nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Na Chalila Kibuda
KAMPUNI ya East African Meat ambayo mwenyekiti wake wa bodi alikuwa Waziri wa zamani wa Viwanda na Biashara, Idd Simba, inatuhumiwa kuchota na kutumia vibaya mabilioni ya shilingi zilizokuwa zitumike kwa ajili ya ujenzi wa machinjio ya kisasa jijini Dar es Salaam.
Ubadhirifu huo wa kutisha umegunduliwa jana na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) ilipokutana na uongozi wa Manispaa ya Kinondoni, ambapo hata matumizi ya kiwanja kilichokuwa kijengwe machinjio hayo yamebadilishwa.
Mwenyekiti wa LAAC, Augustine Lyatonga Mrema, alisema fedha hizo zilitolewa na Manispaa ya Ilala sh mil. 364, Kinondoni sh mil. 223, Temeke sh mil. 224 huku Halmashauri ya Jiji ikichangia zaidi ya sh bilioni moja.
Mrema alisema kuwa watu wanaotuhumiwa kuchota fedha hizo ni viongozi makini ambao pia wanatajwa kuwamo katika sakata la Shirika la Usafiri Mkoa wa Dar es Salaam (UDA).
Mrema alisema fedha hizi ni nyingi, na zingeweza kufanya kazi nyingine kwa ajili ya kuwahudumia wananchi lakini matokeo yake zimekwenda kwa wajanja wachache.
Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi, alikiri kutoweka kwa fedha hizo na kudai kuwa zilikusanywa chini ya Idd Simba, ambaye alikuwa mwenyekiti wa bodi ya kampuni hiyo.
Hata hivyo, Masaburi alisema kampuni ambayo ilitatakiwa kuendesha machinjio hayo ilikwisha kufilisika kabla ya kuanza ujenzi huo na wanaotakiwa kuhojiwa ni waliokuwa watendaji na wajumbe wa bodi ya kampuni hiyo.
Waziri huyo wa zamani anatuhumiwa pia kuhusika na sakata ya uuzaji wenye utata wa Shirika la Usafiri la UDA ambapo inadaiwa kuwa fedha za mauzo ya shirika hilo ziliingizwa katika akaunti yake binafsi kinyume cha uuzaji wa mashirika ya umma.
Akionesha kukerwa na ubadhirifu huo mkubwa, Mrema alisema suala hilo
litafikishwa katika kikao cha Bunge lijalo kwa kuwashirikisha Waziri Mkuu na Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
"Nashangaa wanaotuhumiwa na wizi huu ni viongozi wa siku nyingi na wengine wanatuhumiwa katika sakata la Shirika la Usafiri Dar es Salaam, lakini wanaendelea kudunda bila kuchukuliwa hatua kali za kisheria," alisema Mrema.
Alisema kamati yake inaangalia namna ya kuchukua hatua kali ikiwamo kuagiza kukamatwa kwa wahusika na kufikishwa katika vyombo vya dola kwa hatua za uchunguzi na kisha kuwafikisha mahakamani wale wote watakaobainika kuhusika moja kwa moja na ubadhirifu huo.
Katika hatua nyingine, kamati hiyo ya Bunge imeubana vikali uongozi wa Manispaa ya Kinondoni kwa kuingia katika mkataba wenye utata na Oysterbay Villa ambao wamemilikishwa milele kinyume cha sheria za nchi.
Makamu Mwenyekiti wa LAAC, Idd Azzan, alisema kuwa waliohusika na mkataba wa aina hiyo na mingine isiyo na masilahi kwa taifa lazima wachukuliwe hatua za kisheria.
KAMPUNI ya East African Meat ambayo mwenyekiti wake wa bodi alikuwa Waziri wa zamani wa Viwanda na Biashara, Idd Simba, inatuhumiwa kuchota na kutumia vibaya mabilioni ya shilingi zilizokuwa zitumike kwa ajili ya ujenzi wa machinjio ya kisasa jijini Dar es Salaam.
Ubadhirifu huo wa kutisha umegunduliwa jana na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) ilipokutana na uongozi wa Manispaa ya Kinondoni, ambapo hata matumizi ya kiwanja kilichokuwa kijengwe machinjio hayo yamebadilishwa.
Mwenyekiti wa LAAC, Augustine Lyatonga Mrema, alisema fedha hizo zilitolewa na Manispaa ya Ilala sh mil. 364, Kinondoni sh mil. 223, Temeke sh mil. 224 huku Halmashauri ya Jiji ikichangia zaidi ya sh bilioni moja.
Mrema alisema kuwa watu wanaotuhumiwa kuchota fedha hizo ni viongozi makini ambao pia wanatajwa kuwamo katika sakata la Shirika la Usafiri Mkoa wa Dar es Salaam (UDA).
Mrema alisema fedha hizi ni nyingi, na zingeweza kufanya kazi nyingine kwa ajili ya kuwahudumia wananchi lakini matokeo yake zimekwenda kwa wajanja wachache.
Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi, alikiri kutoweka kwa fedha hizo na kudai kuwa zilikusanywa chini ya Idd Simba, ambaye alikuwa mwenyekiti wa bodi ya kampuni hiyo.
Hata hivyo, Masaburi alisema kampuni ambayo ilitatakiwa kuendesha machinjio hayo ilikwisha kufilisika kabla ya kuanza ujenzi huo na wanaotakiwa kuhojiwa ni waliokuwa watendaji na wajumbe wa bodi ya kampuni hiyo.
Waziri huyo wa zamani anatuhumiwa pia kuhusika na sakata ya uuzaji wenye utata wa Shirika la Usafiri la UDA ambapo inadaiwa kuwa fedha za mauzo ya shirika hilo ziliingizwa katika akaunti yake binafsi kinyume cha uuzaji wa mashirika ya umma.
Akionesha kukerwa na ubadhirifu huo mkubwa, Mrema alisema suala hilo
litafikishwa katika kikao cha Bunge lijalo kwa kuwashirikisha Waziri Mkuu na Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
"Nashangaa wanaotuhumiwa na wizi huu ni viongozi wa siku nyingi na wengine wanatuhumiwa katika sakata la Shirika la Usafiri Dar es Salaam, lakini wanaendelea kudunda bila kuchukuliwa hatua kali za kisheria," alisema Mrema.
Alisema kamati yake inaangalia namna ya kuchukua hatua kali ikiwamo kuagiza kukamatwa kwa wahusika na kufikishwa katika vyombo vya dola kwa hatua za uchunguzi na kisha kuwafikisha mahakamani wale wote watakaobainika kuhusika moja kwa moja na ubadhirifu huo.
Katika hatua nyingine, kamati hiyo ya Bunge imeubana vikali uongozi wa Manispaa ya Kinondoni kwa kuingia katika mkataba wenye utata na Oysterbay Villa ambao wamemilikishwa milele kinyume cha sheria za nchi.
Makamu Mwenyekiti wa LAAC, Idd Azzan, alisema kuwa waliohusika na mkataba wa aina hiyo na mingine isiyo na masilahi kwa taifa lazima wachukuliwe hatua za kisheria.