walivyoruhusu watu wakatafute kazi popote walifikiria inashindikana?
"Bora uishi kama mbwa ughaibuni kuliko mtu tanzania'
kwani ukishakuwa Dr unapewa paspoti? Umeuliza swali la kijinga sana!
Madaktari wameamua kujiunga na wadandia meli kwenda kuwa wabeba mabox ughaibuni kulikomchosha Le Mutuz, jambo zuri watajifunza mengi maana wakiwa Tanzania tu wanakuwa na ndito za ajabu ajabu. Huko waendako kodi watakayokokotolewa watajua kuzaliwa. Wawaulize wabeba mabox yanayowakuta, lakini licha ya hayo kidogo kinaingia mfukoni kuliko bongoland.
Huwa naheshimu hoja zako,lakini hii ndugu umepotoka. Kuna watu wanabeba mabox Ulaya na America,lakini daktari aliyefuzu eti anabeba box huyo atakua na tatizo jingine! !! Usiongozwe na hisia wakati wa kuchangia sredi kama hii bali angalia mambo kwa mapana. Mwisho wa mgogoro huu sisi kama taifa/serikali yetu tutashindwa!
Wabeba box tunaozungumzia kila siku ni maprofesa, madaktari, manesi na wengine wengi tu katika fani mbalimbali, wabeba mabox ni msamiati ambao kwa sasa unamaanisha wafanya kazi ughaibuni. Wengi welioughaibuni wamepokea msamiati huu, wala hauwaumizi kwani waliouibua kuna yaliyowashinda huko na kuishia Fedex au UPS hivyo kujega hisia kwamba wote walioko majuu ni wa mtindo huo.
Tukubali tu kuupokea msamiati hii, na nimeingiza hii kwa makusudi kutifua wale wanaochukia msamiati wa wababa box.
Mkuu tatizo ni hivyo vigezo walivyoweka ili mtu apate hiyo hati ya kusafiria. So, inakuwa ngumu kuwa na hati kabla hujapata uthibitisho wa safari. Wewe vipi, ya kwako ulipewa kimagumashi nini? [MENTION][/MENTION]wapi nilipouliza swali?nani amesema ukishakuwa mganga tanzania unapewa hati ya kusafiria?usikurupuke na kufanya kila mtu aujue upumbavu wako.
Hoja hapa ni daktari wa kibongo kutokujua umuhimu wa kuwa na hati ya kusafiria mpaka apate matatizo
Nashauri wasikimbilie ulaya wala nchi jirani wabanane hapa hapa ila akija mgonjwa hospital wamchunguze Kama ni gamba wam mwakyembe tuu au au wamu moi. Operation ya goti wamkate shingo wa kichwa akatwe mkono na wa tumbo akatwe sehemu nyeti tena waanze ma mabalozi, wenye viti, madiwani mpaka wabunge ili majimbo yabaki wazi tuongeze nguvu bungeni na kwenye serikali za mitaa hapo watakuwa wametusaidia kupunguza muda wa mateso au vipi wadau? Ila baba nanihii najua hawata mpata maana anaruka viunzi ulaya kwa treatment ndogondogo Kama mafua etc