Huyu msanii huwa ananikera!!! ......

huyu jamaa nakumbuka kwa mara ya kwanza nilimuona ITV kipindi cha mizengwe pamoja na kina ****** na zembwela. katika scene nyingi za mwanzoni alikua akionekana kama FUNDI CHEREHANI, na kuna mdogo wangu alikua anasoma Reginald Mengi Primary School karibu na baa ya Mawela aliniambia kwamba alikua anamuona sana Wakuvwanga anashona nguo kwenye cherehani jirani na shule yao. nadhani sanaa sio fani yake, arudi kushona nguo!!
 
Acha usengerema kwani lazima uangalie? Kubwa zima kazi kuangalia vichekesho tu!!!! waachie watoto wewe kachakarike
 
unafugwa au yaani unapata mda wa kukaa na kuangalia vichekesho! Dume zima!! Wewe sii bure!?
 
huyu jamaa nakumbuka kwa mara ya kwanza nilimuona ITV kipindi cha mizengwe pamoja na kina mkwerè na zembwela. katika scene nyingi za mwanzoni alikua akionekana kama FUNDI CHEREHANI, na kuna mdogo wangu alikua anasoma Reginald Mengi Primary School karibu na baa ya Mawela aliniambia kwamba alikua anamuona sana Wakuvwanga anashona nguo kwenye cherehani jirani na shule yao. nadhani sanaa sio fani yake, arudi kushona nguo!!

kumbe katoka mbali toka enzi za mkwérè?
 
Nawasalimu wanajeiefu wote, straight to ze point ebwana huyu msanii anayeitwa WAKUVANGA wa kundi la ORIJINO KOMEDY huwa sioni anachokifanya zaidi ya kunikera!! kuchekesha kwenyewe hajui,anaforce fani ambayo sio yake. ushauri wangu kwa huyo jamaa angeenda kuimba taarabu na akina mzee yusuf ndio angependezea zaidi ......mwenye namba zake unipe nimpe MAKAVU LIVE.

chuki binafsi hizo, na si kila unachofanya lazima kila m2 akipende,
 
kweli binadamu tunatofautiana,usiusemee moyo, wewe anakukera lakini kwangu mimi waku is my best comedian
 
Tatizo bado hatujaweza kutofautisha kati ya talanta, karama na kipaji..............tunavamia tu...........hata yule vengu hakuwa na mojawapo kati ya hayo hapo juu lakini nakubaliana na hoja ya kuganga njaa.....
 
Tatizo bado hatujaweza kutofautisha kati ya talanta, karama na kipaji..............tunavamia tu...........hata yule vengu hakuwa na mojawapo kati ya hayo hapo juu lakini nakubaliana na hoja ya kuganga njaa.....

Kweli mkuu .........
 
Mkuu kila mtu anauwezo tofauti na mwenzake sio wote wanaweza kua sawa mfano joti kwa upande wangu namwona yuko juu kuliko wenzake thn masanja,mpoki,na wengine.ww anakukera wakuvwanga wengine watasema makregani ila wote wanafit katika pozisheni wanazowekwa mfano kwangu nlikua napenda sana segmet ya ndoa ndoano na wahusika walikua wanafiti sana japo kwengine wanapwaya.
 
Mkuu kila mtu anauwezo tofauti na mwenzake sio wote wanaweza kua sawa mfano joti kwa upande wangu namwona yuko juu kuliko wenzake thn masanja,mpoki,na wengine.ww anakukera wakuvwanga wengine watasema makregani ila wote wanafit katika pozisheni wanazowekwa mfano kwangu nlikua napenda sana segmet ya ndoa ndoano na wahusika walikua wanafiti sana japo kwengine wanapwaya.

kwenye hiyo segment angecheza mwingine ndio ingekua poa zaidi mana yeyote angeweza kucheza, tena angecheza joti kama demu na mpoki mbona ndio ingenoga zaidi ........yule anajaza tu kundi na anakula jasho la wenzie bora wamuondoe tu!!
 
Back
Top Bottom