? Funguo tu ya gari hatuweki mfuko wa nyuma, sembuse simu? Kwanza mifuko midogo kuweka simu za sasa.
 
Sapphire glass was not used on any of the iPhone screen, it has only been used on the camera lens. Probably next year iPhones 6 S snd 6 Plus S.

So we should wait 6s and 6s plus?
Is this acquired trend already?
 
So we should wait 6s and 6s plus?
Is this acquired trend already?
This is purely my guess that the next generation iPhone may have Sapphire glass. Please don't take my word for it. Sapphire glass is still pretty expensive so Apple may or may not use next year. Not only that it is still very expensive but as well the production is yet to meet the demand.

However I believe 100% that eventually sapphire glass will be used in mobile phone display.
 
Sapphire is quite expensive. It would have driven the costs quit higher, and the Chinese companies that manufacturer iphones would be able to meet the deadlines. But I think apple will apply Sapphire in their Apple Watch!!

Apple iliwapatia GT Advanced Tech zaidi ya $500M kwa ajili ya kujenga furnace Arizona, Im pretty sure the next iPhone will be rocking a sapphire glass, hasa ukizingatia weakness (?) iliyoonekana kwenye iPhone 6+, they will need a major upgrade to keep the lead!
 
Apple shouldn't have used an all Aluminum chasis. Other phones with Aluminum bodies, use magnesium chasis. HTC has done since the HTC one. I think Apple was a Lil arrogant on this one, not having to stress test the phone like the do with all the Macbook's. But then again, the iPhone 6 is not the only phone that bent once torque was applied to it. I guess the reason Apple's #bendgate is getting such notoriety is because people expect a certain premium quality with Apple's manufacturing. I am an Android fan by software but I've always being a fan of Apple's hardware!
 
Propaganda hapana chezea apple sim haiwekwi mfukonwa nyuma.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom