Mkwawa
JF-Expert Member
- Jun 8, 2011
- 1,334
- 1,464
Hatimaye mahakama ya Igunga inayosikiliza kesi ya kupinga matokeo ya Ubunge Igunga inazidi kuwa ngumu baada ya habari kuwa waziri wa barabara nk kukataa kufika mahakamani kutoa ushahidi.
Magufuli anatakiwa mahakani kudhibitisha au kukanusha ahadi alizotoa kama waziri wakati wa uchaguzi. Kama mahakama itaridhia kufuta matokeo ya uchaguzi itailazimu tume ya taifa ya uchaguzi kuita uchaguzi upya.
Chaguzi zinagharama kubwa sana na zinakuwa ni za walipa kodi.
Katiba mpya lazima ingeweka hivi mapingamizi yote yasikilizwe kabla ya kutangazwa kwa mshindi ili kama kuna matatizo yaamuliwe na haki itendeke mapema na kama kuna kesi ifunguliwe ili kama kuna kasoro zirekebishwe na mshindi atangazwe bila kurudia uchaguzi.
Na vile vile makosa yawekwe bayana na kama ni ya kichama yaani ni matatizo ya wapiga debe chama kigharamie gharama zote za uchaguzi kwa uzembe wa kutumia watu wasio makini na janga kwa Taifa.
Igunga huenda uchaguzi ukarudiwa na hii itaonyesha matumizi mengine ya fedha za walipa kodi.
Je uchaguzi ukirudiwa tena mbwembwe za awali zitarudiwa ?? bastola, vituko vya wakuu wa wilaya, matumizi makubwa ya fedha lugha za matusi, dharau na minengua ya ajabu tutaviona??? Ahadi zile zile na kutekwa watu, kuumizwa na kuuliwa vitarudiwa tena???
wananchi wako roho juu roho chini. Tisa kumi uchaguzi unanukia kurudiwa huku Kafumu akiachwa haamini. Usichanganye siasa chafu na elimu haviendani.
Magufuli anatakiwa mahakani kudhibitisha au kukanusha ahadi alizotoa kama waziri wakati wa uchaguzi. Kama mahakama itaridhia kufuta matokeo ya uchaguzi itailazimu tume ya taifa ya uchaguzi kuita uchaguzi upya.
Chaguzi zinagharama kubwa sana na zinakuwa ni za walipa kodi.
Katiba mpya lazima ingeweka hivi mapingamizi yote yasikilizwe kabla ya kutangazwa kwa mshindi ili kama kuna matatizo yaamuliwe na haki itendeke mapema na kama kuna kesi ifunguliwe ili kama kuna kasoro zirekebishwe na mshindi atangazwe bila kurudia uchaguzi.
Na vile vile makosa yawekwe bayana na kama ni ya kichama yaani ni matatizo ya wapiga debe chama kigharamie gharama zote za uchaguzi kwa uzembe wa kutumia watu wasio makini na janga kwa Taifa.
Igunga huenda uchaguzi ukarudiwa na hii itaonyesha matumizi mengine ya fedha za walipa kodi.
Je uchaguzi ukirudiwa tena mbwembwe za awali zitarudiwa ?? bastola, vituko vya wakuu wa wilaya, matumizi makubwa ya fedha lugha za matusi, dharau na minengua ya ajabu tutaviona??? Ahadi zile zile na kutekwa watu, kuumizwa na kuuliwa vitarudiwa tena???
wananchi wako roho juu roho chini. Tisa kumi uchaguzi unanukia kurudiwa huku Kafumu akiachwa haamini. Usichanganye siasa chafu na elimu haviendani.