Bob_Dash
Member
- Nov 1, 2010
- 90
- 13
​Nimefuatilia sana safari za huyu Muhishimiwa Makamu wa kwanza wa Rais Dr. Mohammed Gharib Bilal anapokuwa kwenye safari za kikazi hapa nchini ama nchi za nje kila wakati lazima aambatane na eitha mke ama wake zake wote, ninajua wazi lazima gharama zote zitakuwa zinagharimiwa na kodi za wananchi, je hii ni sahihi? kuna ulazima gani kuambatana na wake zake kila mahala anapokuwa kazini? mbona hata viongozi wa mataifa tajiri huwa hawafanyi hivi, hii kitu huwa inanikera sana, mara nyingi kila ukiona picha za huyo muhishimiwa lazima utaona na picha za mke ama wake zake wote pia, narudia kuuliza, HII NI SAHIHI WAUNGWANA?