Leo nimeona kituko hapa arusha. Kuna jengo linajengwa na NSSF hapa maeneo ya round about ya Florida. Hapa kuna njia inakatiza kwenda maeneo ya kaloleni na soweto gargen. Sasa imefungwa kwa kuwa kampuni inayojenga hilo jengo wemejaza material yote ya ujenzi barabarani na kuweka kibao kuwa barabara imefungwa kwa muda. Sasa najiuliza hilo jengo ni kama la gorofa 20 hivi na ndio liko kwenye foundation, sasa barabara itafungwa mpaka lini? na je watu wanaokaa eneo hilo watapata usumbufu kiasi gani? na je mtu aliyetoa bulding permit hakuweza kujua kwamba pale hakutakuwa na sehemu kwa ajili ya kuweka building materials? Unaomba ufafanuzi wa wana body. Nawakilisha