Kwa kuwa wewe unajua katiba na chain of command, gombea urais ,2025. Kura yangu na watanzania wenye mawazo kama yako unazo.Mahojiano aliyofanya CDF Mstaafu Venance Mabeyo yamenifundisha kitu.
Nchi hii tuna shida kubwa sana ya watu kuwa kwenye nafasi za juu za maamuzi na uongozi ambao hawastahili kuwepo kwenye nafasi hizo kwa kukosa uwezo.
Hivi inakuwaje kwenye nchi tena yenye miaka zaidi ya 60 ya uhuru watu kwenye nafasi za juu kabisa za maamuzi hawajui kuwa kwenye chain of Command baada ya Rais ni Makamu wa Rais?
Hivi inakuwaje Rais anafariki wa kwanza kutarifiwa ni Mkuu wa Majeshi na sio Makamu wa Rais?
Inakuwaje na Mkuu wa Majeshi anaingia Kuanza kusema nimfaarifu Waziri Mkuu au Katibu Mkuu Kiongozi na sio Makamu wa Rais?
Inakuwaje tuna viongozi kwenye nafasi za juu kabisa ambao hawajui hata Katiba ya Nchi inasemaje?
How comes wanaotuongoza hawaijui Katiba?
Kituko zaidi ni mtu aliyefika hadi kuwa Rais wa Nchi anaamuru Mkuu wa Majeshi aamuru atolewe hospitali na kupelekwa kijijini kwake?
Hivi alikuwaje Rais na hajui hata mipaka ya madaraka na uongozi?
Kusema kweli tuna tatizo kubwa kwenye hii nchi na hii ni kansa ambayo kusema kweli itatutafuna na kutumaliza kabisa.