Huu ndio uandishi wa habari?

Donyongijape

JF-Expert Member
May 28, 2010
1,497
811
Nimekuwa nikifuatilia kwa makini taarifa za habari zinazotolewa na vyombo vyetu vya habari has kipindi hiki cha kampeni,televisheni,radio na magazeti.Pia Nimekuwa msomaji mzuri wa magazeti ya kila siku na yale yanayotoa habari kwa mtindo wa makala ( i mean kila wiki).

Kwa mawazo yangu,naona waadishi wa habari ndio wenye uwezo mkubwa wa kuweza kupotosha au kujenga jamii yetu kutokana na umuhimu wao katika kuhabarisha jamii.

Tatizo kubwa ninaloliona kwa waandishi wa habari na hata waahariri wao ni kutofanya Upembuzi yakinifu juu ya habari wanazozitoa,kwa lugha nyingine kutoa habari kwa USHABIKI. Kimsingi hili ndilo tatizo ni kubwa sana hasa kwa magazeti yetu haya ya kila siku.

Wanachofanya ni kutoa HABARI KAMA ILIVYOSEMWA BILA KUFANYA CRITICAL ANALYSIS NA KULETA KITU KILICHOKAMILIKA at the very first delivery kwa wananchi na MATATIZO yake wanakuja kuleta critics at a time habari ikiwa imeshaumiza jamii.

Nitatoa mifano michache ya karibuni:

> Tamko la majeshi:baada ya jeshi kutoa tamko lao,vyombo vingi vya habari vilitoa raw information kutoka kwa vyombo hivyo bila kuwa na chembe ya critical analsyis juu ya uhalali wa jeshi kufanya hivyo..kwa mawazo yangu waandishi wa habari zile walipaswa kufuata maoni ya wadau mbali mbali kisheria na katiba inasemaje,tume ya uchaguzi na wananchi kwa ujumla n.k kuona wao wanasemaje kabla ya kutoa habari zao. Wengi ambao hawaingii JF au hawakusoma na kusikia habari juu ya majeshi tangu siku ya Ijumaa watakuwa bado wana maswali mengi (ninaamini wapo wengi) na wengine bado wanaogopa hayo matamko.

> Tamko la Masheikh: Sijui kama hawa waliulizwa maswali na waandishi au walipotoa tamko waandishi wakaenda kuandika moja kwa moja bila kuhoji..Kimsingi Sheikh aliposema kwamba kuna viongozi wa dini wanataka watu wachague viongozi wa dini zao na ilkhali waandishi wote walikuwa informed kwamba hakukuwa na kiongozi wa dini aliyewahi kusema mchagueni fulani kwa sababu ni dini yetu,nilitegemea waandishi,ambao wao ndio wapata habari ya mwanzo kuhoji juu ya uhalali wa tamko hilo wakati hakuna kitu kama hicho..Kilichotokea kesho yake na jioni ile..WAISLAMU WAKEMEA VIONGOZI WA DINI WANAOLETA UDINI...Hakuna hata critical analysis hata moja,eti mpaka baadaye muanze kuandika kwenye makala juu ya mapungufu ya habari ile..Why not the very first day?.

> Kuhusu REDET: Although habari haijatoka kwenye TV na magazeti kesho,lakini kubwa linalotarajiwa,REDET wasema JK kapata hizi,fulani kapata hizi...Magazeti mengi yataandika juu ya namna REDET walivyosema..Hakuna hata moja (Labda km litakuwepo) litakalotoa kutoa analysis ya ripoti ya REDET hata kama inaonekana ina upotoshaji ndani yake..Kimsingi kuna maswali mengi ndani ya ripot hiyo kama Je Peter Mziray wa APPT kwa nini hakujumuishwa,au kwa nini CCJ ijumuishwe wakati walishafutwa kabla hata ya Uchaguzi..na mengineyo mengi tu amabayo yatawafanya wananchi kupata picha halisi ya ripot yenyewe..!

Mwisho: Mimi nadhani Muda huu hasa reporting ya matukio makubwa kitaifa kama haya ya uchaguzi, waandishi (Hasa wale makini ambao hawajanunuliwa) hawapaswi kuandika habari kama walivyoipata..Ni muhimu kabla ya kuitoa waulize maswali ya msingi juu ya habari husika kwa mhusika lakini pia watafute maoni ya wananchi..Kwa Mfano, waweza andika kichwa cha Habari; REDET WATOA MATOKEO YAO; Lakini ukafanya utafiti wewe binafsi kabla ya kuchapicha habari hiyo na kusema,WANANCHI WAIKUBALI/WAIPINGA kutokana na sababu A,BA,CHE etc.Lakini kutoa tu habari alafu usubirie kesho yake ndio uandike critics kwa mtindo wa makala ambao wengi hawasomi..Umekwisha,unakuwa mwandishi uchwara..Jifunzeni CNN,Raisi/Mkuu wa jeshi etc anatoa tamko au habari inatoka hapo hapo wanaleta matukio yanayoendana na hilo au wanahoji wananchi na kupata pia maoni yao mapema kabisa. Kinachofuata ni habari kamili iliyojaa
 
safi, tathimini nzuri sana tena ungewataja hawa makanjanja kwa majina yao ukianza na habari corporation hawajawahi kuandika kwa weledi hata siku moja.
 
Nimekuwa nikifuatilia kwa makini taarifa za habari zinazotolewa na vyombo vyetu vya habari has kipindi hiki cha kampeni,televisheni,radio na magazeti.Pia Nimekuwa msomaji mzuri wa magazeti ya kila siku na yale yanayotoa habari kwa mtindo wa makala ( i mean kila wiki).

Kwa mawazo yangu,naona waadishi wa habari ndio wenye uwezo mkubwa wa kuweza kupotosha au kujenga jamii yetu kutokana na umuhimu wao katika kuhabarisha jamii.

Tatizo kubwa ninaloliona kwa waandishi wa habari na hata waahariri wao ni kutofanya Upembuzi yakinifu juu ya habari wanazozitoa,kwa lugha nyingine kutoa habari kwa USHABIKI. Kimsingi hili ndilo tatizo ni kubwa sana hasa kwa magazeti yetu haya ya kila siku.

Wanachofanya ni kutoa HABARI KAMA ILIVYOSEMWA BILA KUFANYA CRITICAL ANALYSIS NA KULETA KITU KILICHOKAMILIKA at the very first delivery kwa wananchi na MATATIZO yake wanakuja kuleta critics at a time habari ikiwa imeshaumiza jamii.

Nitatoa mifano michache ya karibuni:

> Tamko la majeshi:baada ya jeshi kutoa tamko lao,vyombo vingi vya habari vilitoa raw information kutoka kwa vyombo hivyo bila kuwa na chembe ya critical analsyis juu ya uhalali wa jeshi kufanya hivyo..kwa mawazo yangu waandishi wa habari zile walipaswa kufuata maoni ya wadau mbali mbali kisheria na katiba inasemaje,tume ya uchaguzi na wananchi kwa ujumla n.k kuona wao wanasemaje kabla ya kutoa habari zao. Wengi ambao hawaingii JF au hawakusoma na kusikia habari juu ya majeshi tangu siku ya Ijumaa watakuwa bado wana maswali mengi (ninaamini wapo wengi) na wengine bado wanaogopa hayo matamko.

> Tamko la Masheikh: Sijui kama hawa waliulizwa maswali na waandishi au walipotoa tamko waandishi wakaenda kuandika moja kwa moja bila kuhoji..Kimsingi Sheikh aliposema kwamba kuna viongozi wa dini wanataka watu wachague viongozi wa dini zao na ilkhali waandishi wote walikuwa informed kwamba hakukuwa na kiongozi wa dini aliyewahi kusema mchagueni fulani kwa sababu ni dini yetu,nilitegemea waandishi,ambao wao ndio wapata habari ya mwanzo kuhoji juu ya uhalali wa tamko hilo wakati hakuna kitu kama hicho..Kilichotokea kesho yake na jioni ile..WAISLAMU WAKEMEA VIONGOZI WA DINI WANAOLETA UDINI...Hakuna hata critical analysis hata moja,eti mpaka baadaye muanze kuandika kwenye makala juu ya mapungufu ya habari ile..Why not the very first day?.

> Kuhusu REDET: Although habari haijatoka kwenye TV na magazeti kesho,lakini kubwa linalotarajiwa,REDET wasema JK kapata hizi,fulani kapata hizi...Magazeti mengi yataandika juu ya namna REDET walivyosema..Hakuna hata moja (Labda km litakuwepo) litakalotoa kutoa analysis ya ripoti ya REDET hata kama inaonekana ina upotoshaji ndani yake..Kimsingi kuna maswali mengi ndani ya ripot hiyo kama Je Peter Mziray wa APPT kwa nini hakujumuishwa,au kwa nini CCJ ijumuishwe wakati walishafutwa kabla hata ya Uchaguzi..na mengineyo mengi tu amabayo yatawafanya wananchi kupata picha halisi ya ripot yenyewe..!

Mwisho: Mimi nadhani Muda huu hasa reporting ya matukio makubwa kitaifa kama haya ya uchaguzi, waandishi (Hasa wale makini ambao hawajanunuliwa) hawapaswi kuandika habari kama walivyoipata..Ni muhimu kabla ya kuitoa waulize maswali ya msingi juu ya habari husika kwa mhusika lakini pia watafute maoni ya wananchi..Kwa Mfano, waweza andika kichwa cha Habari; REDET WATOA MATOKEO YAO; Lakini ukafanya utafiti wewe binafsi kabla ya kuchapicha habari hiyo na kusema,WANANCHI WAIKUBALI/WAIPINGA kutokana na sababu A,BA,CHE etc.Lakini kutoa tu habari alafu usubirie kesho yake ndio uandike critics kwa mtindo wa makala ambao wengi hawasomi..Umekwisha,unakuwa mwandishi uchwara..Jifunzeni CNN,Raisi/Mkuu wa jeshi etc anatoa tamko au habari inatoka hapo hapo wanaleta matukio yanayoendana na hilo au wanahoji wananchi na kupata pia maoni yao mapema kabisa. Kinachofuata ni habari kamili iliyojaa

Uandishi wetu wa habari una aksi elimu yetu kwa ujumla. Elimu yetu haimjengei mwanafunzi uwezo wa kudadisi au kuuliza maswali (critical mind) bali kukariri majibu ya maswali ili apate maksi nzuri. Ndiyo maana unakuta mwanafunzi amefanya vizuri darasani na hata chuo kikuu ana 'first class' lakini mawazo na tabia yake haviendani na ufaulu alioupata. Yaani, huo ufaulu unabaki kwenye vyeti tu.

Waandishi wa habari wengi wanataka watoe habari inayowasisimua watu ili waonekane wameandika kitu cha maana bila kujali athari zake. After all, waandishi wanatafuta habari inayouza hata kama si ya kweli nia ikiwa kuongeza mauzo ya gazeti. Halafu wakijiwa juu, wanaandika 'apology' ukurasa wa kwanza. Upande uliochafuliwa ukiona hivyo, unaridhika na hiyo 'apology' kwani mwathirika hana muda wa kufikiri athari zake.

Wakati mwingine waandishi (na pia wahariri) wanashinikizwa na mwenye gazeti waandike habari yenye mlengo (angle) fulani kulinda maslahi ya mwenye chombo cha habari. Hili ndilo tatizo mama la uandishi wa habari Tanzania. Mfano, mwaka jana gazeti la Mwanahalisi lilishtakiwa Mahakama Kuu ya Tanzania kwa kwa kuandika habari iliyomhusisha Rostam na kampuni ya kufua umeme Richmond. Mdaiwa, ambaye lilikuwa gazeti la Mwanahalisi, hakuwepo mahakamani na hivyo mahakama kutoa hukumu hiyo ex parte (bila kuwepo upande unaodaiwa au lalamikiwa mahakamani ) kumlipa fidia Rostam Aziz 10bn/- (shillingi bilioni 10).

Kwa kawaida, hukumu ikitolewa ex parte huwa ule upande ambao haupo au haukuwakilishwa mahakamani unapewa muda kwenda kutoa sababu za kutokuwepo na unaweza pia kuiomba mahakama kubadilisha uamuzi wake kwa kutoa sababu kwa nini mahakama ifanye hivyo.

Lakini vyombo vya habari vinavyomilikiwa na mdai vilitoka na kichwa cha habari: 'Mahakama yamsafisha Rostam kuhusu Richmond' na kingine 'Court clears Rostam over Richmond' wakati vyombo vingine viliandika: 'Mahakama yaamuru gazeti la Mwanahalisi kumlipa Rostam 10bn/-'.

Kwa mfano huu, nataka tu nikubaliane na wewe kuwa uandishi wetu wa habari una walakini. Mfano, hata habari za kampeni zina matatizo mengi sana licha ya kuwepo semina mbalimbali zinazowasidia waandishi wa habari kujua ni kitu gani inabidi wakifanye na kitu gani inabidi waepuke. Vyombo vya habari vyote vimepata 'Media Election Code of Conduct' inayosema ni vitu gani wanapaswa wavifanye na vitu gani wanapaswa wasifanye wanapoandika habari za uchaguzi.

Lakini unaona uandishi wenyewe unavyoenda na hata mtu unajiuliza kama pamoja na workshops na semina zote, achilia mbali vyuo walivyopitia waandishi wa habari, wanaandika hivyo, je bila semina na hizo workshops za mara kwa mara wangeandika namna gani? Hivyo, ni kweli kuna tatizo kubwa sana. Lakini binafsi naona linatokana na elimu yetu kuanzia ya msingi hadi chuo kikuu. Of course, matatizo mengine yapo pia kama vile kuingiliwa na wamiliki wa vyombo vya habari na rushwa kutokana na malipo kidogo wanayolipwa na hivyo wanapoahidiwa fedha wako tayari hata kuharibu taaluma yao. Angalizo: Si waandishi wote wako hivi lakini wengi wana mwelekeo tunaouongelea hapa!
 
Nimekuwa nikifuatilia kwa makini taarifa za habari zinazotolewa na vyombo vyetu vya habari has kipindi hiki cha kampeni,televisheni,radio na magazeti.Pia Nimekuwa msomaji mzuri wa magazeti ya kila siku na yale yanayotoa habari kwa mtindo wa makala ( i mean kila wiki).

Kwa mawazo yangu,naona waadishi wa habari ndio wenye uwezo mkubwa wa kuweza kupotosha au kujenga jamii yetu kutokana na umuhimu wao katika kuhabarisha jamii.

Tatizo kubwa ninaloliona kwa waandishi wa habari na hata waahariri wao ni kutofanya Upembuzi yakinifu juu ya habari wanazozitoa,kwa lugha nyingine kutoa habari kwa USHABIKI. Kimsingi hili ndilo tatizo ni kubwa sana hasa kwa magazeti yetu haya ya kila siku.

Wanachofanya ni kutoa HABARI KAMA ILIVYOSEMWA BILA KUFANYA CRITICAL ANALYSIS NA KULETA KITU KILICHOKAMILIKA at the very first delivery kwa wananchi na MATATIZO yake wanakuja kuleta critics at a time habari ikiwa imeshaumiza jamii.

Nitatoa mifano michache ya karibuni:

> Tamko la majeshi:baada ya jeshi kutoa tamko lao,vyombo vingi vya habari vilitoa raw information kutoka kwa vyombo hivyo bila kuwa na chembe ya critical analsyis juu ya uhalali wa jeshi kufanya hivyo..kwa mawazo yangu waandishi wa habari zile walipaswa kufuata maoni ya wadau mbali mbali kisheria na katiba inasemaje,tume ya uchaguzi na wananchi kwa ujumla n.k kuona wao wanasemaje kabla ya kutoa habari zao. Wengi ambao hawaingii JF au hawakusoma na kusikia habari juu ya majeshi tangu siku ya Ijumaa watakuwa bado wana maswali mengi (ninaamini wapo wengi) na wengine bado wanaogopa hayo matamko.

> Tamko la Masheikh: Sijui kama hawa waliulizwa maswali na waandishi au walipotoa tamko waandishi wakaenda kuandika moja kwa moja bila kuhoji..Kimsingi Sheikh aliposema kwamba kuna viongozi wa dini wanataka watu wachague viongozi wa dini zao na ilkhali waandishi wote walikuwa informed kwamba hakukuwa na kiongozi wa dini aliyewahi kusema mchagueni fulani kwa sababu ni dini yetu,nilitegemea waandishi,ambao wao ndio wapata habari ya mwanzo kuhoji juu ya uhalali wa tamko hilo wakati hakuna kitu kama hicho..Kilichotokea kesho yake na jioni ile..WAISLAMU WAKEMEA VIONGOZI WA DINI WANAOLETA UDINI...Hakuna hata critical analysis hata moja,eti mpaka baadaye muanze kuandika kwenye makala juu ya mapungufu ya habari ile..Why not the very first day?.

> Kuhusu REDET: Although habari haijatoka kwenye TV na magazeti kesho,lakini kubwa linalotarajiwa,REDET wasema JK kapata hizi,fulani kapata hizi...Magazeti mengi yataandika juu ya namna REDET walivyosema..Hakuna hata moja (Labda km litakuwepo) litakalotoa kutoa analysis ya ripoti ya REDET hata kama inaonekana ina upotoshaji ndani yake..Kimsingi kuna maswali mengi ndani ya ripot hiyo kama Je Peter Mziray wa APPT kwa nini hakujumuishwa,au kwa nini CCJ ijumuishwe wakati walishafutwa kabla hata ya Uchaguzi..na mengineyo mengi tu amabayo yatawafanya wananchi kupata picha halisi ya ripot yenyewe..!

Mwisho: Mimi nadhani Muda huu hasa reporting ya matukio makubwa kitaifa kama haya ya uchaguzi, waandishi (Hasa wale makini ambao hawajanunuliwa) hawapaswi kuandika habari kama walivyoipata..Ni muhimu kabla ya kuitoa waulize maswali ya msingi juu ya habari husika kwa mhusika lakini pia watafute maoni ya wananchi..Kwa Mfano, waweza andika kichwa cha Habari; REDET WATOA MATOKEO YAO; Lakini ukafanya utafiti wewe binafsi kabla ya kuchapicha habari hiyo na kusema,WANANCHI WAIKUBALI/WAIPINGA kutokana na sababu A,BA,CHE etc.Lakini kutoa tu habari alafu usubirie kesho yake ndio uandike critics kwa mtindo wa makala ambao wengi hawasomi..Umekwisha,unakuwa mwandishi uchwara..Jifunzeni CNN,Raisi/Mkuu wa jeshi etc anatoa tamko au habari inatoka hapo hapo wanaleta matukio yanayoendana na hilo au wanahoji wananchi na kupata pia maoni yao mapema kabisa. Kinachofuata ni habari kamili iliyojaa


kwa wale anaosomea sheria au uandishi wa habari nadhani watapata kuelewa nasema kitu gani,kuna sheria inayoguide vyombo vya habari 'media laws in tanzania" ukiangalia katika newspaper act ya 1976 kuna vipengele vinamfunga mwandishi kujihusisha na mambo ya vyombo vya ulinzi na usalama kama vile jeshi,usalama wa taifa nk sas nadhani waandishi wa habari hapa wameshindwa kuchmbua kwa kina kutokana na sheria hizo au pengine media police zao
 
Kwa Tanzania chini ya umbeya wa CCM ushauri wako umeangukia pua hakuna aliyeko kwenye vyombo vya habari atakayefanyia kazi ushauri wako mnono kutokana na miliki hizo kuwa ni za watu ambao walianzisha vyombo hivyo kulinda masilahi yao tu na wala siyo vinginevyo.
 
Mleta makala hii anahitajika kwenda mirembe kwani kwa utafiti nilionao aliwahi kukimbia pale mhimbiri wodi ya wale jamaa wapigao kelele!Angalia pumba anazoleta kwani ukizichambua hata chembe za mtama hazitoki!puuuuuuuuuuuuuuuH
 
new habari co .ltd wajinga tu wanajikomba kwa Rostom azizi mwizi aliyekubuhu na washirika wake jk lowassa na magabachori wengine washamba tu waandishi wa mtanzania na Rai hawamna lolote pamoja na mhariri wawo kanjajatu
 
Back
Top Bottom