Inawezekana Vipi Zanzibar Kuna Div I, Div II, na Div III Chache, Ila Div IV na Div Zero Nyingi?!.

Wanabodi,
Nimekuwa nikipitia matokeo ya form four kwa baadhi ya shule za Zanzibar, kwa shule nyingi nilizopitia, nimeshangazwa kukuta Div I, Div II, na Div III ni chache sana!, kule zimejazana zaidi Div IV na Zero kiasi kwamba kuna baadhi ya shule, shule nzima imepata Div 0!, hii inakuwaje?!. Jee kuna uwezekano kuna tofauti ya akili kati ya Watanzania Bara na Watanzania Visiwani?.

Set up ya baadhi ya taasisi za muungano, zinalazimisha kwenye top management, kama ni bara, deputy, lazima atoke Zanzibar!, moja ya taasisi hizi ni BOT, Gavana akitoka bara, Deputy lazima atoke Zanzibar!, lakini kwa miaka mingi, ile nafasi ilikaa wazi kwa kisingizio kuwa hakukuwa na Mzanzibar mwenye sifa, nilipouliza sifa gani, nikaelezwa lazima awe mchumi aliobobea kwa uzoefu usiopungua miaka 10!. Mimi nilidhani ni visingizio tuu, lakini kama matokeo ya wenzetu hawa ndio haya, na Tanzania ni nchi ya muungano, linapokuja suala la recruitment professionals wa muungano, itakuwaje?!.

Nimebahatika kusoma na kijana mmoja wa Kizanzibari pale UD, ile tumeingia tuu mwaka wa kwanza, kwa fedha za boom, alioa mke wa kwanza, mwaka wa pili akaoa mke wa pili!, mwaka wa tatu akaoa mke wa tatu!, tulipomaliza mwaka wa 4, alisema anakwenda kukamilisha idadi ya mwisho 4, ila kiukweli jamaa alikuwa fit sana upstairs, bado sipati jibu, ikiwa ni kweli Zanzibar ina Div I, Div II, na Div III, chache, hii itakuwa imekaaje kimuungano!. Jee kuna uwezekano kuna tofauti ya akili kati ya Watanzania Bara na Visiwani?!.

Ikithibitika ni makosa ya utungaji mitihani ambayo "sio", usahihisaji au upangaji matokeo, then yule mama wa NECTA, atakuwa hana jinsi, lazima awajibike akitanguliwa na waziri wake!.
Pasco.
Kwa masikitiko makubwa naomba kuwauliza wenzetu wa Zanzibar swali ambalo kwa kweli limekuwa likinitatiza miaka mingi sana. Nalo ni udhaifu mkubwa sana wa taaluma ya Zanzibar ndani ya baraza la mitihani NECTA.

Cha ajabu kabisa ni kuwa, wakati Zanzibar hiyo ikiwa hoi mbele ya NECTA, wapo Wazanzibar wengi sana ambao ni wana vipaji vya hali ya juu sana mfano kina Mohamed Gharib Bilal na wengine wengi sana. Hawa wana vichwa vilivyojaa vipaji.

Katika matokeo ya kidato cha sita ACSEE-2016 Unguja pekee imetoa shule saba kati ya kumi za mwisho, nini tatizo?



Siongelei kuhusu swala la ghafla bin vuu shule kongwe za serikali za vipaji kurudi kwenye chati maana hilo linahitaji uchambuzi wake. Ni wachache watakaoamini kuwa shule zote kongwe za serikali za vipaji kurudi "top ten" kwa kishindo kumetokana na jitihada binafsi za wanafunzi. Shule zote nne? Hapana! Hili tutakuja kulichambua baadaye! Kwanza niwaulize hawa watani zetu, nini tena kimewapata?

Shule 10 zilizofanya vibaya:

1.Mpendae-Unguja
2.Ben Bella-Unguja
3.Tumekuja-Unguja
4.Green Bird Boys-Kilimanjaro
5.Jang'ombe-Unguja
6.Kiembe Samaki-Unguja
7.Tanzania Adventist-Arusha
8.Al- Ishan Girls-Unguja
9.Azania-Dar es Salaam
10.Lumumba-Unguja
 
Pasco,
Usipindishe hoja na kuharibu mjadala. Umeanza vema kwa kuonesha shida ya matokeo kwa shule za Zanzibar (matoke ambayo ni mabaya kwa nchi nzima), hilo liko sawa. Sasa kama Zanzibar wamefeli 'zaidi', huyu mwanamama anahusikaje na usahihishaji? Kama syllabus inayotumika Zenji na bara ni moja, kwa nini Ndalichako alaumiwe linapokuja suala la wanafunzi kufeli mitihani? Nimesoma na Wazanzibari kwa miaka mingi tu bara, tangu sekondari, wako vema sana upstairs kama walivyo wanafunzi wengine. Inawezekana kuna mazingira flani ambayo si 'wezeshi' kwa upande wa visiwani Zanzibar ambayo yanafanya performance ya wanafunzi iwe chini, lakini sio shida ya usahihishaji! Tujipe homework ya kuangalia shida ilipo kwanza, kabla ya kunyosheana vidole!
Katika matokeo ya kidato cha sita ACSEE-2016 Unguja pekee imetoa shule saba kati ya kumi za mwisho, nini tatizo?
Shule 10 zilizofanya vibaya:

1.Mpendae-Unguja
2.Ben Bella-Unguja
3.Tumekuja-Unguja
4.Green Bird Boys-Kilimanjaro
5.Jang'ombe-Unguja
6.Kiembe Samaki-Unguja
7.Tanzania Adventist-Arusha
8.Al- Ishan Girls-Unguja
9.Azania-Dar es Salaam
10.Lumumba-Unguja
 
Jee kuna uwezekano matokeo mabaya ya Zanzibar na shule za dini fulani yanahusiana na imfluence ya dini hiyo kwenye akili za waumini?!, au ni imfluence ya Waarabu?!.

Pasco

Dini ku-influence matokeo ya darasani ni swali muhimu.
Lakini tujiulize, vipi Irani, Egypt, Algeria, Saudi Arabia na maeneo mengine duniani ambako wakazi wengi ni wa 'dini' hiyo, hali ya elimu ya kimagharibi ikoje?

Kuhusu Zanzibar, maoni yangu ni kwamba kuna mgongano mkubwa kati ya imani za kitamaduni za wazanzibari na imani za 'dini'. Mgongano huu wa imani hizi ni kama umepea zaidi kwenye imani potofu zinazofifisha ustawi wa jamii badala ya kuzamia kwenye imani chanya zinazohanikiza maendeleo.

Ni jukumu la 'scholars' wa dini na scholars wa sayansi ya ustawi wa jamii kuwakwamua Wazanzibari hapa walipokwama.
 
Sometimes tusiwe tuanjiuliza na hali ipo wazi tuu, kuna MTU kacoment why shule za kikristo zinafaurisha, ebu nenda katika izo shule ukajionee elimu inavotiliwa mkazo then wakati huo huo nenda Muslim seminary ukaone kinachotiliwa mkazo ni mafunzo ya dini au ya elimu then uje useme unategemea shule zipi zitafaurisha zaid, ingawa zipi shule za kiristo ambazo nazo wanakazia zaid mafunzo ya kidin ambapo matokeo take mfano wake ni iyo shule ya kisabto ya arusha ilyo top ten za mwisho. Point ni kwamba usitegemee kupanda majani ukavuna mahind, kama unawafundisha watoto dini mtiani ukaja wakatolewa elimu dunia unategema watafaulu?
 
Iyo shule ya wasabato arusha nasikia jamaa hata majani ya chai hawatumii wala soda,wapo busy na dini sana! Wanatakiwa wabalance kati ya mafundisho ya dini na elimu za humu dunia pia.Likewise shule za unguja la sivyo wasubirie jecha afute matokeo
 
Wanafunzi wako vizuri ila SMZ iangalie jinsi ya kuboresha maslahi ya walimu Zenji au ikiwezekana Wizara ya elimu iwe ya muungano, wafanyakazi wa SMZ wanalipwa mishajara midogo mno ukilinganisha na wale walio katika taasisi za Muungano
 
Iyo shule ya wasabato arusha nasikia jamaa hata majani ya chai hawatumii wala soda,wapo busy na dini sana! Wanatakiwa wabalance kati ya mafundisho ya dini na elimu za humu dunia pia.Likewise shule za unguja la sivyo wasubirie jecha afute matokeo
Wanakunywa mtundula...
 
Dini ku-influence matokeo ya darasani ni swali muhimu.
Lakini tujiulize, vipi Irani, Egypt, Algeria, Saudi Arabia na maeneo mengine duniani ambako wakazi wengi ni wa 'dini' hiyo, hali ya elimu ya kimagharibi ikoje?

Kuhusu Zanzibar, maoni yangu ni kwamba kuna mgongano mkubwa kati ya imani za kitamaduni za wazanzibari na imani za 'dini'. Mgongano huu wa imani hizi ni kama umepea zaidi kwenye imani potofu zinazofifisha ustawi wa jamii badala ya kuzamia kwenye imani chanya zinazohanikiza maendeleo.

Ni jukumu la 'scholars' wa dini na scholars wa sayansi ya ustawi wa jamii kuwakwamua Wazanzibari hapa walipokwama.
mkuu umenena
 
Mimi ni mwl wa chuo kikuu nchini zaidi ya miaka 20. Nimewafundisha wanafunzi kutoka zanzibar. Wengi ni dhaifu sana kwenye masomo. Usiombe upate mwanafunzi wa ku supervise dissertation, hapo ndipo utakapojua uzito wa kazi hiyo. Tuseme kweli wengi ni wadhaifu hata wale waliomaliza na GPA nzuri ktka degree ha kwanza.
 
Mimi ni mwl wa chuo kikuu nchini zaidi ya miaka 20. Nimewafundisha wanafunzi kutoka zanzibar. Wengi ni dhaifu sana kwenye masomo. Usiombe upate mwanafunzi wa ku supervise dissertation, hapo ndipo utakapojua uzito wa kazi hiyo. Tuseme kweli wengi ni wadhaifu hata wale waliomaliza na GPA nzuri ktka degree ha kwanza.
Duuuh shida kweli kweli, kipi kifanyike ili hawa watu wanyanyuke kielimu
 
Kwanza umepotosha kutokana na kichwa cha habari hapo juu,then znz kuna div 1 na 2 nyingi tu tena za science,pia znz kuna shule znz zina matokeo mazuri mara 10 kuliko ya bara..fanya research kwanza ndio uandike sio unakurupuka tuu
 
Back
Top Bottom